Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w73 2/1 kur. 70-71
  • Je! Kweli Unataka Ufalme wa Mungu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Kweli Unataka Ufalme wa Mungu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • LO! MAGEUZI GANI YAPASWAYO KUJA!
  • ISHI SASA KAMA UTAKAVYOISHI WAKATI HUO
  • Kuwa Raia wa Serikali ya Mungu
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Ufalme wa Mungu—Je, Unapata Maana Yao?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Namna Ufalme wa Mungu Unavyoweza Kukufaidi Wewe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
w73 2/1 kur. 70-71

Je! Kweli Unataka Ufalme wa Mungu

KWA VYO vyote si kila mmoja angejibu “Ndiyo” swali hilo. Duniani leo ni mtu mmoja tu kati ya watu 3.6 ambaye hudai kuwa Mkristo au Myahudi katika imani, hivyo kuwa mwenye dini akubaliye Maandiko Matakatifu yanayosimulia juu ya ufalme wa Mungu. Zaidi ya hayo, sio washiriki wote wa dini za Kristendomu na dini za Kiyahudi kweli huikubali Biblia kama Neno la Mungu.

Lakini pengine wewe ni mmoja unayeikubali​—na tunatumaini hivyo. Kwani Biblia yenyewe inatoa msingi wa hakika wa kuamini kuwa hivi karibuni serikali ya haki itakuwa na uwezo juu ya dunia yote. Serikali hiyo ni ufalme wa Mungu. Kupitia kwa ufalme Mungu atajibu sala, “Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni.” (Mt. 6:10) Hii itakuwa lini? Maelfu ya miaka ya nyuma Biblia ilielekeza zaidi kwa siku zetu, ikieleza sana na kutabiri kuwa hiki kingekuwa ndicho kizazi ambacho serikali ya Mungu ingejitwalia madaraka kamili ya mambo yote ya dunia.​—Dan. 2:44; Mt. 24:3, 7-14, 32-34.

Tunaamini kuwa utakubali dunia yenye masumbufu, kuchafuka, uvunjaji wa sheria kwamba inataka ondoleo la huzuni ambalo laweza kuletwa na Mungu peke yake, na inataka hili upesi.

Lakini kuja kwa ondoleo la huzuni, Biblia inaonyesha kwamba kwa njia ya ufalme wa Mungu mageuzi makubwa lazima yafanywe, yakiwatia ndani wakaaji wote wa dunia. Je! unajua mageuzi hayo ni yapi? Je! unajua yatamaanisha nini kwako mwenyewe, namna gani yatageuza maisha yako na, zaidi, ni lazima yanageuza hata sasa?

Kwanza ya yote, fahamu kwamba ufalme wa Mungu unakuja kufanya​—si mapenzi ya waalimu wa dini za Kristendomu na za Kiyahudi, wala si mapenzi ya watu wote ambao pengine wamekuwa wakiombea kuja kwa ufalme wa Mungu​—lakini utakuja kutekeleza mapenzi ya Mungu duniani.

LO! MAGEUZI GANI YAPASWAYO KUJA!

Mageuzi makubwa lazima na yatakuja. Maandiko yenye kuongozwa na roho ya Mungu yalionyesha mbele milki ya ufalme wa Mungu kuwa ndimo “haki yakaa ndani yake.” (2 Pet. 3:13) Ni wazi kwamba hiyo itaonyesha mageuzi makubwa kwa mambo haya yaliyoko sasa. Kuhakikisha kuwa mapenzi yake yametimizwa, Mungu amempa Mwanawe Yesu Kristo uwezo kama mfalme, na juu yake imeandikwa: “Umependa haki, umechukia maasi; kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekutia mafuta.” (Ebr. 1:9) Kama mfalme, atahakikisha kwamba sheria ya Mungu ya haki inafuatwa kabisa. Hiyo itamaanisha nini?

Biblia inatuambia sisi mengine ya mambo yatakayokomeshwa kwa kufikilizwa kwa sheria ya Mungu. Katika 1 Wakorintho 6:9, 10 inasema: “Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti, wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang’anyi.” Vitendo vyote hivyo ni vibaya kwa maoni ya Mungu. Kwa hiyo havitavumiliwa katika utawala wa ufalme wa Mungu. Ingawa Mungu ni mvumilivu wa watu wanaojitahidi kutafuta kufanya mapenzi yake, wale wanaoendelea kufanya yale anayoyalaumu “hawataurithi ufalme wa Mungu.”​—Gal. 5:19-21.

Basi, unaweza kuona, sababu kwa nini watu wengi leo hawataki ufalme wa Mungu kutawala juu yao. Kwa kweli, huenda wakasema wanataka hali nzuri zaidi​—maisha bila vita, bila kupungukiwa uchumi, bila magonjwa na uvunjaji wa sheria kwa jeuri. Lakini hawataki kujiona wana wajibu kwa Mungu kwa njia ya maisha yao wenyewe. Ulimwengu ambamo mwenendo mwovu hauvumiliwi hauwapendezi wao. Huenda wakasema hawakubali uasi, lakini hiyo ni juu ya namna fulani tu za uasi. Wao si wapenda haki. Matokeo ni kwamba kwa kweli hawataki ufalme wa Mungu.

ISHI SASA KAMA UTAKAVYOISHI WAKATI HUO

Unaonaje juu ya mambo haya? Je! kweli unatamani kuona ufalme wa Mungu ukiondoa udhalimu wote katika dunia? Kama ni hivyo, umewekewa akiba ya baraka tele. Lakini, kupata mibaraka hiyo, yakupasa kuonyesha imani yako katika mpango wa Mungu kwa uzima na kuonyesha unapenda haki kwa kujitahidi kuishi kwa unyofu wa moyo sasa kulingana na Neno la Mungu. Hata sasa chini ya taratibu hii ya mambo lazima ‘tuvifishe viungo vya mwili wetu’ kwa habari ya matendo mabaya. Hata sasa ni lazima ‘tuyaweke mbali nasi haya yote’​—si uasherati tu bali vile vile “hasira, na ghadhabu, na uovu, na matukano, na matusi.” Haitupasi ‘kuambiana uongo.’ Lazima ‘kuvua kabisa utu wa kale, pamoja na matendo yake.’ Yatupasa ‘tujivike utu mpya,’ tukionyesha upendo wa kweli kwa Mungu na kwa wenzetu.​—Kol. 3:5-14.

Je! kweli hivi ndivyo unapenda kufanya? Kama ni hivyo, unaweza kufanyaje? Kwa ‘kufanywa mpya katika roho ya nia yako,’ kama Biblia isemavyo. (Efe. 4:20-24) Hili silo jambo la kuazimu mwenyewe kuwa tofauti na watu walio karibu yako. Zaidi ya azimio, ni lazima kujaza akili yako kwa kawaida na kweli safi na zenye kujenga imani zipatikanazo katika Neno la Mungu Biblia. Kulingana na Warumi 12:2, “msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanya upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.”

Kama kweli mtu anataka ufalme wa Mungu, je! si jambo la akili kujifunza yote awezayo juu yake, sheria zake na yanayotakiwa ili kupata uzima chini ya usimamizi wake wa haki? Je! hilo ndilo ungependa kufanya? Mashahidi wa Yehova watafurahi kukusaidia. Watafurahi kufika kwako, kila juma, bila gharama, kukusaidia kupata taarifa hii ya maana kutoka katika Neno la Mungu. Je! kweli unataka uzima chini ya ufalme wa Mungu? Basi, kwa vyo vyote julisha tamaa yako ya kujifunza zaidi juu yake. Mwulize ye yote wa mashahidi wa Yehova katika eneo lako, au uwaandikie wachapaji wa gazeti hili.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki