Uwe Chombo cha Matumizi Yenye Heshima
“Basi ikiwa mtu amejitakasa kwa kujitenga na hao [wasioheshimika], atakuwa chombo cha kupata heshima, kilichosafishwa, kimfaacho [mwenyewe], kimetengenezwa kwa kila kazi iliyo njema.”—2 Tim. 2:21.
1. Wakristo wanaonaje onyo la Maandiko: “Mashirika mabaya yanaharibu mazoea mazuri”?
WALE wanaotaka “wapate uzima ulio kweli kweli” wanafahamu maana na uzito wa onyo hili: “Mashirika mabaya yanaharibu mazoea mazuri.” Wanajua kwamba inawapasa wajitenge na mambo yasiyoheshimika na watu wasioheshimika, kwamba watu hao wanajidai kuwa watumishi wa Mungu ama sivyo.—1 Tim. 6:19; 1 Kor. 15:33, NW.
2. Kwa sababu gani imewapasa wazazi wahangaike sana juu ya kuenea kwa matumizi ya dawa zenye kulevya?
2 Katika shauri la matumizi ya dawa zenye kulevya, hatari kubwa zaidi iko kwa vijana. Kwa hiyo, daraka liko juu ya wazazi. Inawapasa wahakikishe kwamba wa-toto wao hawaambukizwi na mashirika wanayopata shuleni na kwingineko. Si kazi nyepesi kwa wazazi. Inawapasa wawe na maoni yanayofaa juu ya tatizo la dawa zenye kulevya na kujua namna ya kuwa-linda watoto wao. Kwa maana “nyumba hujengwa kwa hekima, na kwa ufahamu huthibitika.”—Mit. 24:3.
3. Ni sababu gani ambazo watumiaji wa dawa zenye kulevya wanatoa kwa wale wanaojaribu kuwashauri?
3 Watumiaji wa dawa zenye kulevya na wenye kuzifanyiza wanatoa sababu nyingi za kuonyesha wana haki katika kufanya hivyo. Wanajidai wanalo jambo jipya. Shauku hii ya kutumia dawa zenye kulevya inafikiriwa kuwa jambo jipya, la “kisasa,” njia mpya ya maisha au ya kumfikia mungu fulani, jambo ambalo wengine hawalijui. Wengine wanapojaribu kusema nao juu yake, wanasema: ‘Oh, basi, wewe hujui unalosema; wewe hujazijaribu bado.’ Wanasema, ‘Huwezi kuona uzuri, furaha, ufahamu unaopata.’ Je! ni lazima ujaribu dawa zenye kulevya ili ujue unalosema? Je! ni hivyo?
4. Je! ni kweli kwamba mtu ambaye hajazijaribu dawa zenye kulevya hajui lo lote juu ya matokeo yazo?
4 Je! karne hazijatupasha habari juu ya hili? Ebu itazame India; itazame China wakati wa miaka iliyopita. Kuharibika kwa tabia nzuri ya Wachina kwa sababu ya kuingizwa kwa afyuni polepole katika China, zaidi na Wazungu, ilikuwa ndiyo mojawapo ya sababu za Maasi ya Wachina ya mwaka wa 1901. Ebu angalia uharibifu wa tabia nzuri ulioletwa katika nchi hizi na dawa zenye kulevya. Ni shauri la historia. Basi, mtu ye yote anaposema juu ya dawa zenye kulevya, akiwa na mambo haya ya hakika, anajua analosema. Hakuna mtumiaji wa dawa zenye kulevya awezaye kusema kwa kweli hivi, ‘Huwezi kuniambia lo lote.’
5. Taja yallyotukia kuonyesha matokeo mabaya ya hashish, dawa namna moja ya bangi.
5 Bangi au kasumba si kitu kipya, na mambo ambayo inafanya yamejulikana kwa karne nyingi. Dawa hii inatengenezwa kutokana na mmea unaoitwa cannabis, inakotengenezwa namna nyingine ya dawa yenye kulevya inayoitwa hashish. Mara nyingi inaitwa hash na inatumiwa zaidi kuliko namna zote za dawa na wavutaji wa bangi. Asili ya neno “assassin” inashuhudia nguvu ya hashish kuchochea matendo ya jeuri. Neno hili la Kiingereza “assassin” linatokana na neno la Kiarabu hashashin, neno linalotumiwa kueleza juu ya Amri ya Wauaji wa Kisiri, amri ya Kiislamu iliyoanzishwa katika Uajemi wapata mwaka wa 1090 C.E. Wakati wa Vita vya Kidini, watu hawa waliwaogofya Wakristo na maadui wengine kwa mauaji ya kisiri, mauaji ya kidini yaliyofanywa kwa ulevi wa bangi au “hashish.”
MAONI YA YESU JUU YA KUEPA
6-8. Yalikuwa maoni gani ya Yesu juu ya kile ambacho kingemsaidia aepuke yaliyompata?
6 Yalikuwa maoni gani ya Yesu, njia yetu ya kumfikia Mungu, wakati alipopewa dawa zenye kulevya? Alipokaribia kutundikwa juu ya mti wa mateso walitoa kwake “mvinyo iliyotiwa manemane,” ambayo labda ingalimpumbaza akili na kupunguza maumivu kidogo. Habari inasomwa hivi: “Asiipokee.”—Marko 15:23.
7 Ni kwa sababu gani Yesu alikataa dawa yenye kulevya? Basi, kati ya watu wote, Yesu Kristo, ambaye kupitia kwa yeye Mungu aliviumba vitu vyote, alijua kwa hakika matokeo ya dawa zenye kulevya juu ya mishipa na akili. (Kol. 1:16) Hapa Yesu alikuwa akijaribiwa juu ya ukamilifu wake, uaminifu na unyofu kwa Mungu. Yeye alikuwa akijaribiwa vikali, na hakutaka akili zake zipumbazwe mara moja, kwa ajili ya kutuliza maumivu tu. Yeye alitaka awe macho afanye mapenzi ya Mungu. Ilikuwa roho ya Mungu ndiyo Kristo aliyotamani, si kujiona kwa uongo kuwa na ‘ufahamu mkubwa na kupanuka kwa akili.’ Yeye alijua kwamba dawa zenye kulevya, pahali pa kumsaidia, zingezuia hali ya kuwa karibu na Baba yake Yehova katika wakati huu ambapo alihitaji msaada wa Mungu kuliko wakati wote. Akili zilizopumbazwa na dawa zenye kulevya zisingemsaidia akaribie karibu zaidi na Yehova Mungu. Pahali pake, yeye alijua kwamba, kwa kupumbazwa na dawa, angeweza kuwa shauri moja na mashetani na kujipotezea mwenyewe na wanadamu kila kitu.
8 Yesu hakutafuta hata kidogo kitu cha kuwazika tu ili aepuke kupambana na matatizo. Yeye alikikubali “kikombe” ambacho Yehova alikuwa ameweka mbele yake akinywee. (Yohana 18:11) Mapema, wakati Petro alipojaribu kumzuia asiutimize na kuumaliza mwendo ambao Yehova ali-kuwa amemwekea, alijibu mara hiyo kwa kumwambia Petro hivi: “Nenda nyuma yangu, Shetani [adui]; u kikwazo kwangu; maana huyawazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu.” Yesu hakutaka arukwe akili na kuletwa chini ya utawala wa mashetani.—Mt. 16:21-23.
9. Ni jambo gani ambalo ni la lazima, ili tumfikie Mungu na kutumiwa na yeye?
9 Ili tuwe wenye kutumiwa na Mungu inatupasa tufanye mapenzi yake, na Mungu anataka mapenzi yetu yawe yenye nguvu ili tuweze kufanya mapenzi yake kwa moyo wetu wote, nafsi, akili na nguvu, zote. (1 Yohana 2:17) Ili tuyafanye ni lazima tuwe na akili timamu na wenye macho. (Efe. 5:17; Kol. 1:9) Mtume Petro alijifunza kwa Yesu na mwisho akaandika, akisihi hivi: “Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama Simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze. Nanyi mpingeni huyo, mkiwa thabiti katika imani.”—1 Pet. 5:8, 9.
10. Ni njia gani ambayo mashetani wanatumia ili wawatawale wanadamu, na dawa zenye kulevya zinatumikiaje kusudi hili?
10 Kwa upande mwingine, mashetani wanataka watupumbaze ili tusitende sawa-sawa. Wao wanataka wadhoofishe kutaka kwetu kufanya mema. Ndipo wanapoweza kututawala kwa vyepesi. Wanataka wazichafue akili zetu, wazielekeze kwenye mambo mengine ili kwa vyepesi ‘tufanye mambo yasiyopasa.’ (Rum. 1:28) Dawa zenye kulevya zaweza kuwa chombo cha mashetani ambacho wanatumia ili watimize haya. Jarida iliyochapwa na United States Department of Health, Education and Welfare inasema hivi juu ya bangi: “Mtu anayetumia bangi anaona vigumu zaidi kufanya maamuzi yanayotaka fikira safi. Na anajikuta mwenyewe akifuata kwa vyepesi zaidi mashauri ya watu wengine. Akifanya kazi yo yote inayotaka uamuzi mzuri na fikira zinachafuliwa na bangi.”
JE! KIZAZI HIKI Ki “TOFAUTI”?
11. Onyesha kosa la sababu ambazo watumiaji wa dawa zenye kulevya wanatoa ili kutegemeza wanayodhani kuwa “haki” yao ya kutumia dawa zenye kulevya.
11 Wale wanaopigania inayoitwa “haki” ya kutumia dawa zenye kulevya wanatoa sababu kama hizi, ‘Si mbaya zaidi kuliko sigara,’ au ‘Inaonyesha kwamba kizazi chetu ki tofauti.’ Vijana wengine katikati ya mashahidi wa Yehova wameambukizwa na mawazo hayo. Lakini sababu gani kulipinga onyo la Neno la Mungu na la kundi lake, ambalo sikuzote limemtumikia kwa uaminifu na linatuambia kweli juu ya dawa hizi? Inakubaliwa kwamba sigara inaharibu, sawasawa kama vile ulevi. Hata ikiwa bangi si mbaya zaidi kuliko sigara, basi, kuna faida gani katika mojawapo? Ikiwa wengine wanataka kufanya mabaya au kujiharibu wenyewe, sababu gani wewe ujiharibu mwenyewe?
12. (a) Je! Yesu alivutwa katika mwendo wake kwa sababu ya mazoea ya kizazi ambacho katika hicho aliishi? (b) Kwa sababu gani kusema ‘kizazi chetu ki tofauti’ siyo sababu ya kugeuka kuyafuata mazoea yao?
12 Yesu hakuharibika au kuacha adili zake ati kwa sababu kizazi chake kilikuwa kibaya zaidi kuliko vizazi vyote? Oh, walitoa sababu za kuonyesha walihesabiwa haki. Walidhani walikuwa na njia ya kumfikia Mungu. Lakini Yesu aliwauliza viongozi wao hivi: “Mtaikimbiaje hukumu ya jehanum?” (Mt. 23:33) Aliwaambia kwamba watu wa Sodoma walikuwa afadhali kuliko kizazi hicho. (Mt. 10:15) Na kwa habari ya sababu ya kwamba kutumia sana kwa dawa zenye kulevya ‘kunaonyesha kwamba kizazi chetu ki tofauti,’ hiki ndicho kizazi chenyewe ambacho Yesu Kristo alisema kingekuwapo duniani wakati “dhiki kubwa” ingeupata ulimwengu, na ambacho kingeharibiwa.—Mt. 24:21, 34; 2 Tim. 3:1-5.
13. Kwa sababu ya kuongezeka kwa ufisadi, wazazi wengine wanafanya nini?
13 Kizazi hiki kinaendelea kuwa kibaya sana hata kuna wazazi wengi wanaotaka wawaondoe watoto wao katika shule wakati wanapoweza kufanya hivyo kwa halali, kwa sababu ya kuongezeka kwa ufisadi. Wao wanaona afadhali kuwafundisha nyumbani. Wengi wanawatia moyo watoto wao watafute kazi ya kibarua, wawe wakijipatia mahitaji yao wenyewe. Wanataka vijana waone ubora wa mambo yaliyo ya maana na kuwa wanaume na wanawake wenye kutegemewa kweli kweli. Ndipo wanapowatia moyo waingie kazi ya kuhubiri kama mapainia.
MFANO WA WAZAZI JUU YA DAWA ZENYE KULEVYA
14. Ni maulizo gani ambayo wazazi wamepaswa wajiulize wenyewe juu ya mfano ambao wanaweka?
14 Katika shule nyingi watoto wanazungukwa na matumizi ya dawa zenye kulevya kwa kadiri ambavyo vijana wengine kati ya mashahidi wa Yehova wanaambukizwa. Ninyi wazazi, je! mnapendezwa sana na watoto wenu? Basi namna gani juu ya maisha yenu wenyewe—mfano ambao mnaweka? Je! mnakunywa vileo kwa anasa mno? Je! sikuzote mnazungumza juu ya kunywa? Au, bila sababu ya hitilafu ya mwili mnatumia vibonge vya kupunguza ratli, kwa sababu mnakosa kujiweza katika kula? Au, mnatumia vibonge vya kuwachangamsha zaidi kuliko ilivyo kawaida yenu?
15. Matumizi yenye mazoea ya dawa za kupunguza ratli na za kuchangamsha ni yenye hatari namna gani?
15 Daktari George R. Edison, wa Chuo Kikuu cha Utah, anasema kwamba “matumizi mabaya ya dawa za kupunguza ratli ndilo tatizo kubwa la matumizi mabaya ya dawa katika U.S. kuondoa miji mikubwa ambako mazoea ya kutumia dawa zenye kulevya yameenea sana.” Dawa za kupunguza ratli zaweza kuharibu sana ubongo. Mahali pengine madaktari wamependelea kupiga marufuku kutoa agizo juu ya matumizi ya dawa za kupunguza ratli.
16. Kuna hatari gani kubwa katika dawa za kutuliza neva na kuleta usingizi, na pahali pake, imempasa mtu atafute kutia moyo wapi?
16 Ndiyo, kuna matumizi ya halali ya utabibu ya dawa za namna nyingi za kutuliza maumivu ikiwa kunatukia ajali au ugonjwa usioponyeka. Lakini wazazi, je! ninyi mnatumia vibaya au kutumia mno dawa za kutuliza neva na kuleta usingizi ili kuepuka tu kupambana na matatizo ya kila siku? Hizi zinaweza kukufanya uzizoelee vibaya. Zinaweza kukuua kwa ghafula, zaidi ikiwa unachanganya dawa hizi za kutuliza neva na kuleta usingizi pamoja na kileo. Pahali pake, je! wewe hupati faraja na kutia moyo kutokana na Neno la Mungu ili upambane na matatizo ya kila siku? (2 Kor. 1:3, 4) Ukiwa mzoevu wa dawa hizo, usishangae ikiwa unajiona uko kama mama aliyeandika habari kwa idara ya televisheni na aliyesema hivi: “Ninaogopa sana. Binti yangu anajaribu dawa kwa sababu naona nyingine kati ya dawa zangu za kutuliza neva na kuleta usingizi zimekosekana.”
17. Je! tunaweza bila shaka kuzitumia dawa kwa sababu tu daktari ndiye ameagiza tuzitumie?
17 Labda utasema, ‘Lakini daktari wangu ndiye aliyeniagiza nizitumie.’ Mambo ambayo madaktari wanaagiza hayawezi kupokewa sikuzote bila kutiliwa mashaka, zaidi kunapokuwa na dawa zenye hatari. The Journal of the American Medical Association linaripoti hivi: “Watoto watukutu wanaopewa dawa za kutuliza wanakuwa na adabu bora katika darasa, ndivyo walivyosema madaktari waliokutana katika Boston.” Lakini katika hali hizo wazazi ndio wangetangulia kufanya bora kwa kutumia kanuni za Biblia za upendo na ufahamu na adabu inayofaa. Kufanya hivi kunaweza mara nyingi kuleta matokeo bora sana, kama ambavyo wazazi wengine wameona kuwa.
WAZAZI, IWENI MACHO
18, 19. Wazazi wanakutana na hali gani nzito, na imewapasa wafanye nini?
18 Ninyi wazazi, je! mnajua juu ya watoto wenu katika habari hii? Kwa sababu tu ya kwamba ni watoto wenu msijisemeshe wenyewe hivi, ‘Oh, wao wasingetumia dawa.’ Je! kweli mmesema nao juu ya dawa na hatari zake na mkajua namna watoto wenu wanavyoliona jambo hili? Je! mmetangulia kuwaonya juu ya mambo wasiyoyajua? Yaani, si onyo la ukali au kuogofya kwamba kutafanyika jambo fulani wakipatikana wakitumia dawa. Je! pahali pake, mmezungumza pamoja na watoto wenu, ili mjue hali na fikira zao? Hii inataka wakati, lakini ni wakati ambao msingeweza kuutumia katika njia nyingine bora kuliko hiyo, kwa maana maisha zao ni bora kwenu. Tena, huenda mambo ambayo watoto wenu wanafanya yakamaanisha uzima au mauti kwenu NINYI.
19 Basi, wazazi, mara kwa mara zungumzeni shauri hili pamoja na watoto wenu, kwamba mnaona wakitumia dawa zenye kulevya ama sivyo. Sisi sote tunafanya vita ili tuendeleze ukamilifu ili tupate uzima. Kupoteza ukamilifu maana yake ni mauti. Mikazo inatugandamiza zaidi, lakini wakati uo huo kwa fadhili Yehova analifanya ulizo kuwa wazi sana hata hakuna kitu cha kututia shaka. Ni shauri tu la kufanya ambayo Neno lake linasema. Lakini inatupasa tufanye sehemu yetu katika kuendeleza kujiweza na kuendelea kuwa katika njia inayofaa.
HARAKA
20. Kwa sababu gani ni jambo la hatari sana hata kuzichezea dawa, kwa mfano, ‘kuzijaribu angaa mara moja tu’?
20 Sasa sio wakati wa kuwa baridi, mzembe au kupumbazwa na dawa zenye kulevya. Huu ndio wakati wa hukumu ya mwisho juu ya ulimwengu huu. Cho chote kinachodhoofisha kujiweza, au kinachomfanya mtu awe mwenye kukubali mawazo kutoka kwa wengine bila kufikiri kuzuri, kinamnyang’anya kujiweza kwake mwenyewe. Anakuwa katika hatari kubwa. Roho ya ulimwengu inaendelea kuwa ya kishetani sana. Ikiwa mtu anachezea dawa zenye kulevya yu katika hatari kubwa ya kudhoofisha, ukamilifu wake. Kuikubali mara moja tu roho ya ulimwengu huenda kukamaanisha kuwa shauri moja na mashetani, na mauti.
21. Matumizi ya dawa zenye kulevya yanatufanya tuwe wenye kupatwa kwa vyepesi na mambo gani mabaya?
21 Bangi na dawa nyingine zenye kulevya, na vile vile unywaji wa bila kipimo wa vileo unadhoofisha sana uwezo wa kujizuia. Zinaharibu adili. Inakuwa vyepesi kwa mtu kupokea mawazo kutokana na mashirika mabaya. Ni mtego wa mashetani. Biblia inasema hivi: “Asiyetawala roho yake ni mfano wa mji uliobomolewa, usio na kuta.” (Mit. 25:28) Wakati ukuta wa mji wa kale ulipobomolewa, nguvu zake za kulinda zilitoweka. Ilikuwa vyepesi kushambuliwa na adui. Usisahau kwamba kuna mashetani na ndio adui zetu wa kwanza.
KUJICHANGANUA KWA KWELI NA HALI YA KIROHO
22. Je! ni lazima tuzitumie dawa zenye kulevya ili tujue yaliyomo katika akili na moyo wetu?
22 Kwa habari ya kwamba dawa zenye kulevya zinatoa hali ya kujichanganua, si kile kilichomo katika akili na moyo wetu wa kibinadamu ndicho kiletacho wokovu, bali, pahali pake, kile kilichomo katika akili na moyo wa Mungu. Mtume anasema hivi: “Kwa maana najua ya kuwa ndani yangu, yaani, ndani ya mwili wangu, halikai neno jema; kwa kuwa kutaka nataka, bali kutenda lililo jema sipati.” (Rum. 7:18) Je! ni lazima turushwe akili na dawa zenye kulevya na kinachoitwa kujichanganua ili tujue haya, hali Mungu Muumba wetu amekwisha kutuambia hivyo katika Neno lake?
23, 24. Tunaweza kupata kujichanganua wenyewe kunakotegemewa wapi, kwa uongozi unaofaa?
23 Ni kweli, ni lazima tujichunguze wenyewe na kuziweka akili na mioyo yetu katika njia inayofaa. Lakini ni Muumba, ajuaye zaidi kuliko sisi wenyewe, ndiye awezaye kutuambia la kufanya. Biblia inasema hivi: “Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.” Basi, humo ndimo tunamoweza kupata uchanganuzi wenye kutegemeka.—Ebr. 4:12.
24 Mungu, si dawa zenye kulevya, ndiye awezaye kutuongoza sisi tuishi maisha za kiroho. Tunaweza kusoma katika Wakorintho wa Kwanza 2:9-13, NW: “‘Jicho halijapata kuona na sikio halijapata kusikia, wala hayajapata kuwazika katika moyo wa mwanadamu ndiyo mambo ambayo Mungu amewatayarishia wale wanaompenda yeye.’ Kwa maana ni kwetu sisi Mungu ameyafunua kupitia kwa roho yake, kwa maana roho inachunguza mambo yote, hata mambo magumu ya Mungu.”
25, 26. (a) Tunawezaje kupata busara nyingi? (b) Ni neno gani ya mtume Paulo ambayo Mkristo anakana akitumia dawa zenye kulevya?
25 Basi, ikiwa twataka kuwa na busara nyingi, tutatafuta kwa bidii kuipokea roho ya Mungu kupitia kwa sala na funzo la Neno lake. Mtume anaendelea kusema: “Kwa maana ni nani kati ya wanadamu ajuaye mambo ya mwanadamu isipokuwa roho ya mwanadamu iliyo ndani yake? Hivyo, pia, hakuna mtu ambaye ameyajua mambo ya Mungu, isipokuwa roho ya Mungu.” Roho ya Mungu ndicho kitu peke yake kiwezacho kutufundisha sisi mambo ya Mungu.
26 Kwa hakika roho ya ulimwengu ndiyo inayowaongoza vijana wengi sana watumie dawa zenye kulevya. Wanataka wawapendeze au wapendwe na vijana wenzao wanaolingana nao. Hivyo Paulo anatangaza hivi: “Sisi tulipokea, si roho ya ulimwengu, bali roho inayotoka kwa Mungu, ili tupate kuyajua mambo ambayo kwa fadhili yametolewa kwetu na Mungu. Mambo haya tunayasema pia, si kwa maneno yanayofundishwa kwa hekima ya mwanadamu, bali kwa yale yanayofundishwa kwa roho, wakati tunapoyaunganisha mambo ya kiroho pamoja na maneno ya kiroho.”
27. Pahali pa kujaribu kuepuka uhakika, mashahidi wa Yehova wanafanya nini?
27 Mashahidi wa Yehova hawajaribu kuepuka uhakika. Wanaishi sasa kwa kusudi. ‘Wanazigeuza akili zao’ kutoka kwa njia ambayo zamani ‘walifanyizwa kwa mtindo wa taratibu hii ya mambo.’ (Rum. 12:2, NW) Mpiga muziki aliyekuwa ameishi maisha yasiyo ya kweli kwa kutumia dawa zenye kulevya alianza kujifunza Biblia pamoja na mashahidi wa Yehova. Washiriki wake walimdhihaki, wakisema: “Akili zako zinasafishwa.” Alijibu vizuri hivi: “Kwa namna akili zetu zilivyo, zahitaji kusafishwa vizuri.”
28. Wale wanaofuata njia ya Biblia wana tumaini bora kuliko wale wanaotafuta kuepuka kupitia kwa dawa zenye kulevya namna gani?
28 Ndiyo, mashahidi wa Yehova wamesafisha fikira zao. Wanafuata kweli ya maneno ya Biblia: “Utauwa hufaa kwa mambo yote; yaani, unayo ahadi ya uzima wa sasa, na ya ule utakaokuwapo baadaye.” Tena, wanajua, kama alivyosema mtume, kwamba ‘taabu yao siyo bure katika Bwana.’—1 Tim. 4:8; 1 Kor. 15:58.
29. (a) Warumi 14:17 linatuonyeshaje kwamba mambo kama dawa zenye kulevya hayawezi kutusaidia tupate baraka ya Mungu? (b) Mungu atawaonaje na kuwatumia wale wanaotaka sasa kusitawisha matunda ya roho yake?
29 Hivyo si kula au kunywa, au kuvuta bangi au kutumia dawa zenye kulevya kunakofungua njia ya kumfikia Mungu, bali ni ujuzi wa Biblia na kufanya mapenzi ya Mungu. Ingefaa sikuzote kufikiria yaliyoandikwa katika Warumi 14:17, wakati sababu kama zile za watumiaji wa dawa zenye kulevya zinapotolewa kwetu, kwa sababu sisi twajua ya kwamba si kile tulacho, tunywacho, tuvutacho au tukitiacho miilini mwetu kitufanyacho watumishi wa Mungu au kiletacho kibali chake. Mtume aliandika hivi: “Ufalme wa Mungu si kula wala kunywa [na labda iongezwe, kutumia dawa zenye kulevya], bali ni haki na amani na furaha katika [roho takatifu].” (Rum. 14:17) Kufuatia matunda ya roho ya Mungu, tutapatikana kwa matumizi yenye heshima ya Yehova. Yeye atatutayarishia mahali katika taratibu yake mpya.—2 Tim. 2:21.
—Kutoka The Watchtower, Mar. 15, 1973.
[Picture katika ukurasa wa 424]
Wazazi wanapotumia mno dawa kuliko inavyotakiwa, je! wanawawekea watoto wao mfano gani?
[Picture katika ukurasa wa 425]
Zungumza na watoto wako juu ya hatari za dawa zenye kulevya. Jua wanavyoona juu ya kuzitumia