Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w73 6/1 kur. 260-262
  • Ambacho Nia Yako kwa Wazazi Wako Inaonyesha

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ambacho Nia Yako kwa Wazazi Wako Inaonyesha
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Habari Zinazolingana
  • Unawaonaje Wazazi Wako?
    Kupata Faida Zote za Ujana Wako
  • Kufurahisha Mioyo ya Wazazi Wako
    Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha
  • Wazazi—Wazoezeni Watoto Wenu Kwa Upendo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Kukadiria Mahitaji ya Wazazi Wako
    Amkeni!—1994
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
w73 6/1 kur. 260-262

Ambacho Nia Yako kwa Wazazi Wako Inaonyesha

Mambo ya hakika ambayo vijana wanataka kujua

JE! WEWE u mtu wa namna gani? Je! unataka kuwa mtu wa namna gani? Njia moja ya kujua ni kuichunguza nia yako kwa wazazi wako.

Je! hilo linapaswaje katika habari hii? Basi, unayosema na kuwafanyia wazazi wako yanaonyesha yaliyo katika akili yako na moyo. Yanaonyesha mengi juu ya namna ya mtu uliye hivi sasa. Yanaonyesha wazi vile vile namna ya mtu utakayekuwa siku zijazo. Hii ni kwa kuwa namna za nia unazokuza katika jamaa zinakuwa sehemu yako wewe.

Vijana wengine wanasitawisha nia isiyofaa juu ya karibu kila watakalo wazazi wao. Wanaona kwamba wazazi wao hawawaelewi, wanafuata mitindo ya kale na hawawezi kutoa uongozi wa kufaa katika ulimwengu huu unaogeuka. Lakini hii inatokeza uasi na inakuwa tabia isipozuiwa. Itajionyesha katika kushughulika na watu wengine wa umri wote walio nje ya jamaa. Inaweza vile vile kumpa mtu shida katika nia yake ya kutii sheria zilizokusudiwa kwa faida ya jamii ya kibinadamu kwa jumla.

Lakini, kunao vijana wengine wasioona hivyo. Wanakua wakiwaheshimu wazazi wao. Vijana hawa wanajua sababu ya ulimwengu kuwa katika shida namna hiyo na yanayowangoja siku zijazo. Kwa hiyo hawakwazwi kujipatanisha na nia zisizofaa ambazo wengine wanazo kwa wazazi wao. Wanajua ubora wa uongozi unaotolewa na wazazi wao. Sababu gani? Kwa sababu vijana kama hao wamelelewa na wazazi wanaoheshimu kanuni za juu zaidi za tabia ya kibinadamu​—zile zinazopatikana katika Neno la Muumba wa mwanadamu, Yehova Mungu​—na wameitikia kwa kushukuru mazoezi hayo. (Efe. 6:4) Kwa sababu ya mazoezi haya katika kweli zinazopatikana katika Neno la Mungu, vijana hawa wanaona ubora wa nafasi yao katika mpango wa jamaa. Kwa hiyo ujamaa mwema unakuwako nyumbani.

Lakini namna gani juu ya vijana walio na wazazi wasiowafunza kanuni za Biblia? Je! hii maana yake ni kwamba hawapaswi kuwaheshimu wazazi wao na kuwatii? Ingawa ni kweli kwamba uongozi wa wazazi utapatwa na madhara unapoacha kanuni za Mungu, bado, hii haipunguzi takwa kwa vijana hawa kukuza nia inayofaa kwa wazazi wao. Sababu gani sivyo? Kunazo sababu nyingi.

Kwa mfano, je! umekwisha fikiria kwa uzito juu ya waliyokufanyia wazazi wako? Kama bado hujaishi peke yako, huenda usifahamu hili kabisa. Lakini simama na ufikiri: tangu kuzaliwa kwako, baba yako na mama yako wamekutunza kila siku. Wamekulisha, kukupa mavazi, nyumba ya kuishi na wamehakikisha unapata elimu.

Kama ingalikupasa kumwandika mtu akufanyie ambayo wazazi wako wamekufanyia tangu kuzaliwa, ungefanikiwa kidogo tu. Wazazi wako, basi, wanastahili heshima kwa hayo yote. Nyumaye, ukioa na kuwa mzazi, utashukuru zaidi sana kwa kadiri ya waliyokufanyia wazazi wako. Lakini sababu gani usionyeshe shukrani yako sasa? Lipa kadiri ya upendo unaowiwa na wazazi wako kwa kuwaheshimu na kuwatii. Ndipo utakapoonyesha kwamba unakua na kuwa mtu aliyekomaa, mwenye busara, anayeona ubora wa wanaomfanyia mema.

Hii si kusema kwamba wazazi wako ni wakamilifu. Ni kweli wanafanya makosa. Lakini, hata wewe unafanya. Inaelekea utafanya mengi zaidi, kwa kuwa huna maono waliyo nayo katika maisha. Je! unashindwa kuyavumilia makosa ya wazazi wako, na hali unataka kwamba wayavumilie yako? Ili upatane, unapaswa kujifunza kuyasahau makosa wanayofanya wazazi wako, kama vile wanavyopaswa kuyasahau mengi unayofanya. Na kwa kuwa wana madaraka mazito zaidi, ni wazi kwamba huenda wakakosa nyakati fulani.​—Zab. 130:3; Yak. 2:13.

Lakini, nyakati nyingine unaloona kama kosa la mzazi huenda yakawa ni maoni yanayotofautiana na yako. Mzazi anamwakilisha mtu aliye juu zaidi yako katika mpango wa Mungu wa mambo. Mungu amewapa wazazi wako uwezo na madaraka usiyo nayo mpaka sasa. Hivyo, maamuzi ya mwisho katika mambo yanayokupasa ni ya wazazi wako. Hiyo ndiyo sababu Neno la Mungu linashauri: “Ninyi watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote; maana jambo hili lapendeza katika Bwana.” (Kol. 3:20) Kweli, hii maana yake ni kutii kila kitu wanachotaka wazazi wako kisichovunja sheria za Mungu.

Unaona, lazima uweko utaratibu katika jamii ya kibinadamu. Pasipo utaratibu, mchafuko, hata ule wa utawala, unatokea. Kwa hiyo, vile vile, lazima uweko utaratibu katika jamaa. Na humo Mungu amemgawia baba kama kichwa, mama naye akishirikiana sana. Wazazi wote wamewekwa kama wasimamizi wa watoto wao. Kwa hiyo wazazi wako wanapokuwekea matakwa fulani, kama vile nyakati unazopaswa kuwa nyumbani wakati wa jioni, wale unaoweza kushirikiana nao, namna unavyovalia, na mambo mengine kama hayo, na unawatii, basi unauheshimu mpango wa Mungu. Usipowatii wazazi wako, huuheshimu mpango wa Mungu. Hiyo maana yake ni kugongana dafurao na Mungu! Na unajua ni nani atakayeumia. Hivyo, unavyoitikia kwa uongozi wa wazazi wako inaonyesha unavyoona juu ya Yeye aliye juu zaidi yao, Yehova Mungu.

Hiyo ndiyo sababu Neno la Mungu linasema: “Jicho la mtu amdhihakiye babaye, na kudharau kumtii mamaye; kunguru wa bondeni wataling’oa, na vifaranga vya tai watalila.” (Mit. 30:17) Ndiyo, nia isiyofaa kwa wazazi itawapotezea vijana maisha zao!

Siku moja, utakapokuwa mwenye umri wa kutosha na labda kupata jamaa yako mwenyewe, ungetaka watoto wako wakuheshimu na kukutii? Lakini ikiwa hujajifunza kufanya hivyo kwa wazazi wako mwenyewe, haielekei kwamba utawazoeza watoto wako kwa kufanikiwa sana katika upande huu. Unavuna unachopanda, Biblia inasema. Jifunze namna ya kufanikiwa katika cheo kidogo ulimo sasa, na hilo litakusaidia kufanikiwa katika madaraka makubwa zaidi ya mtu mzima, na labda ya mzazi, nyumaye.

Vile vile, ukisitawisha nia isiyofaa kwa wazazi wako, inaweza kuonekana katika mambo mengine ufanyayo nyumaye. Kwa mfano, ikiwa unamfanyia kazi aliyekuandika, je! kila mara utaudhiwa na usimamizi wake juu yako? Anapokupa jambo la kufanya, je! utaona ni vigumu kuitikia? Je! sikuzote utalalamika juu ya kazi yako? Namna gani juu ya nia yako kwa wale unaofanya kazi nao? Unaweza kujikuta ukilalamika juu yao sikuzote, pasipo kuwasifu hata kidogo kwa mambo mema wanayokufanyia. Au ukienda shuleni kujifunza kazi fulani, au ndio unazoezwa kazi ile, huenda ukaanza kujiona unajua mengi zaidi ya mwalimu wako. Nia hizi zote huenda zikakuletea huzuni nyingi nyumaye katika maisha. Lakini yanaweza kuwa matokeo ya kuwa ulisitawisha nia mbaya kwa wazazi wako.

Hivyo, ukubali uhakika wa maisha ya jamaa na nafasi yako humo. Shukuru kwamba ndiyo njia ya Mungu, na kwamba njia yake ndiyo iliyo bora.

Lakini ukishindwa kuyakubali madaraka kama kijana katika jamaa, basi unatafuta taabu. Si kwamba tu kukamatana kwako na wazazi wako na wengine kutapaswa, vile vile na maisha yako ya nyumaye; lakini la maana zaidi sana, hali yako mbele za Mungu itadhoofishwa. Na ndiye anayeamua kama utaishi milele katika taratibu yake mpya, au kama utatoweka usionekane tena taratibu mbovu hii ya mambo inapoharibiwa hivi karibuni.​—Mit. 3:1, 2.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki