Je! Sala Zako Zinajibiwa?
JE! KUMEKUWA na nyakati ambapo ulimwomba Mungu na sala zako hazikujibiwa? Wengi wameona hali hii. Je! maana yake ni kwamba sala hazina maana?
Hapana, Mungu anaweza kusikia sala na kutenda zinavyouliza. Kwa kweli, mtumishi wa kale wa Mungu alikuwa na uhakika mwingi hivyo kwamba akaandika: “[Yehova] ameisikia dua yangu; [Yehova] atayatakabali maombi yangu.”—Zab. 6:9.
Sababu gani huyu mtumishi wa Mungu na wengine kama yeye walikuwa na matumaini kama hayo katika sala? Na, bado, sababu gani sala nyingi hazijibiwi?
KUTIMIZA MATAKWA YA MUNGU
Sababu ni kwamba Mungu ana matakwa ambayo wale wanaotaka kumkaribia ni lazima watimize. Mojawapo linakamatana na imani. Biblia inasema: “Mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao.” (Ebr. 11:6) Je! una imani ya kwamba Mungu kwa kweli yuko, na ya kwamba anaweza kujibu sala? Hii inatakiwa.
Matakwa mengine yalielekezwa kwayo na mwanafunzi wa Kikristo Yakobo alipoandika: “Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi. Itakaseni mikono yenu . . . [Jinyenyekezeni] mbele za [Yehova].” (Yak. 4:8-10) Kwa wazi, basi, ili kufurahia kusikiwa na Mungu mtu hawezi kwa makusudi kuvunja sheria za Mungu. Kuliko hivyo, mtu ni lazima atake kwa unyofu wa moyo kufanya yaliyo haki, kwa unyenyekevu kutaka kufanya mapenzi ya Mungu, na si mapenzi tu ya mtu mwenyewe. Je! wewe unafanya hivyo?
Ikiwa unafanya, Mungu atasikia sala zako. Kwa kuwa mtume wa Kikristo Yohana aliandika: “Tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia.”—1 Yohana 5:14.
Lakini mapenzi ya Mungu ni nini? Yanakamatana na kitakachowafaidi wanadamu zaidi. Biblia inasema kwamba ‘mapenzi ya Mungu ni kwamba wanadamu wa namna zote waokolewe na kuja kwenye maarifa yaliyo sahihi ya kweli.’ (1 Tim. 2:4, NW) Je! umekwisha omba ili uje katika “maarifa yaliyo sahihi ya kweli,” yaani, kweli juu ya Mungu na kusudi lake kwa wanadamu? Sala kama hizo zenye unyofu wa moyo zinasikiwa na Mungu.
SALA AMBAZO MUNGU AMESIKIA
Kuna mfano wa mkuu wa kijeshi wa Kiitaliano aliyeitwa Kornelio. Biblia inasema kwamba alikuwa “mtu mtauwa, mchaji wa Mungu,” na kwamba ‘alimwomba Mungu daima.’ Yehova Mungu alisikia sala zake, na akahakikisha kwamba mtume wa Kikristo Petro ameongozwa kwa Kornelio kumfundisha ili kwamba apate maarifa (ujuzi) sahihi ya kweli.—Matendo 10:1-5, 22-43.
Watafutaji wenye unyofu wa moyo leo vilevile wamejibiwa sala zao. Kwa mfano, mtaalamu wa moyo katika Afrika Kusini siku moja alivutwa kumwambia mkewe: “Kuna jambo moja tu ninalojutia katika maisha haya—kwamba tumewaleta watoto sita katika ulimwengu huu wasioamini kuwako kwa Mungu.” Hii ilimhimiza mkewe kumwomba Mungu: “Baba, tusaidie tukupate wewe.”
Siku mbili nyumaye mashahidi wa Yehova walifika mlangoni mwa mume huyu na mkewe. Kwa haraka mke wa daktari aliwakusanya watoto, na wote wakafurahia mazungumzo ya Biblia. Matembezi yaliyofuata yaliongoza kwenye funzo la kawaida la Biblia. Leo mwanamke mwenyewe ni shahidi aliyebatizwa wa Yehova, na mumewe na watoto wanaendelea kufanya maendeleo katika funzo lao la Neno la Mungu.
Nyakati nyingine majaribu na taabu kubwa za maisha zinawafanya watu wawe bila tumaini kabisa. Huenda hata wakajisikia vibaya sana mpaka wakafikiria kujiua. Je! watu kama hao wanaweza kusali kwa Mungu na kusikizwa? Kwa kweli wanaweza! Lakini imewapasa waombe kitu gani? “Maarifa sahihi ya kweli” juu ya Mungu na makusudi yake. Haya, bora kupita kitu kingine cho chote, yanaweza kuwasaidia kushindana na magumu yao. Mwanamke wa New Caledonia anasimulia namna ombi lake kwa msaada lilijibiwa:
“Nikiwa katika hali yenye wasiwasi ya kutaka kujiua, niliomba msaada katika barua wa mtu ambaye niliona angeweza kunisaidia—padre wangu. Lakini hakuitikia. Lakini, juma moja nyumaye mmoja wa mashahidi wa Yehova alinitembelea. Nilikubali msaada wa kujifunza Biblia, na mara tu mwanamke huyo alipoondoka nilisoma yaliyomo kwa bidii. Nyuma ya siku fulani nilianza kupata kitulizo cha akili na kuendelea kujiona huru.” Leo mwanamke huyu na mumewe wote ni mashahidi wa Yehova.
Lakini mtu anawezaje kujua iliyo kweli? Mwanamke wa Kikatoliki wa Msumbiji (Mozambique) alitembelewa na mmoja wa mashahidi wa Yehova. Mwanamke huyo alipenda aliyosikia. Lakini kuna dini nyingi, na alishangaa kama kweli hii ndiyo ya kweli. Kwa hiyo akamwomba Mungu, “Ikiwa hii ndiyo kweli, mwache mwanamke huyu arudi.” Yule mwanamke Shahidi alirudi, na funzo la Biblia likaanzishwa. Mwanamke huyo alifanya shangwe alipojua kwamba kweli alikuwa ameipata kweli.
SALA KWA AJILI YA WENGINE
Kweli, si wote wenye mioyo minyofu wanaomba kwa wazi kwamba wajue njia iongozayo kwenye kibali cha kimungu. Kwa habari yao sala za kuwaombea za watumishi waliojiweka wakf wa Mungu zinaweza kuwa na “nguvu nyingi.” (Yak. 5:16, NW) Wakifahamu kwamba ni kusudi la Mungu kwamba wanadamu wa namna zote waokolewe, watumishi wake wanaendelea kuwaombea wote ambao huenda ikawa wana nia yenye haki.—1 Tim. 2:1-6.
Kuna mfano wa Shahidi katika Ureno (Portugal) aliyemwona jirani yake akilima kisehemu chake cha ardhi. Aliitumia nafasi hii kwa faida, akimwuliza namna angependa kuona dunia yote ikigeuzwa kuwa bustani nzuri siku moja. Jirani huyo alifikiri ya kwamba jambo hili halingewezekana. Lakini Shahidi alimhakikishia kwamba Mungu amekwisha fanya ahadi kama hiyo, na kwamba kwa sababu hiyo ingetimia.
Bila kuridhika, jirani alijibu kwamba kwa kweli hakujua cho chote juu ya Mungu, licha ya hata kujua cho chote juu ya paradiso iliyoahidiwa kwa dunia hii. “Sababu, hata sijui njia ya kumwomba Mungu,” akaongeza. Kwa njia ya waziwazi, Shahidi alisema: “Manueli, hivyo hujamwomba Mungu wakati wo wote. Basi, njoo hapa na uvue kofia yako. Nitakuonyesha.” Shahidi ndipo akamshukuru Yehova kwa ahadi ya taratibu mpya yenye haki. Aliomba vilevile kwamba Yehova aufungue moyo na akili ya jirani yake Manueli ili ajifunze juu ya ufalme wa Mungu. Matokeo yalikuwa nini?
Yehova Mungu aliufungua moyo wa Manueli. Funzo la nyumbani la Biblia lilianzwa kwake. Kwa muda wa miezi mitatu yeye na mkewe walianza kuwaambia wengine juu ya mambo mema waliyojifunza. Miezi sita tangu funzo lao la kwanza la Biblia walibatizwa.
Kwa wazi Mungu anajibu sala za wenye mioyo ya haki. Anahakikisha kwamba wanapata msaada unaotakiwa ili kuwa katika kukamatana kulikowekwa wakf naye. Wanapofurahia hali njema mbele zake, anaendelea kujibu sala zao. Yesu Kristo aliwaambia wafuasi wake, waliokuwa wakiomba kupatana na mapenzi ya kimungu: “Yo yote mtakayoyaomba katika sala mkiamini, mtapokea.”—Mt. 21:22.