Ushuhuda Mkuu wa Ulimwenguni Pote Katika Mwaka wa 1972!
1, 2. Ni kwa kadiri gani, na chini ya usimamizi wa nani, kazi ya mashahidi wa Yehova inafanywa?
HAKUNA shaka juu yake, kazi ya mashahidi wa Yehova leo iko chini ya usimamizi wa Bwana Yesu Kristo aliyetukuzwa. Bila hivyo, isingewezekana kwao kutimiza mengi sana kila mwaka, mara nyingi usoni mwa upinzani mkubwa. Kazi hii inafanywa kama vile Yesu alivyosema ingefanywa.—Mt. 24:14.
2 Utaona inapendeza sana kuangalia tarakimu za ripoti kutoka kila nchi katika ramani inayofuata. Ramani inaonyesha kwamba matawi 95 ya Sosaiti yalipokea ripoti kutoka nchi na visiwa vya bahari 208 ambamo Mashahidi wamekuwa wakihubiri kwa bidii, kutia na nchi kumi na moja ambako kazi yao nzuri imepigwa marufuku na watawala wenye kumpinga Mungu.
3. Kilikuwa kilele gani cha juu sana katika wahubiri kilichofikiwa wakati wa mwaka wa 1972, na wakati wa mwaka ule ule, wangapi walioonyesha wakf wao kwa ubatizo wa maji?
3 Kwa hakika watu wa Yehova ‘wamezidi sana kutenda kazi ya Bwana,’ na matokeo yanaonyesha kwamba haikuwa bure. (1 Kor. 15:58) Walipata kilele kipya katika wahubiri wa Ufalme, jumla ya 1,658,990. Hivyo, mashahidi wa Yehova wamekuwa wakisaidia maelfu waone uhitaji wa kusimama upande wa ufalme wa Mungu na pendeleo lao la kuzihubiri habari njema juu ya serikali hiyo ya kimbinguni iliyosimamishwa kwa wengine. Je! wewe ulikuwa mmoja aliyejifurahisha pendeleo hili na hivyo ukahesabiwa kati ya wasifaji hawa wenye umoja wa Yehova? Ikiwa ndivyo, basi labda ulishiriki katika kusaidia wengine kati ya wapenda haki 163,123 walioweka maisha zao wakf ili wafanye mapenzi ya Yehova na waliobatizwa wakati wa miezi kumi na miwili iliyopita. Hili ni jambo la maana sana, kuwa na wengi sana wakibatizwa katika mwaka mmoja kama ushuhuda wa kwamba wanazifuata sana nyayo za Kielelezo Yesu Kristo.
4. Ni kadiri gani ya wakati uliotumiwa na Mashahidi katika kuhubiri na kufundisha habari njema?
4 Angalia sasa yale ambayo wote hao wanaoshika sana “uzima ulio kweli kweli” waliyoweza kufanya kwa msaada wa Yehova wakati wa mwaka wa utumishi uliopita. (1 Tim. 6:12, 19) Kweli, wamekuwa wenye bidii sana katika kueneza ujuzi wa “neno la uzima.” (Flp. 2:16) Walitumia saa 291,894,945 katika kazi hiyo yenye furaha—wakienda nyumba kwa nyumba, wakifanya ziara za kurudia, wakiongoza mafunzo ya Biblia ya nyumbani, na vivyo hivyo—wakigawa Biblia, vitabu, magazeti na vitabu vingine.
5. Tarakimu zinaonyesha ni kusudi gani katika kuwaachia watu vitabu?
5 Walipoona watu wanaopendezwa, mashahidi hawa wa Yehova walifanya ziara za kurudia 135,898,447 na wakaongoza mafunzo ya Biblia ya nyumbani 1,269,277, mara nyingi pamoja na jamaa nzima zikifaidika na funzo. Kwa jumla, mafunzo haya yanaongozwa kwa watu wale wale kwa muda kama miezi sita kisha mafunzo mapya yanaanzwa. Hivyo labda hesabu ya watu ambao walijifunza nao wakati wa mwaka ni zaidi ya milioni mbili na nusu. Yote haya yanaonyesha kwamba mashahidi wa Yehova wa Kikristo si watu wavivu. Wanaona haraka ya nyakati na kwa bidii wamekwenda ‘kufanya mataifa yote kuwa wanafunzi.’—Mt. 28:19, 20.
6. Jambo gani linaonyeshwa kwa tofauti kubwa katika hesabu ya wale wanaohudhuria Ukumbusho na wale wanaoshiriki mifano?
6 Penye mwadhimisho wao mmoja wa kila mwaka, Ukumbusho wa mauti ya Yesu Kristo, mashahidi wa Yehova walikuwa na jumla ya watu 3,662,407 waliohudhuria ulimwenguni pote. Mwadhimisho huu ulifanywa jioni ya Machi 29, 1972, wakati jua limekwisha kuchwa. Kati ya hesabu hii kubwa, watu 10,350 tu ndio waliojidai kuwa wafuasi waliotiwa mafuta wa Yesu Kristo, wanaotumaini kushirikiana naye katika utukufu wa kimbinguni. (Luka 12:32; 22:19, 20; Rum. 8:16, 17; Ufu. 14:1-4; 20:6) Hii ni punde kuliko sehemu tatu za kumi za persenti moja ya wale waliohudhuria. Kwa hiyo, wengi zaidi kuliko hao wanatazamia kwa furaha uzima wa milele duniani katika taratibu mpya ya Mungu iliyoahidiwa kufuata mwisho wa taratibu hii mbovu ya mambo katika “dhiki kubwa” iliyoko mbele.—Mt. 24:3, 20-22; 2 Pet. 3:13.
7. Ni kwa kadiri gani ujumbe wa ufalme wa Mungu ulienezwa ulimwenguni pote mwaka jana kwa njia ya vitabu?
7 Wahubiri wa ufalme wa Mungu walikuwa na mwaka mzuri sana katika kuangusha vitabu kwa watu, wakifanya iwezekane kwao kusoma na kujifunza Neno takatifu la Mungu Biblia kwa wakati wao wenyewe. Wakati wa miezi kumi na miwili iliyopita mashahidi wa Yehova waliangusha vitabu vikubwa 18,360,561 na vidogo 9,747,270. Walipata maandikisho mapya kwa Mnara wa Mlinzi na Awake! 1,696,260, na kwa kuongeza waligawa nakala moja moja 217,109,764 za magazeti haya bora katika huduma yao.
8. Tarakimu zinaonyesha nini juu ya mapendeleo mbalimbali ya utumishi wa wakati wote wa kuhubiri?
8 Watangazaji wengi wa Ufalme wamo katika kazi ya wakati wote. Wakati wa mwaka uliopita 13,995 walikuwa katika kazi ya upainia wa pekee na utumishi wa umisionari katika ulimwengu wote, na 78,031 walitumikia kama mapainia wa kawaida na wa muda pamoja na makundi ulimwenguni pote. Hawa si wengi kama walivyokuwa mwaka uliotangulia, lakini inatumainiwa kwamba wakati wa mwaka wa utumishi wa 1973 wengi watazifikiria kwa sala hali zao na kuona kama inawezekana kuingia na kujifurahisha ama utumishi wa upainia wa kawaida ama wa muda. Wakifanya hivyo, tutazidi saa nyingi zilizotumiwa kwa kazi ya kuhubiri katika mwaka wa 1971, wakati kilele cha juu zaidi kilipofikiwa. Ijapokuwa tulipungukiwa saa 57,430 mwaka huu, ikilinganishwa na mwaka wa 1971, bila shaka tulikuwa na watu wengi zaidi katika kazi ya kuhubiri na hesabu ya juu zaidi ya watu waliobatizwa.
9, 10. (a) Ni kwa kadiri gani Yehova ameibariki kazi hii ya kuhubiri katika miaka michache? (b) Kwa hiyo, kunatokea ulizo gani, na jibu gani la wazi?
9 Kutokana na muhtasari hii ya ripoti ya utumishi wa mwaka wa 1972 tunaweza kuona kwamba mashahidi wa Yehova duniani pote wanajifurahisha bila shaka baraka nyingi za Mungu ambaye katika jina lake wamechagua kutembea. (Mik. 4:5) Bila shaka yeye anafanikisha kazi yenye furaha ambayo wanafanya kwa sifa yake. Ebu fikiria! Kwa muda wa miaka mitano iliyopita watu 680,871 wameweka maisha zao wakf wafanye mapenzi yake makuu!
10 Je! wewe vile vile unataka uushike sana uzima ulio kweli kweli, uzima wa milele katika dunia ya paradiso? Basi usikawie kushirikiana na wafuasi hawa waliojiweka wakf wa nyayo za Bwana Yesu Kristo. Ndipo, pamoja na wao, wewe vile vile unaweza kushiriki katika ibada na utumishi wa Yehova Mungu.
—Kutoka The Watchtower, January 1, 1973.
[Chati katika kurasa za 308-311]
1972 RIPOTI YA MWAKA WA UTUMISHI WAOF JEHOVAH’S WITNESSES WORLD WIDE
(See bound volume)