Kujibidiishia Thawabu ya Uzima wa Milele
“Mkazidi sana kutenda kazi ya Bwana sikuzote, kwa kuwa mwajua ya kwamba taabu yenu siyo bure katika Bwana.”—1 Kor. 15:58.
1, 2. (a) Mara kwa mara vijana wanauliza maulizo gani, na kwa sababu gani? (b) Watu wengine wanakubali nini juu ya maisha zao za siku zilizopita? (c) Mtunga Zaburi na Yesu Kristo walisema nini juu ya uzima na takwa la haraka zaidi la wanadamu?
JE! KAMA nafasi ingetolewa kwako leo uanze njia mpya kabisa ya maisha, ungeikubali? Au unaridhishwa na kazi unayofanya na maisha unayoendesha? Mara kwa mara vijana wanawauliza wazee, ‘Kama ungekuwa na nafasi ya kuishi upya, ungefanya kazi ii hii unayofanya sasa, au ungechagua jambo tofauti? Ungetaka watoto wako wa kiume na wa kike wafanye kazi ile ile unayofanya?’ Maulizo haya ya kuchunguza ndiyo njia ya vijana ya kuamua kama kazi yako imekuwa ya kuthawabisha na kama ungekuwa mwendo unaofaa kwao kufuata.
2 Watu wachache, hata hivyo, watakubali walitumia maisha zao vibaya kwa kazi zisizo na maana, ijapokuwa namna maisha zao zimekuwa zisizothawabisha. Mtu mmoja wa namna hiyo, Andrew Carnegie, mwanamume aliyeonewa wivu kwa sababu ya utajiri wake, alisema: “Ningetoa mamilioni yangu yote, kama ningekuwa kijana na kupata afya. Kama ningeweza kufanya maafikiano ya Faust, ningefanya. (Faust alikuwa mchawi Mjeremani na mnajimu anayesemwa kuwa aliuza nafsi yake kwa Ibilisi ili apate ujuzi wa kilimwengu na uwezo.) Ningeuza cho chote kwa furaha niishi upya.” Lakini, ole! uzima wa milele hauuzwi. Ujana na afya haviwezi kununuliwa na utajiri. Labda wale watu kati ya wanadamu wanaojishughulisha sana wakichuma utajiri kana kwamba ni namna fulani ya dawa ndio wa kuhurumiwa zaidi sana. Kwa kuwa maisha yao ni ndoto tupu kabisa. Aliandika mtunga Zaburi mwenye uongozi wa roho ya Mungu: “Binadamu huenda tu huko na huko kama kivuli; hufanya ghasia tu kwa ajili ya ubatili; huweka akiba wala hajui ni nani atakayeichukua.” (Zab. 39:6) Akichunguza habari ii hii ya kuamua shughuli kubwa ya maisha, mfikiriaji mkuu kati ya watu wa nyakati zote, yaani, Yesu Kristo, alitoa wazi jibu katika maulizo mawili ya kuchunguza, akisema: “Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kupata hasara ya nafsi yake [au, uhai]? au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake [au, uhai]?” (Mt. 16:26) Takwa la haraka zaidi sana na la milele, kulingana na Yesu Kristo, si sifa ya kujulikana sana au utajiri, raha au mali, bali uhai wenyewe. Kila mtu katika dunia anapaswa kuwa akijibidiishia thawabu ya uzima wa milele. Je! wewe unafanya hivyo?
3, 4. (a) Maelfu ya watu wanafanya nini leo, wakifanya nini kuwa lengo lao? (b) Kuwa mwanafunzi wa Kristo kunataka nini, kwa kutazamia thawabu ipi?
3 Kwa kweli mamia ya maelfu ya watu kila mahali leo wanafikiria kwa uzito maneno ya Yesu juu ya uzima. Wanajibidiishia sasa thawabu ya uzima wa milele kwa kuitikia njia mpya ya maisha kwa kumwiga Yesu Kristo. (1 Pet. 2:21) Miaka mitatu tu iliyopita, 1969,1970 na 1971, kutoka katika nchi 207, jumla kubwa ya watu 434,906 wamefurahia mageuzi makubwa katika maisha zao kwa kujifanya wenyewe kustahili thawabu ya uzima wa milele. Wameweka maisha zao wakf kwa Yehova Mungu na wameonyesha wakf huo kwa kuzamishwa katika maji. Shughuli za kimwili zimewekwa nyuma nao. Wameweka moyoni ombi la Yesu: “Msikitendee kazi chakula chenye kuharibika, bali chakula kidumucho hata uzima wa milele; ambacho Mwana wa Adamu atawapa.” (Yohana 6:27) Ingawa wanajitafutia wenyewe matakwa ya maisha, mambo haya siyo miradi yao mikubwa tena. Wanajua kwamba wakimtumainia Yehova kabisa atawapa matakwa ya maisha. Kwa hiyo wanautafuta kwanza ufalme wa Mungu na haki yake, na kama Mungu aahidivyo, mambo haya yanayotakiwa wanaongezewa.—Mt. 6:25-33.
4 Maisha haya kwa kumwiga Yesu Kristo yanataka imani. Ni kazi ngumu na inataka bidii na ustadi. Inataka kujitolea kwa kupenda, kupenda kushiriki ambacho ni cha mtu mwenyewe. Inataka uvumilivu, kazi hii ya kufanya wanafunzi wa Kristo wa watu wa mataifa yote. Lakini, mfanya kazi mwenye bidii anapata furaha katika kazi hii ya Mungu, kama mtunga Zaburi alivyotangaza: “Kuyafanya mapenzi yako, Ee Mungu wangu, ndiyo furaha yangu.” (Zab. 40:8) Kwa wasikilizaji wake, Yesu alisema: “Mkiyajua hayo, heri ninyi mkiyatenda.” (Yohana 13:17) Mtu asiyerudi nyuma katika kazi yenye bidii ya kuwa Mkristo atakuwa katika njia ya thawabu ya ajabu na ya kwanza—uzima wa milele.—Mt. 16:24, 25.
KARIBU KWENYE TENGENEZO LENYE BIDII LA YEHOVA
5. Katika kusanyiko la mwaka wa 1971 la New York, wanafunzi wenye tumaini wa Kristo walisalimiwaje na msemaji wa ubatizo, na aliwakaribisha kwenye kundi la namna gani?
5 Kwa wafanya kazi wa Kikristo, tukio kuu, lenye furaha kwa mwaka wa 1971 lilikuwa mfululizo wa ajabu wa “Jina la Kimungu” Makusanyiko ya Wilaya. Haya yalifanywa katika dunia yote. Mojawapo la mambo ya kusisimua yaliyoonwa katika haya makusanyiko ni kuona mamia, ndiyo, hata maelfu ya watu wakisimama na kushuhudia hadharani uamuzi wao kuchukua kazi ngumu ya kuwa mwanafunzi wa Yesu Kristo. Katika mojawapo la makusanyiko haya, katika New York, msemaji wa ubatizo aliwasalimu wenye kutaka kubatizwa kwa kusema: “Namna lilivyo jambo la kusisimua na kufurahisha kuona asubuhi ya leo hapa umati mkubwa namna hii wa watu ambao upendo wao kwa Yehova Mungu unawasukuma kufuata nyayo za Mwanawe mpendwa, Yesu Kristo! Kwa miezi mingi mmekuwa mkijifunza Biblia kwa utaratibu. Mmekuja kuikubali kama kitabu cha uongozi cha Mungu kwa viumbe vyake vya kibinadamu. Mmejifunza mafundisho yake ya msingi. Mmejua zaidi yanayotiwa ndani katika kuwa mtumishi wa kweli wa Mungu Aliye Juu Zaidi. Funzo lenu limetokeza matunda mema, kwa kuwa limezaa tamaa yenye nguvu katika mioyo yenu, tamaa ya kufanya ambayo viumbe vyote vyenye akili vya Mungu vinapaswa kwa haki kufanya—kuweka wakf maisha zenu kwa Mungu, kwa sababu hiyo mkiwa watumishi wake wenye hiari milele. . . . Tu wenye furaha kweli juu yenu na tunawakaribisha kwenye kundi la watumishi wenye furaha wa Mungu, wenye bidii, mashahidi wake.”
6, 7. (a) Mambo yamegeukaje katika maisha kwa wengi waliobatizwa, na walikaribishwa kushiriki katika kazi ya namna gani? (b) Ni kweli zipi zinazohakikisha kwamba wafanya kazi hawa wapya wamekuja katika tengenezo lenye shughuli?
6 Ndipo fikira zao zilipokaziwa kwenye tengenezo la duniani la Yehova lenye watu wenye shughuli sana. “Nyakati zilizopita wengi wenu,” msemaji akaendelea, “inaelekea sana, mmeona maisha yalikuwa hayana kusudi, utaratibu wenye ajali wa kumalizika mwishowe na ajali ile kubwa, kifo. Wengine wenu huenda wakawa walikuwa . . . wanajua kabisa kwamba maisha yamejawa na matendo yasiyo ya haki na vizuizi. Lakini sasa hayo yote yamegeuka kwa upande wenu. Mna sababu ya kuishi. Mmefahamu kwamba Yehova Mungu na Kristo Yesu wanaongoza kazi kubwa duniani kote siku hizi—na zaidi, kwamba wanatoa nafasi wazi kwa makutano ili kufanya kazi nao ya kutoa uzima, ya kugeuza maisha. Wafanya kazi pamoja na Mungu! Hilo halisikiki kama kuchukua mambo ivi hivi, sivyo?”
7 Wakati wa mwaka wa 1971, kwa mfano, wale walio katika tengenezo la mashahidi wa Yehova walitumia saa 291,952,375 wakiwaambia wengine juu ya Neno la Mungu, Biblia. Walifanya ziara za kurudia 133,785,116, kwa sababu walipendezwa na maisha za watu. Zaidi ya hayo, waliongoza mafunzo ya nyumbani ya Biblia kwa wengi wenye kupendezwa, wakiongoza, kwa wastani, mafunzo 1,257,904. Makutano haya ya watu walifanywa wanafunzi, na wote kwa kutii agizo ambalo Yesu aliwapa wafuasi wake: “Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza.”—Mt. 28:19, 20.
8. Sababu gani watu wa Mungu wanajibidiisha namna hiyo?
8 Sababu gani watu waliojiweka wakf wa Mungu wanajibidiisha namna hiyo? Ni kwa sababu moyo wao umo katika kazi ya Mungu. Wakf wao ni wa kweli. Walipochagua kuweka mapenzi ya Mungu kwanza katika maisha zao walimaanisha hivyo. Na mbali na hilo, wanakumbuka thawabu kubwa ambayo Mungu amewawekea—thawabu ya uzima wa milele! Kichocheo chenye nguvu namna gani hicho!
9. Sababu gani wapenda uzima wanapaswa kutaka kuungana na mashahidi wa Yehova?
9 Wapenda uzima wote wanapaswa kutaka kuungana na mashahidi wa Yehova. Na zaidi hivyo leo, kwa sababu tumebarikiwa kuwa tunaishi katika wakati wa takwa kubwa zaidi sana la wafanya kazi zaidi. Yakumbuke maneno ya Yesu alipowatazama watu kwa huruma na kusema: “Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache.” (Mt. 9:36-38) Sisi sasa tu katika sehemu ya kumalizia ya kazi nyingine kubwa sana ya kukusanya. Wapenda Mungu wanapaswa kutaka kushiriki katika kazi hii ya Mungu na kuvuna thawabu ya ajabu ya kazi zao za uaminifu, yaani, uzima wa milele.
10. Sababu gani nia ya haraka inapaswa kusitawishwa, na kwa nia gani kuelekea kazi iliyo mbele?
10 Kuna takwa, unapochukua kazi ya Mungu, kujua hatari, vikwazo, ambavyo vinaweza kutisha kukuondosha upande usifuate mwendo wa utumishi mwaminifu wa Mungu. Unataka kuwa na maoni yanayofaa ya kazi hii ambayo ni lazima ifanywe na ifanywe upesi kati ya sasa na “dhiki kubwa” itakayomaliza taratibu mbovu iliyopo ya mambo, na ni lazima uyashikilie maoni hayo yanayofaa. (Mt. 24:21) Lakini ni namna gani mtu anaweza kushikilia maoni hayo yanayofaa na asivutwe na mienendo ya kivivu au ya ubaridi ya watu wa kilimwengu au na watu wasio na imani?
KILA MARA KUWA NA MAONI YANAYOFAA YA BIDII YETU
11. (a) Ni kibali cha nani anachotafuta mfanya kazi wa Kikristo, na kwa sababu gani? (b) Ni nia gani kuelekea kazi inamwonyesha Mkristo wa kweli? (c) Paulo anatoa shauri gani?
11 Kwa kuwa Wakristo wa kweli ni watumishi wa Yehova na wameweka maisha zao wakf kwake kwa sababu wanampenda, inajalisha nini wanayofikiria watu wengine juu yao au kazi yao? Wanataka kibali cha Mungu. “Huku ndiko kumpenda Mungu, kwamba tuzishike amri zake.” (1 Yohana 5:3) Uvuguvugu kwa kuhubiri kwa Ufalme na kazi ya kufanya wanafunzi sio alama ya mtumishi wa kweli, aliyejiweka wakf wa Mungu. Pahali pake, ni bidii na shauku kushiriki katika kazi ngumu ya tengenezo kubwa la kutoa ushuhuda la Mungu vinavyowaonyesha Wakristo wa kweli. (Ufu. 3:16; Luka 13:24) Inatupasa tutake kufanya zaidi na zaidi, kila mara kuendelea katika kazi yetu iliyochaguliwa kama wafanya kazi pamoja na Mungu. (2 Kor. 1:24) Mtume Paulo, yule mfanya kazi asiyelegea, alikuwa na shauri linalofaa kwetu alipopendekeza: “Lo lote mfanyalo, lifanyeni kwa moyo, kama kwa [Yehova], wala si kwa wanadamu, mkijua ya kuwa mtapokea kwa [Yehova] ujira wa urithi.” (Kol. 3:23, 24) Angalia hilo! Yehova ndiye mthawabishaji. Ni kanuni yake ya utumishi tunapaswa kufikia. Je! hiyo haishauri kwamba tungeweza kufanya zaidi?
12. Upendo wa kweli kwa Mungu utamsukuma Mkristo kufanya nini?
12 Pahali pa kuwaiga walimwengu katika jitihada zao za kufanya kazi ndogo iwezekanavyo na kupata malipo zaidi iwezekanavyo, Mkristo anapaswa kuweka utumishi wa Mungu katika cheo cha juu zaidi na katika msingi imara zaidi, na kisha aendelee kufanya maendeleo sikuzote. (Flp. 3:16) Atajaribu kupendeza, si wanadamu, bali Mungu, anayepima mioyo yetu. (1 The. 2:4) Kama Kristo na mitume wake, hatajipendeza mwenyewe au kujiweka kando, lakini ataendelea kufanyia kazi kile ambacho Mungu anakubali.—Yohana 8:29; Matendo 20:31.
13. Sababu gani kazi ya Kikristo ya kukusanya ni ya haraka, zaidi hivyo sasa?
13 Ndipo, tena, kuna takwa la haraka kwa kazi ya Mungu ya kukusanya ifanywe, kwa kuwa wakati sasa ni mchache mbele ya mwisho kuichukua taratibu hii mbovu ya mambo na wote ambao wangali sehemu yake. Fikiri ni wengi namna gani wanaoweza kusaidiwa bado kuwa katika amani na Mungu na kusimama imara upande wake na kupambana na taratibu hii ya kale na mungu wake, Shetani Ibilisi. Wakati huu wenye nafasi unapoendelea kumalizika kwa haraka, je! ni nini unachoweza kufanya kuwafikia hawa watu na Neno la kuokoa la kweli la Mungu? Ni mwito wa kweli, usio wa kukosa.—Efe. 5:15-17.
JILINDE NA NGUVU ZENYE KUPINGA NA KULEGEZA
14. Mfanya kazi wa Kikristo anaweza kutazamia nini, na ni shauri gani lenye msaada tunapata katika Wagalatia, sura ya 6?
14 Ni lazima itazamiwe kwamba kazi ya Mungu na wafanya kazi wake ingeamsha hasira na chuki ya Shetani na tengenezo lake, na kwamba hawa, nao, wangewaweka Wakristo chini ya mikazo ya kila namna katika jitihada ya kumfanya Mkristo avunje ukamilifu kwa Mungu. Lakini kataa kuondolewa katika ujamaa wako uliowekwa wakf kwa Mungu, hata mwenzi asiyeamini wa ndoa, mshiriki wa jamaa yako mwenyewe au rafiki mkubwa awe ndiye chombo kile kile Ibilisi atatumia kukuvunja moyo. Hata ambapo wale ambao ni wafanya kazi wenzetu katika kundi la Mungu wanashindwa kwa njia fulani kukufariji na kukusaidia unapotaka sana, hiyo siyo sababu ya akili kuigeuzia kisogo kazi yenye heshima, ya maana ambayo Yehova amekupa. Pahali pake litegemee sana Neno la Yehova na utumainie ahadi zake kabisa. Uwe na uhakika kwamba wale wanaopanda kwa kiroho watavuna uzima wa milele kutoka kwa roho, wasipolegea.—Gal. 6:8-10.
15. Mawazo yenye mashaka yakitokea, tunapaswa kutafuta majibu ya nani? Ni mfano wa nani tunaoweza kuiga?
15 Mtu anapaswa kufanya nini Ibilisi akimsumbua akili kwa mawazo ya kutia shaka, mawazo kama haya: ‘Yote ni kazi bure? Kwa kweli mimi nafanya lo lote? Ninatazamiwa kufanya kazi hii yote katikati ya mikazo, upinzani na watu wenye dharau?’ Kumbuka, Yehova peke yake anaweza kutoa majibu yanayofaa, majibu ya kutegemewa, kwa kuwa ndiye aliyewaagiza watumishi wake wafanye kazi ya kufanya wanafunzi. Maulizo yanapotokea, ni majibu Yake unayotaka. (Mit. 3:5, 6; Mt. 7:7) Mkumbuke nabii Ayubu! Namna alivyoendelea kumheshimu Mungu kwa midomo yake katika majaribu makali ya imani yake. Mungu alimbariki vile vile kwa kufanya hivyo. Wakumbuke vile vile wale watu wa imani walioonyeshwa katika sura ya kumi na moja ya Waebrania na upate faida kutokana na waliyoona. “Angalieni, twawaita heri wao waliosubiri,” aliandika mwanafunzi Yakobo. “Heri mtu astahimiliye majaribu; kwa sababu akiisha kukubaliwa ataipokea taji ya uzima, [Yehova] aliyowaahidia wampendao.”—Yak. 5:11; 1:12.
KULIPA KUTOJALI KULIKOPITA KWA MAPENZI YA MUNGU
16. (a) Ni kukumbuka mambo gani kunakoweza kuwa kwa faida, na sababu gani? (b) Ni maneno gani ya mtume Petro tunaweza kuona ubora wake? (c) Mfano wa Yona ni wa kufaidi namna gani?
16 Ni vizuri mara kwa mara kutazama nyuma, kukumbuka hali yetu ya kwanza, mbele ya kuwa mtumishi wa Mungu, wakati ambao hatukuwa na Mungu na tumaini katika ulimwengu. Kukumbuka huko kunapaswa kuamsha tamaa yenye bidii ndani yetu kulipa kutojali huko kwa kwanza wakati ambao Mungu hakuwa katika mawazo yetu hata kidogo. Lakini tunawezaje kulipa kutomjali Mungu na mapenzi yake wakati uliopita? Kwa kujitahidi katika utumishi wa Yehova na hivyo kuhakikisha kwamba tunatubu kwa mambo yaliyopita. Petro anatusihi tutwae silaha hii ya nia inayofaa, ‘tusiendelee kuishi katika tamaa za wanadamu, bali katika mapenzi ya Mungu, wakati [wetu] uliobaki wa kukaa hapa duniani. Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuenenda katika ufisadi.’ (1 Pet. 4:2-11) Nabii Yona ni mfano mwema. Aliporudia hali yake na kujua namna alivyokuwa amesukumia mbali wajibu wake kwa Mungu, aligeuka, na tunamwona akitangaza kwa sauti kubwa: “Namcha [Yehova], Mungu wa mbingu, aliyeziumba bahari na nchi kavu.” Aliendelea kutangaza: “Lakini mimi nitakutolea sadaka kwa sauti ya shukrani; nitaziondoa nadhiri zangu. Wokovu hutoka kwa [Yehova].” (Yona 1:9; 2:9) Alikuwa na shauku ya kulipa kutojali kwake kwa wakati uliopita; na ndivyo tunapaswa na sisi.
17. (a) Wakristo wenye shughuli wanapaswa kukumbuka nini? (b) Paulo alionyeshaje kushughulika kwake juu ya jambo ili hili?
17 Kumbuka vile vile kwamba ingawa Yehova kwa fadhili anatuitia ushirika katika kazi yenye shughuli ya Ufalme, vile vile anatazamia tuendelee kuwa na mwenendo mwema katika namna zote za maisha. Kuwa mwenye shughuli katika utendaji wa kuhubiri, lakini wakati ule ule akiharibu kanuni yake ya adili, ingehakikisha kwamba mtu hatumikii kwa sababu ya upendo kwa Mungu. Kutumikia kwa nia isiyofaa kungeweza kufanya kazi yetu yote kuwa ya bure. Kwa hiyo tunapojishughulisha katika kazi ya Bwana, ebu kila mmoja na atafute kibali cha Mungu kwa njia zetu zote. Hili ndilo jambo aliloshughulikia mtume Paulo, ingawa alikuwa mfanya kazi imara, alipotangaza: “Nautesa mwili wangu na kuutumikisha [kwa kuuangalia sana]; isiwe, nikiisha kuwahubiri wengine, mwenyewe niwe mtu wa kukataliwa.”—1 Kor. 9:27.
18. Ni nini kinachoweza kumlinda mtu asije akakataliwa na Mungu?
18 Angalia usikataliwe, kwa kuuvaa huo utu mpya unaosemwa na Biblia. (Efe. 4:22-24; Kol. 3:9, 10) Ruhusu kumiminika kwa bure kwa roho ya Mungu kuongoze kila upande wa maisha yako ili kwamba matunda ya roho yajionyeshe wazi. Ndipo upendo, furaha, amani na matunda mengine ya roho yatakuwa na matokeo yenye kufaidi juu ya ujamaa wetu mtu na mwenzake. Uaminifu huo ulioazimiwa kwa upande wetu ni ushuhuda wa nia inayofaa na moyo safi katika utumishi wetu wa Mungu.—Gal. 5:16-25.
MAONI YANAYOFAA YA THAWABU NI KICHOCHEO CHENYE MSAADA
19. Sababu gani vile vile ni lazima kuwe na maoni yanayofaa ya thawabu?
19 Si maoni yanayofaa ya kazi ya kuhubiri tu yanayotakiwa, bali na maoni yanayofaa ya thawabu. Usikosee, kufanyia kazi thawabu kunaweza kweli kweli kupatanishwa na kufanya kazi kwa sababu ya upendo kwa Mungu. Namna gani hivyo? Ni Mungu aliyeweka thawabu na anatukaribisha tujitahidi tuipate. Katika Tito 1:2 twasoma: “Katika tumaini la uzima wa milele, ambao Mungu asiyeweza kusema uongo aliuahidi tangu milele.” Ni kwa kuwa na kipawa hicho kilichoahidiwa cha uzima akilini kwamba Mungu akamtoa Mwana wake mzaliwa wa pekee Yesu Kristo kama ukombozi, “ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.” (Yohana 3:14-16, 36) Ikiwa Mungu alitoa kipawa cha bei ya juu hicho, bila shaka anawapenda wale ambao watajitahidi kabisa wakipate. Na, mbali na hilo, Maandiko yaliyoongozwa na roho ya Mungu yanatuhakikishia kwamba “pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao [kwa bidii].” (Ebr. 11:6) Na thawabu hiyo ni nini? Kila mara kumbuka kwamba thawabu yenyewe ni uzima wa milele chini ya hali zenye haki katika taratibu mpya ya Mungu. Kwa hiyo, ichuchumie sasa thawabu, na ustahili kuipokea, hali kungali na nafasi.
20, 21. (a) Maisha katika taratibu mpya ya Mungu yatakuwaje? (b) Watu kila mahali watafurahia nini, wakiigeuza dunia hii kuwa nini?
20 Namna maisha katika taratibu mpya ya Mungu yatakavyokuwa tofauti na tuonayo leo! Sasa mtu anaweza kutumia saa nyingi akijenga nyumba na kutengeneza bustani nzuri, na kwa ghafula afe akiiacha kwa mtu mwingine. Lakini katika Taratibu Mpya iliyoahidiwa mtu atafurahia matokeo ya kazi zake kwa miaka isiyo na kikomo. Fikiria maajabu yote ya mbingu, bahari na nchi! Wanasayansi wenye maendeleo kupita wengine wamefukua juu tu katika jaribio lao la kutaka kujua hekima na kanuni ambavyo ndivyo msingi wa ulimwengu wetu wote. Thawabu ya uzima wa milele ambayo watumishi wenye kushika ukamilifu wa Mungu watafurahia itawapa nafasi ya kutosha kuchunguza maajabu haya yote ya uumbaji. Ndipo wakati utakuwapo wa kujifahamisha kabisa na wanadamu wenzetu wa mataifa yote na wanyama katika sehemu zote za dunia.
21 Lililo bora sana, watu kila mahali duniani watakuwa wakifurahia amani na uhuru kama watoto wa kidunia wa Mungu. Watakuwa huru na hofu inayosumbua taratibu hii ya kale ya mambo. Wataweza kumtumikia Yehova katika lo lote watakalofanya kwa mikono yao, kwa kuwa Mungu atahakikisha kwamba kuna kazi ya maana kwa wote. Hapana, si kazi zinazoleta mizigo au kuhatirisha maisha za wafanya kazi wake au wengine, bali kazi ambayo inakamatana na kumrudishia mwanadamu cheo chake na kuigeuza hii dunia kuwa paradiso ya bustani ya kupendeza.
22. Sababu gani si hekima kuwaza kupita kadiri juu ya taratibu mpya ya mambo inayokuja?
22 Kwa kweli, ni vizuri kujihadhari kutoruhusu kuwaza kunakopita kadiri unapofikiria hali katika Taratibu Mpya ambazo hazijaahidiwa na Yehova katika Neno lake Biblia. Hakuna lazima, kwa mfano, kujizoeza sasa kwa kazi fulani unayotumainia katika kipindi hicho kizuri mno, kwa kuwa wakati utakuwapo kupata mazoezi hayo na ujuzi. Chini ya utawala wa Ufalme wa Mungu watu watakuwa wakiishi katika taratibu ambamo hakutakuwa kukimbizana na wakati. Wakati bado utakuwa ukihesabu siku na miaka, lakini kutokwisha kwa uzima wakati huo kutafanya kusiwe na haraka.
23. Sababu gani wafanya kazi wa Kikristo wana uhakika juu ya thawabu, na ni mifano ya akina nani wanatakiwa kuiga?
23 Thawabu ambayo watu wa Mungu wanajibidiishia ni ya hakika, kwa maana imehakikishwa na Muumba mwenyewe, ambaye juu yake mtume Paulo alitangaza kwa matumaini: “Mungu si dhalimu hata aisahau kazi yenu, na pendo lile mlilolidhihirisha kwa jina lake.” (Ebr. 6:10) Kazi yako yenye juhudi katika kutangaza habari njema za ufalme wake, na kwa sababu hiyo kulishuhudia jina lake takatifu Yehova, haitapita bila kuthawabishwa. Kwa kuhakikishiwa ukweli huo, na uwe kama Ibrahimu aliyeshikilia kabisa imani yake katika neno la Mungu kwake: “Usiogope, Abramu, Mimi ni ngao yako, na thawabu yako kubwa sana.” (Mwa. 15:1) Vile vile, na uwe kama Mmoabu Ruthu aliyekubali kwa imani kabisa tumaini la ajabu lililotolewa kwake: “[Yehova] na akujazi kwa kazi yako, nawe upewe thawabu kamili na [Yehova], Mungu wa Israeli, ambaye umekuja kukimbilia chini ya mabawa yake.” (Ruthu 2:12) Wewe vile vile na upate nguvu na ushujaa utafute kimbilio chini ya mabawa yaliyokunjuliwa ya Yehova kama mfanya kazi mwenzake.
24. Sababu gani kazi ya Mkristo ndilo tendo kuu kupita yote, kwa kutazamia nini?
24 Unapoonyesha nia inayofaa kuelekea kazi usipunguze bidii yako lakini kuwa imara kila wakati ukazidi sana kutenda katika kazi ya Bwana, ukifanya zaidi na zaidi, ikiwezekana. (1 Kor. 15:58) Utumishi wetu kwa Mungu ndiyo namna ya juu kabisa ya kazi ambayo kwayo mwanadamu anaweza kujitolea. Ndilo Tendo kuu kupita yote. Linakamatana na Jina la Mungu wetu na Muumba, Yehova, na bila shaka hilo silo tendo la bure. Pahali pake, ni tendo la kufurahisha, na linalotoa ahadi kwa wale wanaoliendeleza kwa bidii ya maisha kamili na yanayoridhisha sasa na tumaini la uzima usiomalizika katika taratibu mpya ya Mungu inayokaribia sana. Na ustahili kuungana na sisi katika tendo hili la haraka sana sana kupita matendo mengine yote sasa.
—Kutoka The Watchtower, Aug. 15, 1972.