Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w73 8/1 kur. 339-341
  • Je! Kulikuwako Ufufuo?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Kulikuwako Ufufuo?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • SI UFUFUO WA KIMWILI
  • ‘Miili Mingi ya Watakatifu Iliinuliwa’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Tumaini la Ufufuo Lina Nguvu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • “Kifo Kitafanywa Kuwa Si Kitu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Tumaini la Ufufuo Ni Hakika!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
w73 8/1 kur. 339-341

Je! Kulikuwako Ufufuo?

JE! KULIKUWAKO ufufuo kutoka kwa wafu wakati Yesu alipokufa? Waelezaji wengi wa Biblia wanadhani hivyo. Wanaweka imani yao juu ya Mathayo 27:52, 53. Katika Revised Standard Version (tafsiri ya Kirumi Katoliki Confraternity Version karibu inafanana), mistari hii inasomwa hivi: “Makaburi pia yalifunguka, na miili mingi ya watakatifu waliokuwa wamelala usingizi iliinuliwa, na wakitoka makaburini baada ya kufufuka kwake waliingia katika mji mtakatifu na wakaonekana kwa wengi.”

Kulingana na Commentary on Holy Scripture ya Kirumi Katoliki, lile tetemeko la nchi, linalotajwa katika mstari unaotangulia, lilifungua wazi yale makaburi ya miamba ili kutayarisha mlango wa kutokea miili, ambayo haikufufuka mpaka baada ya ufufuo wa Kristo. Lakini na ifahamike kwamba hivi sivyo andiko linavyosema kwa kweli, ama katika tafsiri za Kikatoliki ama za Kiprotestanti.

Kwa habari ya mistari hii mojawapo ya maelezo yenye kujulikana sana ya Biblia ya Kiprotestanti, yale ya Adam Clarke, yanasema hivi: “Ni vigumu kutoa sababu ya habari inayotajwa katika mistari ya 52 na 53. Wengine wamefikiria kwamba mistari hii miwili imeingizwa katika andiko la Mathayo kutoka kwa injili ya Wanazorayo, wengine wanafikiri maana yenyewe ndiyo hii:​—miili mingi iliyokuwa imezikwa ilitolewa nje na ikafunuliwa wazi, na ikaendelea kuwa juu ya ardhi mpaka baada ya kufufuka kwa Kristo, na ikaonwa na watu wengi mjini. Sababu ya makaburi kufunguliwa Ijumaa, na miili isifufuliwe mpaka Jumapili, ni vigumu kufahamu. Mahali hapaeleweki kabisa.”

Mwelezaji mwingine wa Biblia, Dr. Jenks, anasema kwa habari ya mistari hii: “Jambo hili halisimuliwi sana kwa kadiri ambavyo tungeweza kutaka kujua. . . . Huenda tukatokeza maulizo juu yake ambayo hatuwezi tukayajibu.” Waelezaji wengine wa Biblia wanasema kama hivyo.

Je! kweli tukio linalotajwa katika mistari hii miwili lingaliweza kuwa ndio mwanzo wa ufufuo wa wafu ambao juu yake Yesu alisema kama ilivyoandikwa katika Yohana 5:28, 29? Sivyo, kwa maana Yesu alisema kwamba wale wote waliomo katika makaburi ya ukumbusho wangetoka ama kwa ufufuo wa uzima ama kwa ufufuo wa hukumu. Kwa kuwa habari inasema kwamba hawa walikuwa “watakatifu,” wangaliinuliwa kwenye ufufuo wa uzima. Je! ndivyo? Hapana, au wangekuwa bado wakiishi leo, hata kama ambavyo Yesu ameendelea kuishi tangu kufufuliwa kwake kwenye uzima.​—Ufu. 1:18.

Ndiyo sababu tunasoma kwamba “Kristo amefufuka katika wafu, limbuko lao waliolala [katika mauti].” “Ni mzaliwa wa kwanza katika wafu, ili kwamba awe mtangulizi katika yote.” Kwa hiyo, watakatifu hawa wasingaliweza kufufuka wakiwa na tumaini la uzima usio na mwisho wamtangulie Yesu.​—1 Kor. 15:20; Kol. 1:18.

Wasingaliweza hata kufufuliwa kwenye uzima mara baada ya kufufuka kwa Yesu, kama inavyoonyeshwa na wengine, kwa sababu Paulo anaonyesha kwamba watakatifu wa Kikristo watafufuliwa na kupokea thawabu yao “siku ile,” wakati “Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu.” Paulo hakuandika barua hii mpaka miaka mingi Yesu alipokuwa amekwisha kufufuka, na maneno haya yalipaswa yatimizwe katika wakati ujao ulio mbali.​—2 Tim. 4:8; 1 The. 4:16.

Basi je! ingeweza kuwa kwamba hawa walikuwa watakatifu waliotangulia Wakristo, waliokusudiwa uzima, si mbinguni, bali duniani? Ikiwa ndivyo, bado wasingaliweza kupokea ufufuo wao wakati Yesu alipofufuka, kwa sababu Paulo aliandika juu yao hivi: “Na watu hao wote wakiisha kushuhudiwa kwa sababu ya imani yao, hawakuipokea ahadi; kwa kuwa Mungu alikuwa ametangulia kutuwekea sisi kitu kilicho bora, ili wao wasikamilishwe pasipo sisi.” Kama hawa wangalifufuliwa kwenye uzima wakati huo, wangalikamilishwa pasipo “sisi,” watakatifu wa Kikristo.​—Ebr. 11:39, 40.

SI UFUFUO WA KIMWILI

Zaidi ya hayo, hakuna mahali katika Maandiko tunaposoma ya kwamba miili ya wafu itafufuliwa; ijapokuwa iitwayo Imani ya Mitume inafundisha ufufuo wa mwili wa kibinadamu. “Wafu,” ndiyo, lakini si “miili iliyokufa.” Watu waliokufa watafufuliwa katika wakati wake Mungu, nao watapewa mwili unaofaa; watakuwa na utu ule ule. Fahamu namna mtume Paulo anavyotoa sababu za kuthibitisha hili shauri juu ya ufufuo wa watakatifu wa Kikristo: “Wafufuliwaje wafu? Nao huja kwa mwili gani? . . . Uipandayo haihuiki, isipokufa; nayo uipandayo, huupandi mwili ule utakaokuwa, ila chembe tupu, . . . lakini Mungu huipa mwili kama apendavyo . . . Kadhalika na [ufufuo wa] wafu. Hupandwa katika uharibifu; hufufuliwa katika kutokuharibika; . . . hupandwa mwili wa asili; hufufuliwa mwili wa roho. . . . nyama na damu haziwezi kuurithi ufalme wa Mungu; wala uharibifu kurithi kutokuharibika.”​—1 Kor. 15:35-38, 42-44, 50.

Kwa kuwa Biblia haifundishi kufufuka kwa mwili wa kibinadamu ama katika ufufuo wa kwanza ama katika ule utakaofuata, uhakika wa kwamba miili ilifufuliwa ungethibitisha kwamba usingaliweza kuwa mwanzo wa mmojawapo wa ufufuo huu. Bila kuzidi hapo ungekuwa ufufuo wa muda tu wa Wayahudi fulani waaminifu ambao inaelekea sana walikuwa wamekufa majuzi hivi. Kwa hiyo, ufufuo wao usingalikuwa na tofauti yo yote na ule ufufuo aliopata Lazaro rafiki ya Yesu na wengine kama yeye.

Lakini hata dhana hii yapaswa iondolewe kulingana na maulizo haya: Ikiwa makaburi yalifunguka wakati Yesu alipokufa, sababu gani miili ya watakatifu ingojee mpaka baada ya kufufuka kwa Yesu ndipo itoke makaburini na kuonekana na wengi? Kulikuwako na tetemeko la nchi wakati Yesu alipofufuka; kwa sababu gani haikuweza kungojea tetemeko hilo? Miili hii ilionekana kwa akina nani? Je! ufufuo wao ulikuwa katika kushindana na ufufuo wa Yesu, aliyeonekana kwa wanafunzi wake siku ya tatu? Lilikuwa kusudi gani la kuonekana kwao? Walivuta fikira kwa au walisema juu ya nini? Je! ufufuo wao uliongeza cho chote kwa ufufuo wa Yesu au ukawa uthibitisho wa ufufuo wake? Mbona tukio hilo lisilo la kawaida halitajwi mahali penginepo katika Maandiko ya Kikristo ya Kigiriki? Zaidi ya hayo, sababu gani mtume Paulo katika kutoa sababu zake za kuthibitisha hakuutaja ufufuo wao, katika Wakorintho wa Kwanza 15, kwamba kuna ufufuo wa wafu? Ikiwa wengi walikuwa wamefufuka na wakaonwa na wengi, jambo hilo lingalijulikana na watu wote na Paulo angalilitaja.

Ufumbuzi unaofaa wa fumbo hili unatolewa na tafsiri ya mistari hiyo inayozungumzwa katika New World Translation of the Christian Greek Scriptures. Ijapokuwa ni tafsiri halisi, inalieleza wazo waziwazi kuliko kutafsiri namna maneno yalivyo tu. Inasomwa hivi: “Na makaburi ya ukumbusho yalifunguka na miili mingi ya watakatifu waliokuwa wamelala usingizi ilitupwa juu, (na watu, wanaotoka miongoni mwa makaburi ya ukumbusho baada ya kuinuliwa kwake, waliingia katika mji mtakatifu,) nao wakaonekana kwa watu wengi.” Kutokana na tafsiri hii inakuwa wazi kwamba huu haukuwa ufufuo wa “watakatifu waliolala usingizi” bali ni kutupwa nje tu kwa miili kutoka makaburini mwao kwa tetemeko la nchi lililofuatana na mauti ya Yesu.

Wala si New World Translation peke yake inayotafsiri mistari hii katika njia hiyo. Tafsiri ya kisasa ya Kijeremani inasomwa sawasawa kabisa kama hivyo: “Makaburi yalifunuliwa wazi, na miili mingi ya wale waliozikwa ilirushwa juu. Katika hali hii ilitupwa kutoka makaburini na ikaonwa na wengi waliopita karibu na mahali walipokuwa wakirudi mjini.”​—Mt. 27:52, 53.

Tukio linalofanana sana na hili lilitukia katika Ecuador katika mwaka wa 1949. Kwa kawaida huko wafu wanazikwa katika kuba kubwa, rafu kwa rafu na kuba kwa kuba. Tetemeko la nchi lilipasua wazi kuba hizi, likiitoa nje miili mingi ya wafu, ambayo ilipaswa izikwe mara hiyo ili kuzuia kusitokee ambukizo.

Ni msingi gani wa tafsiri hizi? Kwanza, na ifahamike ya kwamba neno linalotumiwa pahali pa kijina “nao” (Mt. 27:53, UV; RS) lisingeweza kumaanisha “miili,” kwa sababu maneno yote yatumiwayo pahali pa vijina katika Kigiriki yana namna zake na neno “nao” li katika namna ya kiume, lakini “miili” li katika namna isiyo ya kiume wala ya kike. Wala neno “nao” lisingeweza kumaanisha “watakatifu,” kwa maana andiko halisemi kwamba watakatifu waliinuliwa ila miili yao tu ndiyo iliyoinuliwa au ilitupwa juu. Tena, hata hati ambazo ni za kale kuliko zote hazipatani juu ya kusomeka kwa andiko hili. Hati inayoitwa Sinaitic inaacha maneno “makaburi yakafunuka” na “wakauingia.”

Kwa sababu ya maulizo yote yanayotokezwa na maandiko haya, namna yanavyosomeka kwa kupingana na tofauti zilizomo katika hati ambazo ni za kale kuliko zote, huenda njia nyingine isiondolewe kabisa. Na ni njia gani hiyo? Kwamba mistari hii haikuandikwa na Mathayo mwenyewe bali iliongezwa na mtu fulani wa kwanza kunakili. Maoni haya yanaonekana kuungwa mkono zaidi katika uhakika wa kwamba neno lenyewe la Kigiriki kwa “kufufuka” (UV; RS) linalotumiwa hapa, égersis, halionekani mahali penginepo katika Maandiko ya Kikristo ya Kigiriki. Tena, katika Injili zote hapa ndipo usemi “watakatifu” unapotumiwa peke yake, ulianza kuonekana kwanza kufuata Pentekoste. Uhakika wa kwamba mistari hii inapatikana katika Injili ya uongo ya Wanazorayo lakini si katika yo yote ya Injili nyingine za kweli unafanya tena mistari hii kuwa yenye kutiliwa mashaka. Kwa bahati, Injili hii ya Wanazorayo ilionwa na wengine kuwa ndiyo Injili ya awali ya Mathayo katika Kiebrania, ambayo nyuma akaitafsiri katika Kigiriki. Inafanana sana na Injili yake ya kweli isipokuwa kwa vile inaanza bila habari ya nasaba.

Ni lazima tuseme ya kwamba, mistari 52 na 53 ya Mathayo, sura ya 27, ina mafumbo. Kwa kweli, imo kati ya mistari ambayo ni migumu mno kutafsiri katika Maandiko ya Kikristo ya Kigiriki yote. Kwa sababu ni yenye mafumbo hapana mtu awezaye kusema bila sababu inayofaa namna inavyopaswa kutafsiriwa. Jambo linaloongoza kutafsiriwa kwa maandiko kama haya yanayokuwa yenye mafumbo katika maandishi ya awali si shauri la kufuata sana maandishi ya awali yalivyo, kwa sababu yanazuiwa na hali ya kuwa yenye mafumbo. Kuliko hivyo, maelezo, au tafsiri ya Biblia ya maana iliyokusudiwa na mwandikaji wa awali, ndiyo itakayoongoza. Kwa hiyo namna ambavyo kila mtafsiri angetafsiri maandiko hayo ingetegemea ufahamu wake wa Maandiko mengine. Ili kupatana na mengine ya Biblia, mambo ya hakika ya Maandiko yaliyoandikwa juu yanaamua namna yanavyopaswa kutafsiriwa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki