DOKEZO LA KUJIFUNZA
Dumisha Ratiba Yako ya Kusoma Biblia Kila Siku
Kwa kuwa kuna mambo mengi sana ya kushughulikia, je, ni vigumu kwako kushikamana kila siku na ratiba yako ya kusoma Neno la Mungu? (Yos. 1:8) Ikiwa ndivyo, jaribu mojawapo ya mapendekezo haya:
Jiwekee kikumbusho kila siku. Weka mlio kwenye kifaa chako cha kielektroni utakaokukumbusha kusoma Biblia.
Iweke Biblia mahali panapoonekana. Ikiwa unasoma nakala ya Biblia iliyochapishwa, iweke mahali ambapo unaweza kuiona kwa urahisi kila siku.—Kum. 11:18.
Sikiliza rekodi za sauti. Sikiliza rekodi hizo unapofanya shughuli za kila siku. Tara, ambaye ni painia na mama, na kazi yake ya kuajiriwa ni ya usiku, anasema hivi: “Kusikiliza rekodi za sauti za Biblia ninapofanya kazi za nyumbani kunanisaidia kudumisha ratiba yangu ya usomaji wa Biblia.”
Usikate tamaa. Ikiwa hali zisizotarajiwa zinavuruga ratiba yako, soma angalau mistari michache ya Biblia kabla ya kulala. Hata ukisoma mistari michache kila siku, bado utanufaika.—1 Pet. 2:2.