Kuokolewa kwa Wanadamu Kuingia Katika Taratibu Mpya ya Mungu
”Tazama, mimi ninaumba mbingu mpya na dunia mpya.”—Isa. 65:17, Swahili Congo Bible
1, 2. (a) Ni mashauri gani yanayofanywa kwa sababu ya usemi wa kale, “Jambo jipya hakuna chini ya jua”? (b) Hali hizo zilizoshauriwa zinaamsha maulizo gani?
NI USEMI wa kale, “Jambo jipya hakuna chini ya jua.” (Mhu. 1:9) Lakini namna gani ikiwa kusingekuwako vita, wala hata matayarisho ya vita duniani, wala misiba yo yote ya asili, wala ajali zenye hatari, wala njaa na magonjwa ya kipuku? Namna gani ikiwa kusingekuwako mizigo yenye kulemea sana ya gharama nyingi mno zinazotozwa na serikali, hakuna mapinduzi mabaya ya serikali? Hivyo ingekuwa vyema sana, sivyo? Lakini tusiachie hapo!
2 Namna gani ikiwa watu wasingekuwa wakibaguana kwa sababu ya vyeo, hakuna chuki ya kitaifa, hakuna ubaguzi wa rangi? Namna gani ikiwa hawangekuwako watu kati yetu ambao wangekuwa wakizeeka, pamoja na kupofuka, kuwa viziwi, kuwa na upara, kuwa vibogoyo, kupata udhaifu wa kimwili, bali wangekuwa wakifikia nguvu na uzuri wa ujana na kuuendeleza milele? Namna gani ikiwa hakuna mtu ambaye angekuwa akiwa mgonjwa na kufa, bali, mahali pake, watu wangekuwa wakirudi kutoka makaburini na kurudishwa hali wako hai katikati yetu mpaka makaburi ya mwisho yangekuwa tupu? Namna gani ikiwa kungekuwako elimu ya ulimwengu wote ya kweli iliyo sahihi juu ya dini na kama sisi sote tungekuwa tukipatana na kweli hiyo? Namna gani ikiwa tungekuwa tukiishi kwa amani katika dunia iliyo mfano wa bustani, chini ya serikali moja duniani pote? Hilo lingekuwa jambo jipya kwa wanadamu wote, sivyo?
3. (a) Hali hizo zingetofautisha tu taratibu ya namna gani? (b) Namna gani kutazamia jambo fulani upande wa madaktari na wataalamu wa afya kwa habari ya kifo?
3 Ndiyo, kweli. Na taratibu ya mambo ambayo chini yake hali hizo zingekuwamo duniani pote, pamoja na uhusiano huo mkamilifu kati ya jamaa ya kibinadamu, ingekuwa taratibu mpya, kweli kweli. Hata wazo la taratibu hiyo ya mambo duniani ni jipya kwa mamilioni yasiyo na hesabu ya akili leo. Historia ya kibinadamu inafunua kwamba wanadamu hawajapata kuishi wakati wo wote chini ya taratibu ya namna hiyo mpaka wakati huu wa sasa. Ile ambayo sisi sote tunajua sana ni ile ambayo kwa sasa ni “taratibu ya kale,” hii “taratibu ya sasa.” Taifa la kibinadamu limekuwapo juu ya dunia hii kwa maelfu ya miaka, na hata hivyo uso wa dunia haukujaa sana watu, pamoja na chakula tele kwa wote. Hii imekuwa kwa sababu mauti, kutokana na vyanzo vingi mbali-mbali, imekuwa ikiua polepole maisha za kibinadamu. Imezuia jamaa ya kibinadamu isiongezeke hata kwa haraka zaidi kuliko ambavyo imekuwa ikifanya katika karne hizi mbili za mwisho. Mauti imekuwa sehemu ya sikuzote ya taratibu hii ya kale, na madaktari wa utabibu na wataalamu wetu wa afya chungu zima wa leo hawatupi msingi wa kuwatazamia kuondoa kabisa mauti kwa kadiri taratibu hii ya kale inavyoendelea.
4, 5. (a) Watu wanaonaje juu ya taratibu ya sasa, lakini kunatokea maulizo gani juu ya wanachotaka? (b) Watu wenye vyeo wanamtumaini nani, na hivyo wanafanya nini kwa habari ya wakati ujao?
4 Wanadamu wamechoka na hii “taratibu ya sasa,” au, “mchafuko,” kama wengi wanavyopendelea kuiita. Ni wakati kwa mageuzi. Ndiyo, lakini ni nani anayekusudiwa kuigeuza? Kuna nani awezaye kuigeuza? Kwa muda mrefu wanadamu wamepewa nafasi yao waigeuze iwe bora. Lakini kufanywa kwa hali ya mwanadamu kuwa bora kumekosa kutimizwa mpaka sasa.
5 Watu wenye vyeo katika taratibu ya sasa wangali hawataki kuacha kuwatumaini wanadamu, uwezo wa kibinadamu, zaidi sasa wakati tunayo maendeleo yote ya kisanyansi ya karne hii ya ishirini. Mipango ya wakati wa mbele sana inaendelea kwa shauku sana. Wenye kufanya mipango ya serikali wanatazamia wakati wa mbele wa mwisho wa kame hii. Wamekwisha anza kusema juu ya mwaka wa 2000, na kwa matumaini mazuri wanatazamia hali za dunia zitakazokuwako wakati huo kwa njia za akili ya kibinadamu. Wanatazamia mageuzi makubwa. Wanaona lazima ya mageuzi mengi makubwa.Wanatazamia kujitukuza wenyewe kwa kuleta ustaarabu mkubwa zaidi utakaowapatia wanadamu faida kubwa zaidi kuliko wakati wo wote uliotangulia, utakaofanya maisha kuwa mazuri zaidi. Lakini namna gani sisi sasa?
6. (a) Kunatukia nini kwa mambo yetu magumu ya sasa? (b) Basi sisi tunataka nini, na tunataka iwe wakati gani?
6 Magumu yenye kuenea ulimwengu yanatuandama sisi leo. Mambo hayo yanazidi kuwa mazito na magumu kwa kadiri wakati unavyosonga mbele. Hii ni kweli ijapokuwa ahadi zote na uhakikisho ambao umefanywa na watawala wa kisiasa na viongozi wa ulimwengu ili kuwapa watu “taratibu mpya” yenye tumaini nzuri. Lo! bila shaka, mageuzi fulani ya juujuu tu yanafanyika kwa nje, lakini “taratibu ya kale” ile ile imeendelea pamoja na sisi pamoja na vita vyake, uonevu, matendo yasiyo ya haki, kushindana kwa mataifa na makabila, njaa kali kwa mamilioni, jeuri, kukosa usalama, maumivu, magonjwa, uzee, na kufa. Sisi tunataka kilicho tofauti na hicho. Tunataka “taratibu mpya” kabisa. Katika tamaa yetu ya asili tunataka ianze katika kizazi chetu hiki. Ndipo sisi wenyewe tunaweza kufaidika nayo milele. Ni nani awezaye kuileta?
7, 8. (a) Kwa kupita maelfu ya miaka ya matukio ya kibinadamu, mtunga Zaburi alisema nini juu ya kutumaini kwetu? (b) Kwa uhakika wa jambo hili mtunga Zaburi anasema nini?
7 Maelfu ya miaka ya matukio ya kibinadamu yalikuwa yamekwisha kupita wakati mwanadamu aliyeongozwa na roho ya Mungu alipoandika hivi: “Msiwatumainie wakuu, wala binadamu ambaye hakuna wokovu kwake. Pumzi yake hutoka, huurudia udongo wake, siku hiyo mawazo yake yapotea.” Karibu miaka 3,000 ya wakati tangu maneno hayo yalipoandikwa imehakikisha usawa wa shauri hilo. Vema, basi, ikiwa hatuwezi kuweka tumaini letu katika binadamu, hata katika wakuu ambao ni bora kuliko watu wa kawaida, kuna nani mwingine ambaye katika yeye tutaweka tumaini letu?
8 Kwa hakika huyo mshauri aliyetangulia kutajwa hapaswi kusema tu pasipo kuwa na hakika na kutuacha sisi katika hali ya kutokujua jambo la kufanya. Kwa akili amepaswa aondoe shauri hilo lisilo na uhakika kwa kutupa shauri fulani lenye uhakika kwa kutuambia nani kuondoa binadamu ndiye katika yeye tunaweza kuweka tumaini bila kukata tamaa. Yeye anafanya hivi, akisema: “Heri ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake, na tumaini lake ni kwa [Yehova], Mungu wake. Aliyezifanya mbingu na nchi, bahari na vitu vyote vilivyomo. Huishika kweli milele, huwafanyia hukumu walioonewa, huwapa wenye njaa chakula.”—Zab. 146:3-7.
9. Yehova alisema nini kwa Yeremia juu ya kumtumaini mwanadamu, na hii imekuwa kweli kwa kadiri gani kulingana na historia ya kibinadamu?
9 Je! ye yote anaelekea kudhihaki shauri hilo lililoongozwa na roho ya Mungu? Hayuko peke yake katika maoni haya. Wingi wa watu wamekataa kuangalia shauri hili, ijapokuwa walilijua. Je! wamefaidika au wamebarikiwa katika kufanya hivyo? Historia ya kibinadamu inaonyesha. Inakubaliana na ukweli wa maneno ambayo Muumba wa mwanadamu mwenyewe alimwambia nabii wake Yeremia: “Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake, na moyoni mwake amemwacha [Yehova]. Maana atakuwa kama fukara nyikani, hataona yatakapotokea mema; bali atakaa jangwani palipo ukame, katika nchi ya chumvi isiyokaliwa na watu.” (Yer. 17:5, 6) Laana ni kutokuwa na baraka, na ushuhuda wote unaonyesha kwamba wanadamu hawakubarikiwa kwa sababu ya kuwatumainia wanadamu kuliko kumtumaini Mungu.
10. (a) Wanadamu wenye kujitumaini wenyewe wanatendaje juu ya kuwa na wajibu kwa Mungu? (b) Kwa sababu hiyo Mungu angeweza kuwatendea nini, na kwa sababu gani?
10 Wanadamu wenye kujitumaini wenyewe, wenye kujisifu kwa sababu ya mambo yao ya kisasa ambayo wanatimiza, wanajiongoza wenyewe kana kwamba hawakuwa na deni yo yote kwa Mungu. Hawaoni kuwa wana daraka kwake na wanazitupilia mbali sheria zake zilizoandikwa. Ikiwa hawakani kuwako kwake au hata kusema kwamba “Mungu amefariki,” wanatenda kwa habari ya mambo ya kibinadamu kana kwamba hakuwako. Ijapokuwa wana deni ya kila kitu kwa Yeye, Mungu Muumba hadaiwi kitu na mwanadamu. Kila kitu ambacho mwanadamu anacho na kujifurahisha, anakula deni kwa Mungu. Na kwa vile sasa mwanadamu bila kushukuru anamwacha Mungu na hajioni ana wajibu kwa Yeye, ili amtii Yeye kama Chanzo cha uzima na cha sheria za haki kwa maisha, Mungu hana deni kwa mwanadamu mwasi. Yeye angeweza kuwaacha wanadamu wale tunda lenye uchungu la mwendo wao wenyewe wa kujitakia. Ndiyo, yeye angeweza kuwaacha wanadamu wafe mpaka wamalizike au hata kujiua wenyewe mbele ya wakati huo kwa matumizi ya njia zao zote za kisasa kwa kujiangamiza wenyewe.
11, 12. (a) Mtu mwenye hekima alisema nini juu ya mwanzo wa wanadamu, na hiyo ilikuwa kweli namna gani? (b) Ni katika njia gani “taratibu mpya” isingalihitajiwa, lakini sisi leo tumejifunza nini juu ya mipango ya zamani ya kibinadamu?
11 Mfalme mwenye hekima kuliko wote wa nyakati za kale, akiikumbuka historia ya wanadamu tangu mwanzo wao mpaka karne ya kumi na moja ya mbele ya Wakati wetu wa Kawaida, alisema hivi: “Hili peke yake ndilo mimi nimeona, kwamba Mungu wa kweli aliwafanya wanadamu wanyofu, lakini wao wenyewe wametafuta mipango mingi.” (Mhu. 7:29, NW) Mungu wa kweli aliwaumba wanadamu wa kwanza wawili waliooana wanyofu, wakamilifu katika mwili, akili, moyo, adili, na akawaweka katika makao ya bustani yenye kupendeza wakiwa na chakula tele ili waendelee kuishi milele katika afya kamilifu.
12 Ikiwa wangaliutumia vizuri uhuru wao wa kuchagua na wakaendelea kuwa wanyofu na wakazaa watoto wao katika unyofu na polepole wakapanua makao yao ya Paradiso ili kuenea dunia yetu hii yote, je! kungalikuwa na uhitaji leo wa “taratibu mpya”? Hapana! Hali ya Paradiso kamilifu ya mambo duniani ingaliendelea mpaka sasa na kusingalitokea na uhitaji wa kurudisha wanadamu kwa hali ilivyokuwa hapo mwanzoni wakati Mungu alipoiumba. Lakini chini ya jaribu la utii mkamilifu kwa Muumba wao na Mpaji wao wa sheria, wanadamu wa kwanza wawili walijitafutia mipango yao wenyewe. (Mwa. 1:26 mpaka 5:5) Leo, ikiisha kupita kama miaka 6,000, sisi sote tunajua namna mipango yao ilivyotokea.
UHAKIKA WA TARATIBU MPYA
13. Nani anayeweza kuleta taratibu ambayo ni mpya kabisa, na kuna wajibu wo wote kufanya hivyo?
13 Kwa kadiri ulivyo uwezo wetu wa kuondoa matokeo ya mpango huo mbaya, wanadamu wamejiumiza wenyewe hata hawawezi kujiponya wenyewe. Sasa ni kuchelewa mno kuliko watu wanavyofikiri. Basi ikiwa watu wanaendelea kuwatumaini wanadamu wasiokamilika na wenye kufa kuleta taratibu mpya isiyo na mambo yote yenye kuumiza ya taratibu hii ya sasa, hawatapata matokeo yo yote ila mgogoro—karibuni sasa! Muumba wetu, Mungu Mwenye Nguvu Zote, peke yake ndiye anayeweza kuileta taratibu mpya. Je! atafanya hivyo? Yeye hana wajibu wa kufanya hivyo, hata ijapokuwa mwanadamu hakuomba apate kutokea na hakujiweka mwenyewe hapa duniani. Lakini sababu gani Mungu hayuko chini ya wajibu? Ni kwa sababu mwanadamu amemwacha Mungu. Mwanadamu amechagua aende njia yake katika kumwasi Muumba na Mpaji wake wa sheria. Tena, tukimhukumu mwanadamu kwa kufikiri kwake, mpango wake na jitihada zake, yeye hataki taratibu mpya ya Mungu. Namna gani hivyo? Basi, mwanadamu hataki kutimiza matakwa ya taratibu hiyo mpya.
14. Basi, ni ulizo gani, na tunaweza kupata wapi habari yenye kutegemeka?
14 Basi sasa ulizo kubwa ni, Je! Mungu Mwenye Nguvu Zote anaelekea kuweka taratibu mpya inayohitajiwa sana? Je! Yeye ameamua kufanya hivyo? Majibu yenye kutegemeka, yenye uhakika kwa maulizo hayo—tunaweza kuyapata wapi? Si kwingine ila katika Neno la Mungu lililoandikwa, Biblia Takatifu!
15, 16. (a) Kupitia kwa nabii wake Isaya Mungu alisema nini juu ya kusudi lake kufanya hivyo? (b) Mtume Yohana anaonyeshaje kama Mungu amegeuza akili yake juu ya hili, na kwa sababu gani Yohana aliambiwa aandike juu ya hili?
15 Sikiliza, wakati Yeye anaposema kwa nabii wake Isaya katika karne ya nane mbele ya Wakati wetu wa Kawaida: “Tazama, mimi ninaumba mbingu mpya na dunia mpya, na maneno ya kwanza hayatakumbukwa, wala hayataingia moyoni. Lakini mufurahi, na mushangilie daima, kwa ajili ya hivi ninavyoumba.” (Isa. 65:17, 18, Swahili Congo Bible) ‘Alaa!’ labda msikilizaji fulani atasema, ‘hayo yalisemwa na kuandikwa zamani karne kama 27 na sasa hayatumiki na hayana maana leo.’ Lakini sikiliza, sasa, ufunuo ambao Mungu alimpa mtume wa Kikristo Yohana wakati uliofuata zaidi ya miaka 800. Katika kuandika, Yohana anasema hivi: “Nikaona kiti cha ufalme, kikubwa, cheupe, naye anayeketi yulu yake, dunia na mbingu zikakimbia uso wake; na pahali pao hapakuonekana. . . . Nikaona mbingu mpya na dunia mpya; kwa maana mbingu za kwanza na dunia ya kwanza zimekwisha kupita, wala hapana bahari tena.” (Ufu. 20:11 mpaka 21:1, Swahili Congo Bible) Hivyo ingawa zilikuwa zimepita zaidi ya karne nane Mungu yule yule hakuwa amegeuza akili yake. Tena, Yohana aliandika zaidi:
16 “Na yeye aketiye juu ya kile kiti cha enzi akasema, Tazama, nayafanya yote kuwa mapya. Akaniambia, Andika ya kwamba maneno hayo ni amini na kweli.”—Ufu. 21:5.
17. Hivyo sasa, leo, ikiisha kupita miaka 1900, ni nini habari njema katika neno hili?
17 Kwa hiyo, Mungu huyu anayeketi juu ya kiti chake cha enzi cha kimbinguni asingeweza kuwa wa kweli kwake mwenyewe na wakati ule ule ageuze akili yake kwa habari ya kusudi lake lililotangazwa kuumba taratibu mpya yenye mbingu mpya na dunia mpya ambamo haitakuwamo bahari ya wanadamu waliotengwa na Mungu kupitia kwa dhambi iliyorithiwa kutoka kwa wazazi wetu wa kwanza wa kibinadamu. Hivyo, ijapokuwa Mungu hana deni yo yote na wanadamu, yeye anaelekea kuleta taratibu mpya inayotamanika, na hakugeuza akili yake, hata ingawa miaka 1900 ya wakati imepita. Je! hizo si habari njema?
KINACHOZUIA JITIHADA ZA WANADAMU
18. Mbele ya kuweza kuwako “dunia mpya,” ni lazima kwanza kuweko nini?
18 Na tufahamu kwamba Mungu anaahidi kuumba, si “dunia mpya” tu, bali vile vile “mbingu mpya.” Namna hii inavyoonyesha kwamba Mungu anajua jambo ambalo ni la lazima zaidi ili wanadamu wenye kufa wawe na taratibu mpya. Hakuwezi kukawako “dunia mpya” bila kuwako kwanza “mbingu mpya”! Jua, mwezi, nyota, sayari na makundi ya nyota mpya juu katika upeo wa macho ya mwanadamu? Hapana! Vitu hivi vinavyoonekana na visivyo na akili katika anga havina na haviwezi kuwa na matokeo yo yote juu ya taratibu ya mwanadamu ya mambo kama vile wanajimu (wataalamu wa nyota) kutoka siku za Babeli wa kale wamefundisha. Lakini kwa usemi huu “mbingu mpya” Yehova Mungu anamaanisha watu wenye akili wa kiroho wasioonekana katika utawala wa kimbinguni usio wa kibinadamu juu ya wanadamu.
19. Maana hii ya usemi “mbingu mpya” ilionyeshwa namna gani na nabii Danieli, na vile vile na Yesu Kristo?
19 Hiyo ilikuwa ndiyo maana yake wakati nabii Danieli alipotumia neno “mbingu” alipokuwa akitafsiri ndoto ya mfalme wa Babeli wa kale juu ya mti mkubwa na kusema: “Nyakati saba zitapita juu yako; hata utakapojua ya kuwa Aliye juu ndiye anayemiliki katika ufalme wa wanadamu, naye humpa yeye amtakaye, awaye yote. Na kwa kuwa waliamuru kukiacha kisiki cha shina lake; ufalme wako utakuwa imara kwako, baada ya wewe kujua ya kuwa mbingu ndizo zinazotawala.” (Dan. 4:25, 26) Wazo hili la utawala na uongozi usioonekana, wenye akili wa kimbinguni juu ya wanadamu lilikuwamo vile vile katika maneno ya Yesu Kristo, wakati alipotangaza hivi: “Ufalme wa [mbingu] umekaribia.”—Mt. 4:17.
20, 21. (a) Usemi “mbingu mpya” unaonyesha nini, na hii inaelezaje kutoweza kwa mwanadamu kugeuza mambo yawe bora? (b) Watu wenye hekima ya kilimwengu wanajipumbaza wenyewe namna gani juu ya jambo hili?
20 Ahadi ya Mungu ya “mbingu mpya” inaonyesha kwamba kuna “mbingu” za kale zinazotawala wanadamu na ambazo pasipo kuonekana zinaongoza taratibu ya sasa ya mambo. Mbingu hizi za kale za mfano ndio mgogoro unaozuia jitihada zote za unyofu za wanaume na wanawake kuigeuza taratibu ya sasa iwe bora na kuwa na maendeleo yenye kudumu katika kutumaini kuokoa wanadamu wasijiangamize wenyewe. Kwa wanadamu “mbingu” hizi za kale ni adui asiyeonekana mwenye uwezo wa kuwadanganya mara nyingi sana wanaume na wanawake wenye kujitegemea, kama historia ya kibinadamu imeonyesha tangu mwanzo mpaka sasa.
21 Watu wenye hekima ya kilimwengu wa hiki Kizazi cha Akili cha sayansi wanakataa kusadiki na wanadhihaki kuwako kwa adui huyo wa kiroho asiyeonekana, mwenye kupita uwezo wa kibinadamu, mwenye akili. Lakini adui uyo huyo anajua kwamba hakuna wapumbavu wakubwa zaidi kuliko hao wanaojipumbaza wenyewe. Lakini sisi si wapumbavu wakati tunapouliza, Ni nani adui huyo kama anavyoonyeshwa na “mbingu” za kale?
22, 23. Yeye aliyeshuka kutoka mbinguni na akarudia huko aliwaambiaje wanadamu kuwa adui huyu ni nani?
22 Mtu aliyeshuka kutoka mbinguni na akaishi kama mwanadamu duniani kwa zaidi ya miaka 33 mbele ya kurudi kwenye mbingu zisizoonekana anatuambia adui huyo ni nani. Wakati mmoja alipokuwa duniani wanaume 70 ambao alituma kama wahubiri wa injili ili wautangaze ufalme wa Mungu walirudi na kutoa ripoti hivi: “Bwana, hata [mashetani] wanatutii kwa jina lako.” Katika kujibu, Yesu Kristo aliwaambia wahubiri wa injili hao wenye kushangilia jambo gani? Hili: “Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni kama umeme.” (Luka 10:1-18) Katika mfano ambao alitoa mwishoni mwa unabii wake juu ya mwisho wa taratibu hii ya mambo yeye alitabiri wakati ambapo angesema maneno haya kwa watu walio mfano wa mbuzi: “Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake.” (Mt. 24:3; 25:31-33, 41) Siku tatu zilizofuata, alipokuwa akiwaambia mitume wake waaminifu juu ya kusalitiwa kwake na kifo chake kibaya kilichokuwa kikija juu ya mti wa kufishia, Yesu Kristo alisema:
23 “Sasa kuna hukumu ya ulimwengu huu; sasa mtawala wa ulimwengu huu atatupwa nje.” “Mtawala wa ulimwengu anakuja. Naye hana lo lote la kushughulika na mimi.” (Yohana 12:31; 14:30, NW) “Tazama, Shetani amewataka ninyi apate kuwapepeta kama vile ngano.”—Luka 22:31.
24. Katika njia hiyo Yesu alionyesha nini juu ya “mbingu” ambazo sasa zinatawala wanadamu, na, kulingana na Paulo, ulimwengu wa wanadamu unamwabudu nani?
24 Hapo tunapata maneno ya Yesu Kristo mwenyewe akisema: Shetani Ibilisi na malaika zake za kishetani ndio mbingu za kale za mfano, “mbingu” za sasa zenye kupita uwezo wa kibinadamu, zinazotawala na kuongoza wanadamu wakati wa taratibu hii ya sasa ya kale. Pahali pa kumwabudu Mungu wa kweli anayeahidi “mbingu mpya na dunia mpya,” wingi wa wanadamu wanamwabudu Ibilisi na mashetani wake. Ibilisi ni mwerevu na mjanja katika kuficha matendo yake na udanganyifu wake juu ya watu, kwa maana mtume wa Kristo Paulo aliandika hivi: “Mungu wa taratibu hii ya mambo amepofusha akili za wasioamini, kwamba mwangaza wa habari njema zenye utukufu juu ya Kristo, ambaye ni mfano wa Mungu, usipate kung’aa kwa kupenya.” (2 Kor. 4:4, NW) Kwa maelezo hayo mtume Paulo alimaanisha mungu wa uongo, Shetani.
25. Nani aliyewashawishi Adamu na Hawa wajitafutie mipango yao tofauti na mapenzi ya Mungu?
25 Tena, Yesu Kristo alionyesha Shetani Ibilisi kama akiwa mtu asiyeonekana aliyewashawishi Adamu na Hawa watu wanyofu wajifanyie mipango tofauti na mapenzi ya Mungu. Hivyo ndivyo Shetani alivyoleta hali hii ya kufa, isiyokamilika juu ya sisi sote.
26. Shetani aligeukaje akawa kama Yesu alivyomwita, “mwuaji”?
26 Wakati mmoja Yesu alisema kwa watu fulani katika watu waliokuwa wakimsikiliza waliokuwa wakitaka kumwua na kuwaambia hivi: “Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa huo.” (Yohana 8:44) Katika makao ya kwanza ya mwanadamu, Bustani ya Edeni, Shetani Ibilisi alimwita Yehova Mungu mwongo; na mwanamke wa kwanza, Hawa, akamwamini Ibilisi, halafu mume wake, Adamu, akamwunga mkono na kujiunga pamoja naye katika kumwasi Mungu. Kwa hiyo Yehova alitamka hukumu ya kifo juu ya wazazi wetu wa kwanza; na kwa sababu Shetani Ibilisi ndiye aliyetokeza haya, aligeuka akawa ambavyo Yesu alimwita, “mwuaji.” Alituua sisi vile vile, kwa maana sisi tumerithi hali yetu ya kufa kutoka kwa Adamu na Hawa wenye dhambi.—Mwa. 2:7–5:5.
27, 28. (a) Ni udhaifu gani ambao wanadamu wenye uwezo wa ulimwengu hawawezi kutuondolea, au ni nini ambacho majeshi na watu wenye mapinduzi hawawezi kutuondolea? (b) Paulo aliwapa Waefeso wazo namna gani juu ya kitu tunachoshindana nacho?
27 Ingawa yote ambayo watawala wa serikali na watunga sheria na mahakimu na madaktari na wanasayansi wanaweza kufanya, hawawezi kutuondolea laana ya mauti ambayo bado iko juu yetu kwa sababu ya hali yenye dhambi na kutokukamilika tulikorithi. Hawawezi kuturudisha katika Bustani ya Edeni ambamo wazazi wetu wa kwanza walifukuzwa watoke humo kwa sababu ya kumwasi Mungu Muumba. Ijapokuwa yote ambayo majeshi ya kivita ya ulimwengu na watu wenye mapinduzi huenda wakajaribu kufanya, hawawezi kutuondolea “mbingu” za kale za kishetani ambazo zimejiimarisha kwa nguvu juu ya wanadamu. Katika hili majeshi ya kilimwengu na watu wenye mapinduzi wanashindana, si na viumbe vingine vya kibinadamu, bali na majeshi yenye kupita uwezo wa kibinadamu, yasiyoonekana. Mtume Paulo alitupa wazo juu ya kitu ambacho wanadamu wote wanashindana nacho, alipoandikia kundi la Kikristo katika Efeso katika Asia:
28 “Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani. Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.”—Efe. 6:11, 12.
29. Ijapokuwa kufukuza mashetani, Yesu na mitume wake hawakujaribu kufanya nini, kwa matokeo gani leo?
29 Mtume Paulo, na vile vile Yesu Kristo mwenyewe na mitume wake wengine, walifukuza mashetani kutoka katika watu waliopagawa nao, kwa njia hiyo wakiwaokoa wanadamu wasio na uwezo wenye kupatwa nao. Walakini, Yesu Kristo, alipokuwa duniani, na mitume wake hawakujaribu hata kidogo kupindua “mbingu” hizi za kale zisizoonekana, zenye serikali, mamlaka, watawala wa ulimwengu wa kishetani wa giza hili na pepo wabaya katika ulimwengu wa roho. Karne kumi na tisa zilizopita haukuwa wakati wa kuwaokoa wanadamu katika njia hiyo. Kwa hiyo “mbingu” hizo za kishetani zenye uovu zimeendelea kuwatawala wanadamu na mambo ya kibinadamu mpaka sasa. Sasa jamaa ya kibinadamu inapata matokeo mabaya sana ya utawala huu usioonekana, na haina msaada kabisa juu yake.
30. Tuna wajibu wa kumtumaini nani kwa kumtoa Mkombozi, na ili tuepuke kuwa ‘wenye kulaaniwa’ tusimtumainie nani?
30 Wanadamu wanahitaji sana Mkombozi wa kuwakomboa na mbingu hizi za kishetani zenye kuharibu. Yehova Mungu amemsimamisha Mkombozi! Wakati uliowekwa wa Yehova kwa ukombozi unaotamaniwa uko karibu! Sisi hatuwezi kuwatumaini “wakuu” wala binadamu kuwa Mkombozi. Kama tungefanya hivyo tungekuwa ‘wenye kulaaniwa’! Mkazo wa hali unatulazimisha sisi tumtumaini Yehova kwa Mkombozi. Ni nani?
31. Mteule wa Yehova ataweza kufanya nini, na kwa sababu gani hilo ndilo takwa la msingi kwa taratibu mpya?
31 Ni yeye aliyechaguliwa na Yehova Mungu, yeye anayeweza kuziondoa “mbingu” hizi za kishetani za kale. Hakuwezi kukawako taratibu mpya kwa wanadamu bila kuziondoa “mbingu” hizo zenye uovu ambazo zimetawala taratibu hii ya kale. Hakuwezi kukawako taratibu mpya kwa wanadamu bila “mbingu mpya.” Hili ndilo takwa la msingi. Ndilo takwa la kwanza. Yehova Mungu ameahidi kuziumba hizo “mbingu mpya.”
32. Wale waliomo katika ‘mbingu za sasa’ watasawazishwaje na wale waliomo katika “mbingu mpya,” na ni nani ambaye ni wa lazima, anayehitajiwa sana katika “mbingu mpya”?
32 Kama vile ‘mbingu za sasa’ zenye uovu zilivyo na viumbe vya kiroho vyenye kupita uwezo wa kibinadamu, visivyoonekana, vivyo hivyo lazima mbingu mpya ziwe zenye viumbe vya kiroho vyenye kupita uwezo wa kibinadamu, visivyoonekana. Mtume Petro aliwachangamsha Wakristo wenzake katika kumngojea kwao Mungu na kumtumaini Mungu kwa kuandika hivi: “Lakini ziko mbingu mpya na dunia mpya ambazo sisi tunangojea kulingana na ahadi yake, na katika hizi haki itakaa.” (2 Pet. 3:13, NW) Mungu amekwisha kumsimamisha mkuu, yeye ambaye ni wa lazima na anayehitajiwa sana, wa hizo “mbingu mpya,” na huyo ni Mwana wake mwaminifu, Yesu Kristo Bwana. Mshangilie Mkombozi huyu!
[Picha katika ukurasa wa 172]
Kuokolewa kuingia katika taratibu mpya ya Mungu kutakuwa na maana ya kuishi katika afya na furaha kamilifu katika dunia yenye kupendeza iliyo mfano wa bustani, chini ya serikali moja duniani pote