Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w25 Desemba uku. 31
  • Je, Unakumbuka?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Unakumbuka?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2025
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Unakumbuka?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Haraka Inayokupasa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Sehemu ya 1
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Je! Unakumbuka?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2025
w25 Desemba uku. 31

Je, Unakumbuka?

Je, umesoma kwa makini matoleo ya Mnara wa Mlinzi ya mwaka huu? Ona ikiwa unaweza kujibu maswali yafuatayo:

Ni nini kinachotuchochea kumpa Yehova utukufu?

Tunafanya hivyo kwa sababu tunamheshimu sana na tunampenda sana. Pia, tunampa utukufu kwa sababu tunataka wengine wamjue.—w25.01, uku. 3.

Mtu anapotuudhi, tunawezaje kuwa wenye kusamehe zaidi?

Hatutapuuza hisia zetu; hata hivyo, kutokuwa na hasira na kinyongo kunaweza kutusaidia kuepuka kuathiriwa na uchungu.—w25.02, uku. 15-16.

Kwa nini mwanafunzi Marko ni mfano mzuri kwa akina ndugu vijana?

Marko alikuwa tayari kukubali mgawo wa utumishi. Ingawa huenda alivunjika moyo kwa sababu ya hali fulani, Marko hakukata tamaa. Alisitawisha uhusiano wa karibu pamoja na Paulo na Wakristo wengine wakomavu.—w25.04, uku. 27.

Yesu alimaanisha nini aliposali hivi: “Nimewajulisha jina lako”? (Yohana 17:26)

Tayari wanafunzi wake walilijua jina la Mungu. Hivyo, Yesu alimaanisha kwamba aliwafundisha Yehova ni Mungu wa aina gani. Yesu aliwasaidia wanafunzi wake wamjue Yehova vizuri zaidi. Hilo lilitia ndani kuwafundisha kuhusu kusudi, matendo, na sifa Zake.—w25.05, uku. 20-21.

Tunatambua nini ikiwa sisi ni wenye kiasi?

Tunatambua kwamba kuna baadhi mambo ambayo hatujui. Kwa mfano, hatujui mwisho utakuja lini na jinsi ambavyo huenda Yehova akatenda wakati huo. Wala hatujui mambo yatakayotukia kesho na hatuelewi kikamili jinsi Yehova anavyotujua vizuri.—w25.06, uku. 15-18.

Ni nini kinachoweza kutusaidia kunufaika kutokana na makala fulani au hotuba ya watu wote?

Tunaweza kujiuliza hivi: ‘Ni uthibitisho gani unaotumiwa kuwasadikisha wasikilizaji? Je, kuna mfano wenye matokeo ninaoweza kutumia ninapomfundisha mtu mwingine kweli hii? Ni nani atakayependezwa na habari hii?’—w25.07, uku. 19.

Tunajifunza nini kuhusu msamaha wa Mungu kutokana na jinsi alivyoshughulika na Daudi?

Ingawa Daudi alitenda dhambi nzito, Yehova alimsamehe alipotubu kikweli. (1 Fal. 9:​4, 5) Yehova anapotusamehe, hatatuhukumu wakati ujao kwa sababu ya dhambi hiyo.—w25.08, uku. 17.

Ikiwa kuna jambo ambalo ni gumu kwa mwanafunzi wa Biblia kuelewa, unaweza kufanya nini?

Ikiwa bado jambo fulani ni gumu kwake kuelewa hata baada ya kujitahidi kumfundisha vizuri kwa kutumia Biblia, unaweza kuendelea na habari nyingine, kisha upange kulizungumzia jambo hilo wakati mwingine.—w25.09, uku. 24.

Biblia inasema kwamba dhambi ina “nguvu za udanganyifu.” (Ebr. 3:13) Jinsi gani?

Hali yetu ya dhambi inaweza kutushawishi tutende mambo yasiyofaa. Pia, inaweza kutudanganya tuendelee kuwa na shaka, kama vile kutilia shaka ikiwa kwa kweli Mungu anatupenda.—w25.10, uku. 16.

Ni mambo gani matatu yanayoweza kutusaidia kutoa sala zinazotoka moyoni?

(1) Tunaweza kutafakari kuhusu sifa za Yehova. (2) Tunaweza kutafakari kuhusu matatizo tunayokabiliana nayo na kuyataja katika sala, kama vile ikiwa tunahitaji kumsamehe mtu. (3) Tunaweza kutumia muda wa kutosha katika sala. Kuna uwezekano mkubwa zaidi hilo litatusaidia kumweleza hisia zetu za ndani.—w25.10, uku. 19-20.

Tunawezaje kuwasaidia walio na umri mkubwa?

Tunaweza kuwatembelea au kuwapigia simu wenye umri mkubwa. Tunaweza pia kuandamana nao wanapoenda kwa daktari. Au tunaweza kuhubiri pamoja na wale wenye umri mkubwa katika aina mbalimbali za huduma.—w25.11, uku. 6-7.

Harusi ya Kikristo inayoheshimika inapaswa kuwa na mambo gani muhimu?

Tii matakwa yoyote ya kisheria yanayohusika. Jitahidi kutengeneza mazingira mazuri wakati wa hotuba ya ndoa na sherehe ya harusi yanayoonyesha sifa za tunda la roho ya Mungu. Uwe mwenye kiasi inapohusu mavazi yako, na hakikisha kwamba unaepuka desturi zisizopatana na Maandiko. Muwe na mawasiliano mazuri mnapopanga siku yenu ya harusi.—w25.12, uku. 21-24.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki