Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w73 9/1 kur. 406-407
  • Usiweke Kinyongo Moyoni

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Usiweke Kinyongo Moyoni
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Habari Zinazolingana
  • Yehova—“Mungu Anayetoa Amani”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Yakobo Alipewa Urithi
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Yakobo na Esau Wafanya Amani
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Mapacha Waliokuwa Tofauti
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
w73 9/1 kur. 406-407

Usiweke Kinyongo Moyoni

KILA mtu alionekana kufurahia karamu alipofika mwenye nyumba. Alisalimiwa kwa moyo na wote​—na wote isipokuwa mmoja. Sababu gani? Kwa maana miezi fulani mbeleni katika karamu ya kumwaga mtu fulani mwenye nyumba hakuangalia mkono wa mtu huyu alipotaka kumsalimu. Bila shaka alikuwa akiweka kinyongo moyoni, na namna alivyokuwa na moyo mzito alipomwona aliyemfanya awe na kinyongo!

Je! wewe pengine unakuza chuki kwa kuweka kinyongo moyoni, na hivyo kujisikia asiye na furaha wengine wote walio karibu yako wanapoelekea kuwa wenye furaha?

Namna lisivyo jambo la busara! Kwa kweli, kunazo sababu nyingi za kuonyesha inatupasa kutii shauri la Biblia kutoweka kinyongo moyoni: “Usifanye kisasi, wala kuwa na kinyongo juu ya wana wa watu wako; bali umpende jirani yako kama nafsi yako; Mimi ndimi [Yehova].”​—Law. 19:18.

Kwanza huwezi kuweka kinyongo moyoni juu ya mtu bila kutompenda huyo, na kutopenda kunaweza kuwa chuki. Biblia inasema nini juu ya hilo? “Kila amchukiaye ndugu yake ni mwuaji.” (1 Yohana 3:15) Kwa kweli, kunaweza kutokeza kuua kwenyewe, kama vile katika mfano wa waokokaji wawili katika bas iliyoanguka Belem, Brazil. Walipigana kwa kutumia visu, matokeo yakiwa kwamba mmoja aliuawa na yule mwingine akakamatwa kwa shtaka la kuua.​—New York Times, Julai 21, 1972.

Biblia inatoa mifano mingi juu ya yanayoweza kuletwa na kinyongo. Kutaja mmoja tu, tuchukue Esau. Aliweka kinyongo moyoni juu ya ndugu yake Yakobo kwa kuwa Yakobo alipata baraka ya mzaliwa wa kwanza, ambayo Esau alikwisha mwuzia. Kwa sababu hiyo, Yakobo alikimbilia kwa mjomba wake Labani mpaka, kama mama yake alivyosema, “ikuondokee ghadhabu ya ndugu yako.” Na, bila shaka, kama Yakobo asingalifanya hivyo, Esau, kwa chuki yake kwa sababu ya kutopokea baraka ya mzaliwa wa kwanza kutoka kwa baba yake Isaka, angalimwua. Ikawa kwamba, walipokutana tena nyuma ya miaka 20, Esau alikuwa amegeuza moyo, kwa kuwa tunasoma kwamba ‘Esau alikuja mbio kumlaki, akamkumbatia, na kumwangukia shingoni, akambusu; nao wakalia.’​—Mwa. 27:41-45; 33:4.

Huenda tukaona tumekosewa. Labda tulikosewa kweli, au huenda sisi tunakosea. Lakini ‘tusipolipiza kisasi’ kwa anayeelekea kuwa alitukosea, nyumaye labda jeraha linaweza kupona na yaliyopita tukayasahau.

Lakini namna ilivyo bora kuwa kama Yusufu, mwana mpendwa sana wa Yakobo! Wengine wa ndugu zake waliweka kinyongo moyoni juu yake kwa sababu alikuwa aliyependwa sana wa baba yake (na kwa sababu ya ndoto zake zilizoonyesha kwamba wangemwinamia yeye), na walikuwa karibu ya kumwua. Lakini kwa sababu ya kujitia ndani kwa Yuda aliuzwa utumwani kuliko hivyo, na mwishowe akaingia gerezani kwa kushitakiwa uongo. Lakini je! aliweka kinyongo moyoni juu ya ndugu zake kwa sababu ya ubaya huu wote uliompata? Hata kidogo. Mambo yalipogeuka na wakawa chini yake, pahali pa kulipiza kisasi, Yusufu aliwasamehe kwa kupenda.​—Mwa. 45:1-8; 50:15-21.

Je! wewe unataka kuwa kama nani? Kama wale walioweka kinyongo moyoni kufikia kutaka kuua, au kama Yusufu, aliyekuwa mwenye msamaha na rehema?

Kunazo sababu nyingi zinazoweza kumfanya mtu aweke kinyongo moyoni. Mtu anaweza kuona amekosewa kwa kuwa mwingine amesema maneno yasiyo na maana na ya kuchukiza. Au huenda ikawa mtu amepuzwa au kutojaliwa alipotaka kuonyesha urafiki. Au huenda mtu akachukia kwa kuwa inaelekea alikaripiwa isivyo haki au kwa ukali mno.

Labda umemsikia mtu mwingine akisema jambo la kuchukiza juu yako. Je! inawezekana kwamba kuna ukweli kadiri fulani na hiyo ndiyo sababu ukachukizwa namna hiyo? Ikiwa lilikuwa jambo lisilo na maana yo yote, sababu gani usitumie fadhili na kusamehe, ukimwona kama asiye na hatia kwa sababu huna uhakika? Huenda ikawa alipokwisha kulisema alifahamu kwamba ingalikuwa bora kutolisema, lakini bado anashindwa kukuambia hivyo. Kumbuka shauri la Yehova kwamba, tusipowasamehe wengine makosa yao wanayotufanyia, Mungu hatatusamehe tunayomfanyia.​—Mt. 6:12-15; 18:23-35.

Au mtu fulani amekudharau, kutokujali au kukujibu vikali? Wakati fulani mwanamke wa Kikristo mzee kwa miaka alimfikia mzee katika kundi la Kikristo na kumwuliza sababu alimdharau, kama alimwonea chuki jambo fulani, na ikiwa ndivyo, lilikuwa jambo gani. Alishangaa mshangao mkuu, kwa kuwa mwanamke huyu wa Kikristo alikuwa mmoja wa rafiki zake wakubwa na alimheshimu sana. Hakujua alikuwa amemdharau wakati fulani, kwa kweli, alikuwa amefurahia kumwona sikuzote. Lakini kisa hiki, nacho, kilimfanya mzee aendelee kufikiri. Kwa muda mrefu alikuwa ameweka kinyongo moyoni juu ya mwingine yeye alipodharauliwa​—kama ilivyoelekea kuwa. Sasa akafahamu inawezekana yeye vile vile alikuwa amekosea kama mwanamke huyu.

Vile vile huenda tukaona haikuwapo maana ya kukaripiwa au labda kulikuwa kukali mno. Hii inatukumbusha alivyosimulia mcheshi wakati fulani. Nyakati nyingine baba yake alimpiga kofi pasipo lo lote alilokuwa amefanya. Alipolalamika, baba yake alijibu: ‘Basi, hiyo ilikuwa ni kulipa ulilokuwa umefanya wakati fulani lililostahili kofi wala hukulipata.’ Sisi sote tunapaswa kukubali kwamba tumekosa mara kwa mara bila kukaripiwa. Halafu, tena, labda kunazo sababu zilizomfanya anayepaswa awe mkali mno; au huenda anaona ni haki kabisa kuliko tuonavyo sisi. Jiweke katika hali yake, na utaweza kusamehe na kusahau.

Kwa hiyo, jihadhari usije ukaweka kinyongo moyoni. Usiwe mwepesi wa kukosewa, “maana hasira hukaa kifuani mwa wapumbavu.” (Mhu. 7:9) Huwezi kuweka kinyongo moyoni bila kujiumiza mwenyewe na wengine. Na inaelekea utajiumiza si kwa kimwili peke yake bali vile vile na afya yako ya kiroho. Huwezi kufurahia ujamaa mwema na Mungu isipokuwa unakuwa na ujamaa mwema na ndugu yako wa Kikristo vile vile. Kwa kweli, upendo wetu kwa Mungu unajaribiwa na upendo wetu kwa ndugu zetu. Kama alivyosema Yohana mtume mwenye upendo kwa mkazo: “Asiyempenda ndugu yake ambaye amemwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hakumwona.” (1 Yohana 4:20, 21) Kwa hiyo na uwe mwenye hekima, uwe mwenye haki, uwe mwenye upendo, na hutaweka kinyongo moyoni.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki