Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w73 9/1 kur. 403-406
  • Je! Wewe Wazionaje Mali za Kimwili?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wewe Wazionaje Mali za Kimwili?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MALI ZENYE KULETA FURAHA KUBWA ZAIDI, INAYOKAA ZAIDI
  • MIFANO YENYE KUTIA MOYO
  • ONYESHA NGUVU NA HEKIMA
  • Wazionaje Mali?
    Kupata Faida Zote za Ujana Wako
  • ‘Jilinde na Kila Namna ya Tamaa’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Wewe Unaweza Kupataje Usalama wa Kweli?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Wewe ‘Umeacha Kuweka Hazina Duniani’?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
w73 9/1 kur. 403-406

Je! Wewe Wazionaje Mali za Kimwili?

Mambo ya hakika ambayo vijana wanataka kujua

JE! WAWEZA kuwazia nyumba iliyojaa kabisa maelfu ya zawadi nzuri za namna zote mbalimbali? Je! wewe ungependa kuishi humo na kupokea nyingi za hizo zawadi kutoka kwa baba yako kama kichwa cha nyumba hiyo?

Kwa kweli, tayari unaishi katika nyumba kama hiyo​—sayari hii Dunia​—na Yehova Mungu, Mpaji wa kila zawadi kamili, ameijaza na vitu vizuri mbalimbali. (Yak. 1:17) Kama vile mtunga Zaburi alivyoandika: “Ee [Yehova], jinsi yalivyo mengi matendo yako! Kwa hekima umevifanya vyote pia. Dunia imejaa mali zako.”​—Zab. 104:24.

Baba ye yote anayewapenda watoto wake kweli kweli anapata furaha katika kuwapa vitu na kuona wanavyofurahia zawadi yenyewe. Ndivyo ilivyo kwa Mungu kama Baba yetu wa kimbinguni. (Linganisha Mathayo 7:9-11.) Yeye alikusudia kwamba wanadamu wavifurahie kabisa vitu vyote vilivyomo katika dunia​—vyakula, mavazi, vito vya bei, mti na vyuma vya kutengenezea vitu mbalimbali, wanyama kwa faida ya wanadamu na matumizi katika kufanya kazi.

Lakini, la ajabu sana ni kwamba, kupata kwetu furaha yote kutokana na vipawa hivi vya kimwili​—kwa kweli, kupata kwetu furaha yote kutokana na maisha yenyewe​—kunategemea sana juu ya kutovifanya jambo lililo la maana zaidi katika maisha zetu. Je! hiyo yawezekanaje? Ni kwa maana kunayo mambo mengine yenye maana kubwa zaidi kuliko mali za kimwili.

Labda utakumbuka namna, ulipokuwa mdogo sana, ulivyochukizwa sana na huenda hata ulihamaki wakati mtoto mwingine alipotaka kuchezea kibaramwezi chako. Ukitazama nyuma, huenda ikawa nia hiyo yaelekea kuwa ya kipumbavu kwako sasa. Akili yako ya kuona mambo yenye maana zaidi imeendelezwa. Lakini ni vyepesi kurudia nyuma kwenye njia hiyo ya kitoto tusipojihadhari. Imetupasa tuendelee kujikumbusha wenyewe yaliyo ya maana kweli kweli katika maisha.

Bila shaka unawajua vijana fulani wanaotoa heshima nyingi sana kwa mali za kimwili. Kwa mfano, kwa wengine, kuwa na radio au tepu rekoda, au mavazi ya kipekee, kamera, pikipiki au, katika nchi zilizo tajiri zaidi, hata na gari lao wenyewe, ndicho kitu wanachoelekea kuthamini zaidi. Wengine wanapendezwa zaidi na vitu hivyo kuliko masomo yao, jamaa zao au kitu kinginecho chote. Huenda hata wakaelekea kuwadharau wengine, wewe ukiwamo, kwa sababu ya vile walivyo navyo kwa habari ya mali za kimwili. Je! hili ni jambo la akili?

Ebu tua na ufikiri. Je! kuwa kwako na mali za kimwili kama hizo ama kutokuwa nazo kunaleta tofauti yo yote kwako kwa kweli kama mtu? Je! wewe ni mtu bora iwapo unazo, au mtu mbaya zaidi iwapo huna? Kwa kweli, mali zilizo bora kupita zote, zile zinazoamua ubora wako kweli kweli kama mtu na ambazo zinaweza kukuletea uradhi na furaha, ni za namna nyingine. Je! waweza kuwaza ni vingine gani kati ya vitu hivi?

MALI ZENYE KULETA FURAHA KUBWA ZAIDI, INAYOKAA ZAIDI

Namna gani juu ya ujuzi? Linganisha ubora, kwa mfano, wa kujua lugha nyingine na kuwa na kinanda au radio. Ni kweli, ukiwa na vitu hivyo waweza kufurahia kuwasikia watu wengine wakizungumza na kuimba​—katika lugha yako. Lakini ukiwa na ujuzi wa lugha nyingine wewe mwenyewe waweza kuzungumza na watu kufikia milioni mia moja duniani zaidi ya uwezavyo kufanya kwa kutumia lugha unayoijua sasa peke yake. Kama ungepata pendeleo la kusafiri kwenye nchi nyingine, ujuzi kama huo ungezidisha furaha yako sana ya safari​—zaidi sana kupita kama ungebeba radio.

Ndivyo na kupata ujuzi wa Kujifunza namna ya kufanya mambo. Kujifunza namna kuwa mpishi mwema au mshoni au seremala mwenye uwezo au kuwa fundi wa kurekebisha mashine​—haya yangekuwa yenye ubora mwingi zaidi kwako katika kufanya jambo fulani linalofaa katika maisha yako, kwa ajili yako mwenyewe na kwa ajili ya wengine, kuliko kuwa na mali fulani za kimwili.

Bila shaka, ujuzi wenye ubora mwingi zaidi kupita wote ni ule wa Neno la Mungu. Kwa huo unaweza kuwaletea watu waliovunjika moyo na kukata tumaini faraja na tumaini, ndiyo, kwa njia ambayo muziki kutoka katika kinanda hauwezi wakati wo wote. Kwa kweli, hata unaweza kuokoa uhai kwa kutumia ujuzi wa kweli ya Mungu. Je! kunazo mali za kimwili unazoweza kufikiria zinazoweza kufanya hivyo? Si ajabu yule mtu mwenye hekima anawasihi vijana wanunue anachopendekeza anaposema: “Inunue kweli, wala usiiuze; naam, hekima, na mafundisho, na ufahamu. Baba yake mwenye haki atashangilia; naye amzaaye mtoto mwenye hekima atamfurahia. Na wafurahi baba yako na mama yako; na afurahi aliyekuzaa.”​—Mit. 23:23-25.

Vile vile fikiria namna ilivyo bora zaidi sifa njema kupita kuwa na mali za kimwili. (Mit. 22:1) Ikiwa unajulikana kama asiye mchoyo, mwaminifu, mwenye bidii, mwenye kutegemeka na mwenye heshima, hiyo inaweza kukufanya wewe mtu wa kupendeza zaidi kuliko ambavyo mavazi yo yote ya namna ya pekee yanavyoweza kufanya. Sifa kama hiyo inaweza kufanya utafutwe kama rafiki bora au kama mfanya kazi mwenzi wa wengine. Inaweza kuleta makaribisho kutoka kwa watu uwatembelee au ufanye mambo pamoja nao, kushiriki mambo yao mzuri pamoja nao. Je! hii isingeuondoa ugumu wo wote wa upweke kwa njia bora zaidi kupita televisheni?

Kwa kweli, furaha yetu nyingi katika maisha inategemea kuwa na uhakika wa kwamba tunafurahiwa, kwamba wengine wanapendezwa nasi, kwamba tunaongezea maisha zao kitu fulani ambacho wangekikosa kama tusingalikuwa hai. Kuwa mwenye wingi wa sifa njema kutakufanya ufurahiwe zaidi sana na watu bora kupita kuwa kwako tajiri katika mali za kimwili. Ni kama vile kitabu cha misemo yenye hekima kinavyosema: “Apendaye usafi wa moyo, na neema ya midomo; mfalme atakuwa rafiki yake.” “Afadhali maskini aendaye katika unyofu wake, kuliko mpotofu wa midomo aliye mpumbavu. Haja ya mwanadamu ni hisani yake; ni afadhali maskini kuliko mwongo.”​—Mit. 22:11; 19:1, 22.

Kijana Timotheo alikuwa na pendeleo la kuchaguliwa afuatane na mtume Paulo katika safari zake za umisionari. Hii haikuwa sababu ya mali za kimwili za Timotheo lakini kwa sababu ya sifa zake njema, zilizotajwa na Wakristo katika miji miwili ya Asia Ndogo. (Matendo 16:1-4) Ujuzi alioupata Timotheo kama matokeo ulikuwa wa ajabu na nyumaye ulimstahilisha kuchukua migawo ya pekee kama mtu ambaye angeweza kutumainiwa sana na mtume. Kwamba Timotheo hakuzifanya mali za kimwili jambo la maana zaidi katika maisha yake inaonekana kutokana na maneno ya Paulo yaliyosemwa alipokuwa akimtuma Timotheo kwenye kundi katika Filipi katika Makedonia: “Sina mtu mwingine mwenye nia moja nami, atakayeiangalia hali yenu kweli kweli. Maana wote wanatafuta vyao wenyewe, sivyo vya Kristo Yesu. Ua mwajua sifa yake, ya kuwa [Timotheo] ametumika.”​—Flp. 2:19-23.

Je! rafiki za kweli si bora zaidi sana kupita mali za kimwili? Ni kweli, mtu anapokuwa na mali fulani za kimwili huenda zikaelekea kutoa “sifa” nyingi katika vikundi vya vijana, na huenda wengine wakamiminika kuzifurahia, kama vile mainzi wanavyomiminikia chakula. Lakini chakula kisipokuwapo, mainzi wanakwenda. Na wengi waitwao “rafiki” ndivyo walivyo. Ndivyo mwana mpotevu alivyoona wakati fedha yake ilipokwisha. (Luka 15:11-16) Huenda ukawa una kinanda au hata gari na huenda hii ikawavuta vijana wengine kwako. Lakini namna gani kama ukipoteza mali hiyo yenye kuvuta au namna gani kama mtu mwingine akipata kinanda bora cha kisasa au gari la kupendeza zaidi, ni wangapi wa “rafiki” hao watakaobaki nawe?

Lakini rafiki za kweli watakufurahia wewe kwa namna ulivyo wala si kwa vile ulivyo navyo. “Rafiki hupenda sikuzote; na ndugu amezaliwa kwa siku ya taabu.” (Mit. 17:17; 18:24) Zaidi ya hayo, Yehova mwenyewe atakuwa rafiki yako ukiufanya utumishi wake jambo la maana zaidi katika maisha yako, na “njia za mtu zikimpendeza [Yehova], hata adui zake huwapatanisha naye.”​—Mit. 16:7.

Vile vile, kumbuka kwamba vitu kama ujuzi, utu mwema na rafiki za kweli ni vitu visivyoweza wala kuibwa wala kuchakaa wala kupoteza ubora wavyo nyuma ya muda fulani au matumizi. Lakini watu wanaweza kuziiba au kuziharibu mali zako za kimwili. Mwana wa Mungu kwa hekima alishauri hivi: “Jiwekeeni hazina mbinguni, kusikoharibika kitu kwa nondo wala kutu, wala wevi hawavunji wala hawaibi; kwa kuwa hazina yako ilipo, ndipo utakapokuwapo na moyo wako.” (Mt. 6:20, 21) Ukiwa na sifa njema na kuendelea kuwa nayo kwa Mungu, furaha yako ya wakati ujao i salama, hakika, na kwa wakati wake, katika taratibu yake mpya, utaweza kufurahia kabisa hazina yote ya vitu vizuri vilivyomo katika dunia hii.

MIFANO YENYE KUTIA MOYO

Unayo mifano ya ajabu katika Biblia ya watu wasioweka mali za kimwili kwanza katika maisha zao. Musa alikuwa mmoja. Akiwa alizaliwa Mwebrania lakini, kwa hali zisizo za kawaida, akalelewa katika nyumba ya binti Farao, alikuza maoni yanayofaa ya mambo yenye maana kama kijana. Alipokuwa mtu mzima, yeye “akakataa kuitwa mwana wa binti Farao; akaona ni afadhali kupata mateso pamoja na watu wa Mungu kuliko kujifurahisha katika dhambi kwa kitambo; akihesabu ya kuwa kushutumiwa kwake Kristo ni utajiri mkuu kuliko hazina za Misri; kwa kuwa aliyatazamia hayo malipo.” (Ebr. 11:23-26) Ni kweli, aliacha mengi ya kimwili. Lakini alipata mapendeleo ya ajabu katika kuliongoza taifa la Israeli kutoka Misri mpaka kwenye Nchi ya Ahadi, akiwapitishia sheria ya Mungu na kuandika vitabu fulani vya Biblia. Na hata baraka kubwa zaidi zinamngoja katika ufufuo katika taratibu mpya ya Mungu inayokaribia. Nani asiyemsikia Musa? Wote wanaweza kufaidika kutokana na maandishi yake yaliyoongozwa na roho ya Mungu katika Biblia. Lakini je! nani anayemujua Farao tajiri wa wakati huo ama binti yake? Na je! walitimiza nini wao ambacho kwa kweli kikawa na faida na matokeo yenye kuendelea?

Bila shaka, mfano ulio bora ni ule wa Mwana wa Mungu. Kama vile 2 Wakorintho 8:9 inavyosema: “Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake.” Mtume Paulo na wanafunzi wengine waliufuata mfano mwema wa Yesu. Paulo angeweza kujitaja mwenyewe pamoja na wenzi wake kama “maskini, bali tukitajirisha wengi; kama wasio na kitu, bali tu wenye vitu vyote.” (2 Kor. 6:10; linganisha Wafilipi 3:7, 8.) Kwa kusoma habari ya Matendo ya Mitume tu utafahamu namna walivyokuwa na maisha nyingi na zenye kupendeza. Kama Yesu alivyosema, kwa kweli “kuna furaha nyingi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.” (Matendo 20:35, NW) Utaona ndivyo ilivyo ukijihakikishia mwenyewe.

ONYESHA NGUVU NA HEKIMA

Kwa hiyo, basi, sababu gani uziache taratibu za kisasa za kibiashara pamoja na matangazo yake yenye nguvu nyingi yakukaze ukajenge maisha yako katika mali za kimwili? Sababu gani uzitajirishe na mwishowe ujifukarishe mwenyewe kwa habari ya mambo yenye faida kweli kweli katika maisha? Sababu gani usionyeshe nguvu kweli kweli za kuushinda mvuto wa mambo ya kimwili na kujitahidi kupata mengi uwezavyo katika maisha kwa kutafuta vitu vyenye ubora mwingi zaidi kuliko mali za kimwili?

Zaidi hii ni la lazima sasa. Unabii wa Biblia unaonyesha kwamba taratibu iliyopo, pamoja na biashara yake yote, inaukaribia mwisho wake. Ungekuwa mtego kwetu kukusanya vitu vya kimwili kupita kadiri, fikira zetu zikivutwa upande mwingine tusiione haraka ya nyakati zetu. Huenda tukajikuta tumetopea katika taratibu hii na kuondoshewa mbali pamoja nayo wakati Mungu atakapoiondoa na kuileta taratibu yake mpya. Ni kama vile Yesu alivyoonya: “Angalieni, jilindeni na choyo, maana uzima wa mtu haumo katika wingi wa vitu vyake alivyo navyo.”​—Luka 12:15; angalia mfano alioutoa katika mistari ya 16-21.

Si kwamba tusiwe na mali zo zote hata kidogo. Lakini hatutaki ziyaongoze maisha yetu. Na imetupasa tuweze kutofautisha kati ya mali zitakazozidisha furaha ya kweli na zile ambazo kwa kweli zaweza kutuzuia tusiupate mradi wetu.

Ziwe ni mali kadiri gani ulizo nazo, lifanye lengo lako kuzitumia kwa faida ya wengine na zaidi sana “mheshimu [Yehova], kwa mali yako.” (Mit. 3:9) Kwa maana “mali hazifaidi kitu siku ya ghadhabu; bali haki huokoa na mauti.”​—Mit. 11:4.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki