Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb26 Machi kur. 6-7
  • Machi 23-29

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Machi 23-29
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2026
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2026
mwb26 Machi kur. 6-7

MACHI 23-29

ISAYA 48-49

Wimbo 89 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)

HAZINA ZA NENO LA MUNGU

1. Nufaika kwa Kumsikiliza Yehova

(Dak. 10)

Yehova huwafundisha watumishi wake (Isa 48:17; it “Mwalimu, Kufundisha” ¶2)

Ni lazima tuchague kumsikiliza Yehova (Isa 48:18a; ijwbq makala ya 44 ¶2-3)

Ndipo amani yetu itakuwa “kama mto” na uadilifu wetu “kama mawimbi ya bahari” (Isa 48:18b; lv 199 ¶8)

Dada akitembea kwenye ufuo wa bahari jua linapozama.

MAANA: Neno la Kiebrania linalotafsiriwa “amani” linaweza kuleta wazo la afya, usalama, utulivu, nguvu, urafiki, na ukamili.

2. Hazina za Kiroho

(Dak. 10)

  • Isa 49:8—Unabii huu ulitimizwa kwa njia gani tatu? (it “Wakati Unaokubalika” ¶1-3)

  • Ungependa kushiriki nasi hazina gani kutoka kwenye usomaji wa Biblia wa juma hili?

3. Usomaji wa Biblia

(Dak. 4) Isa 48:​9-20 (th somo la 11)

BORESHA HUDUMA YAKO

4. Kuanzisha Mazungumzo

(Dak. 3) MAHUBIRI YASIYO RASMI. Mwalike mtu wa ukoo asiyetenda ahudhurie hotuba ya pekee na Ukumbusho. (lmd somo la 5 jambo kuu la 3)

5. Kufuatia Upendezi

(Dak. 4) MAHUBIRI YASIYO RASMI. Mweleze mtu anayepanga kuhudhuria Ukumbusho mambo anayoweza kutarajia. (lmd somo la 9 jambo kuu la 3)

6. Kufuatia Upendezi

(Dak. 5) MAHUBIRI YASIYO RASMI. Baada ya hotuba ya Ukumbusho, jibu maswali ya mhudhuriaji anayependezwa. (lmd somo la 8 jambo kuu la 3)

MAISHA YA MKRISTO

Wimbo 107

7. Nufaika na Siku Muhimu Zaidi Katika Mwaka

(Dak. 15) Mazungumzo.

Tunapohudhuria Ukumbusho kila mwaka, tunaonyesha kwamba tunatii amri ya Yesu na tunaonyesha uthamini wetu kuelekea zawadi ya fidia ambayo Yehova ametupatia. (Lu 22:19) Hata hivyo, hii ni pindi muhimu ambayo tunakumbushwa kuhusu jinsi Yehova na Mwana wake wanavyotupenda. (Gal 2:20; 1Yo 4:​9, 10) Tunawezaje kunufaika kikamili na uandalizi huu kutoka kwa Yehova? Tunawezaje kuwasaidia wanaopendezwa kufanya hivyo?

  • Jitayarishe kwa kusoma na kutafakari usomaji wa Biblia wa Ukumbusho kila siku

  • Tafakari kuhusu zawadi ya fidia na jinsi unavyoweza kuishi kwa njia inayoonyesha kwamba unaithamini

  • Shiriki kikamili katika kampeni kwa kuwaalika watu unaowafahamu, watu wa ukoo, na wale walio katika eneo lenu kwenye hotuba ya pekee na Ukumbusho

  • Wakaribishe wageni wanaohudhuria Ukumbusho kwa uchangamfu na kwa urafiki. Huku ukiwakazia uangalifu wale uliowaalika, uwe tayari kuwasaidia wale ambao wamehudhuria kwa sababu walialikwa wakati wa kampeni na uwakaribishe waketi pamoja nawe

  • Uwe tayari kujibu maswali ya wageni

  • Uwe tayari kuwaalika wale wasiotenda. Wazee watakuwa tayari kuwakaribisha wale ambao wameondolewa kutanikoni

Kisehemu kutoka kwenye video: “Yesu ‘Alikuja Kutafuta na Kuokoa Kilichopotea.’ ” Ndugu na dada wakiwa kwenye Jumba la Ufalme jioni wakati wa Ukumbusho wakizungumza kwa uchangamfu.

Onyesha VIDEO Yesu “Alikuja Kutafuta na Kuokoa Kilichopotea.” Kisha waulize wasikilizaji:

  • Umejifunza nini kuhusu umuhimu wa kuwakaribisha kwa uchangamfu wale wasiotenda kwenye Ukumbusho?

    Kisehemu kutoka kwenye video: “Yesu ‘Alikuja Kutafuta na Kuokoa Kilichopotea.’ ” Dada asiyetenda anahudhuria Ukumbusho, na dada mwingine anamkubatia kwa shauku.

8. Funzo la Biblia la Kutaniko

(Dak. 30) lfb somo la 72-73

Umalizio (Dak. 3) | Wimbo 134 na Sala

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki