Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w73 4/1 kur. 167-168
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Habari Zinazolingana
  • Kuongozwa na Dhamiri Katika Kufanya Mema kwa Wote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Mungu atahisije nikitumia tumbaku?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Maadili ya Tumbaku?
    Amkeni!—1992
  • Tumbako na Uchunguzi wa Kama Yafaa Kutumiwa
    Amkeni!—1990
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
w73 4/1 kur. 167-168

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

● Je! Biblia inaonyesha kwamba mtu anayetaka kumtumikia Mungu imempasa aache kutumia tumbako?​—U.S. A.

Biblia haitaji tumbako, kwa kuwa kama historia inavyoandika, tumbako haikutumiwa wakati wa kuandika Biblia. Lakini tunaweza kufikia uamuzi juu ya matumizi ya tumbako kwa kuangalia kanuni za Biblia.

Mkristo yumo katika mbio ya uzima. Mtume Paulo alitaja jambo hili kwa Wakristo katika Korintho waliofahamiana na michezo ya huko, iliyofanywa karibu. Wapiga mbio katika michezo hii walikuwa na orodha ngumu ya mazoezi iliyochukua karibu wakati wote waliokuwa nao, chini ya kusimamiwa kwa kuangaliwa sana na mahakimu. Mtu aliyevunja kanuni aliondolewa katika mashindano.

Akitumia mambo haya, Paulo alikazia katika akili za Wakristo kwamba sikuzote walikuwa wakiangaliwa na Hakimu mkuu, Yehova. Akieleza kwamba kufuata kanuni za mashindano ya mbio ya Kikristo kunatia kupigana na tamaa za mwili, alisema hivi: “Kila ashindanaye katika michezo hujizuia katika yote; . . . bali nautesa mwili wangu na kuutumikisha; isiwe, nikiisha kuwahubiri wengine, mwenyewe niwe mtu wa kukataliwa.”​—1 Kor. 9:24-27.

Wakati mwingine mtume aliwaandikia Wakristo katika Rumi hivi: “Itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana.” (Rum. 12:1) “Takatifu” ina maana ya usafi katika njia ya kimwili na ya kiroho vile vile. Inawapasa Wakristo wajitakase wenyewe na “uchafu wote wa mwili na roho, huku tukitimiza utakatifu katika kumcha Mungu.”​—2 Kor. 7:1.

Uchafu wa kimwili si wenye kutamanika na ni wenye hatari, zaidi kwa Mkristo. Kufuata kwa makusudi mazoea yanayotia matumizi ya sumu katika mwili, kuuchafua, kunamzuia mtu katika kumtumikia Mungu. Ikiwa harufu ya tumbako, au alama ya tumbako kinywani na katika meno inaonwa na wengine, inaondoa fikira za watu kutoka kwa habari njema za Ufalme ambazo mtu anatangaza. Tena inaondoa fikira kutoka kwa uzuri na uvutano wa ibada ya Mungu ambaye mtu huyo anawakilisha na kuabudu.

Mtu mwenye kufuata tamaa za mwili wenye dhambi na ambaye kwa mazoea anakuwa mlafi au anakula kitu fulani ambacho ni cha hatari kwa mwili wake anakuwa mtumwa wa tamaa yake. Mtume alisema: “Vitu vyote ni halali kwangu, lakini mimi sitatiwa chini ya uwezo wa kitu cho chote.” Ndipo alipoendelea kusema kwamba mtu mwenye kujiachilia kutawaliwa na cho chote asingeendelea kuishi muda mrefu zaidi kuliko kitu kinachomtawala. “Vyakula ni kwa tumbo, na tumbo ni kwa vyakula,” akatangaza. (1 Kor. 6:12, 13) Kwa hakika sisi hatutaki tutawaliwe na kitu kinachoharibika katika kutumiwa, kwamba ni chakula, tumbako, au kingine cho chote.

Mawazo haya ya Maandiko juu ya matumizi ya tumbako si mapya. Wengine, walipoyajua, walikumbuka kuyatumia katika maisha zao, lakini wakaahirisha kwa siku nyingine. Waliona wangeweza kushirikiana pamoja na mashahidi wa Yehova bila kuacha kabisa kutumia kwao tumbako. Basi, sasa, ingawa walijiona ni wenye hatia juu ya mazoea yao ya tumbako, hawajitahidi kweli kweli wapate kuyavunja.

Walakini, inawapasa watu hao wajiulize wenyewe kwa unyofu wa moyo: Je! kufuata mwendo huo unaoonyesha kutojali kutumia kanuni za Biblia kunaleta kibali cha Yehova? Je! mtu anayeendelea kuzoea kitu anachojua kuwa ni kosa kweli anampenda Yehova ‘kwa moyo wake wote’? Au pahali pake yeye anafurahia kile kisichompendeza Mungu? Ikiwa kweli anataka kuwa kati ya wale ambao Yehova atapendelea kuwapa uzima katika taratibu yake mpya, inampasa ajitahidi kwa moyo alete maisha yake katika kupatana na Neno la Mungu sasa. Kumbuka kwamba wakati wengine wa wanafunzi wa Yesu walipomwuliza: “Je! Bwana, watu wanaookolewa ni wachache?” alishauri wajitahidi sana sana kwa sababu wengi wangetaka kuingia katika Ufalme lakini wasingeweza.​—Luka 13:23, 24; Mt. 22:37.

Paulo aliandika kwa namna iyo hiyo: “Angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima, bali kama watu wenye hekima; mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu. Kwa sababu hiyo msiwe wajinga [si kutumia mawazo ya uongo au ya kujipendekeza kusaidia kitu ambacho huenda tukataka kujihesabia haki], bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya Bwana.” (Efe. 5:8-17) Imempasa mtu ‘akomboe’ wakati na asikawie katika kuacha mazoea mabaya. Siku ni zenye uovu na kukawia kutii katika shauri moja huenda kukaongoza kwenye kutokutii kukubwa zaidi katika njia nyingine.

Wakristo wanataka kuwa na dhamiri nzuri kwa Mungu sasa, maana hii ni ya lazima kwa kumwabudu yeye kwa moyo wote. Ikiwa mtu ambaye sasa anatumia tumbako anafikiria kubatizwa, inampasa afikirie shauri hili kwa uzito sana, kwa sababu ubatizo unaonyesha “si kuondolewa kwa uchafu wa mwili, bali ombi lifanywalo kwa Mungu kwa dhamiri njema.” (1 Pet. 3:21, NW) Imempasa aondoe uchafu wa mwili mapema. Angekuwa mtu asiye na upatano katika kuomba dhamiri njema iliyo nzima ikiwa angejua kwamba alikuwa akishindwa au kukataa kuacha mazoea machafu, yenye kudhuru. Na ikiwa amekwisha kubatizwa imempasa aondoe mazoea hayo sasa ili kusiwe kizuizi kwa dhamiri yake njema, na kumshukuru Mungu kwa fadhili Zake zisizostahili.​—Ebr. 4:16.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki