MACHI 23-29
ISAYA 48-49
Wimbo 89 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)
1. Nufaika kwa Kumsikiliza Yehova
(Dak. 10)
Yehova huwafundisha watumishi wake (Isa 48:17; it “Mwalimu, Kufundisha” ¶2)
Ni lazima tuchague kumsikiliza Yehova (Isa 48:18a; ijwbq makala ya 44 ¶2-3)
Ndipo amani yetu itakuwa “kama mto” na uadilifu wetu “kama mawimbi ya bahari” (Isa 48:18b; lv 199 ¶8)
MAANA: Neno la Kiebrania linalotafsiriwa “amani” linaweza kuleta wazo la afya, usalama, utulivu, nguvu, urafiki, na ukamili.
2. Hazina za Kiroho
(Dak. 10)
Isa 49:8—Unabii huu ulitimizwa kwa njia gani tatu? (it “Wakati Unaokubalika” ¶1-3)
Ungependa kushiriki nasi hazina gani kutoka kwenye usomaji wa Biblia wa juma hili?
3. Usomaji wa Biblia
(Dak. 4) Isa 48:9-20 (th somo la 11)
4. Kuanzisha Mazungumzo
(Dak. 3) MAHUBIRI YASIYO RASMI. Mwalike mtu wa ukoo asiyetenda ahudhurie hotuba ya pekee na Ukumbusho. (lmd somo la 5 jambo kuu la 3)
5. Kufuatia Upendezi
(Dak. 4) MAHUBIRI YASIYO RASMI. Mweleze mtu anayepanga kuhudhuria Ukumbusho mambo anayoweza kutarajia. (lmd somo la 9 jambo kuu la 3)
6. Kufuatia Upendezi
(Dak. 5) MAHUBIRI YASIYO RASMI. Baada ya hotuba ya Ukumbusho, jibu maswali ya mhudhuriaji anayependezwa. (lmd somo la 8 jambo kuu la 3)
Wimbo 107
7. Nufaika na Siku Muhimu Zaidi Katika Mwaka
(Dak. 15) Mazungumzo.
Tunapohudhuria Ukumbusho kila mwaka, tunaonyesha kwamba tunatii amri ya Yesu na tunaonyesha uthamini wetu kuelekea zawadi ya fidia ambayo Yehova ametupatia. (Lu 22:19) Hata hivyo, hii ni pindi muhimu ambayo tunakumbushwa kuhusu jinsi Yehova na Mwana wake wanavyotupenda. (Gal 2:20; 1Yo 4:9, 10) Tunawezaje kunufaika kikamili na uandalizi huu kutoka kwa Yehova? Tunawezaje kuwasaidia wanaopendezwa kufanya hivyo?
Jitayarishe kwa kusoma na kutafakari usomaji wa Biblia wa Ukumbusho kila siku
Tafakari kuhusu zawadi ya fidia na jinsi unavyoweza kuishi kwa njia inayoonyesha kwamba unaithamini
Shiriki kikamili katika kampeni kwa kuwaalika watu unaowafahamu, watu wa ukoo, na wale walio katika eneo lenu kwenye hotuba ya pekee na Ukumbusho
Wakaribishe wageni wanaohudhuria Ukumbusho kwa uchangamfu na kwa urafiki. Huku ukiwakazia uangalifu wale uliowaalika, uwe tayari kuwasaidia wale ambao wamehudhuria kwa sababu walialikwa wakati wa kampeni na uwakaribishe waketi pamoja nawe
Uwe tayari kujibu maswali ya wageni
Uwe tayari kuwaalika wale wasiotenda. Wazee watakuwa tayari kuwakaribisha wale ambao wameondolewa kutanikoni
Onyesha VIDEO Yesu “Alikuja Kutafuta na Kuokoa Kilichopotea.” Kisha waulize wasikilizaji:
Umejifunza nini kuhusu umuhimu wa kuwakaribisha kwa uchangamfu wale wasiotenda kwenye Ukumbusho?
8. Funzo la Biblia la Kutaniko
(Dak. 30) lfb somo la 72-73