Kuishiriki Kweli Katika “Siku ya Kushiriki”
◆ Wanafunzi katika darasa la tatu katika shule moja katika Washington, D.C., walikaribishwa washiriki katika “Siku ya Kushiriki.” Katika siku hii iliwapasa wanafunzi waliochaguliwa walete kitu fulani darasani kutoka nyumbani kwao na kukishiriki pamoja na wanadarasa wenzao. Ilipofika zamu yake, Jimmy mwenye umri wa miaka tisa, ambaye mamaye ni mmoja wa mashahidi wa Yehova, alishangaa ataleta nini, ‘atakachoshiriki’ na wanadarasa wenzake.
Kwa ruhusa ya mwalimu wake alileta nakala ya Kutoka Paradiso Iliyopotea mpaka Paradiso Iliyopatikana shuleni, kitabu alichotumia mamaye kwa kumfundisha yeye Biblia. Mwalimu wake alifurahi naye ‘akashiriki’ pamoja na darasa lote sura “Jinsi Mtu Alivyoishi na Kupita Gharika Akaenea Pote Duniani.” Hii ilikuwa yenye kufundisha sana na kufurahisha kwa mwalimu na wanafunzi wengine hivyo kwamba akaendelea kuisoma sura inayofuata, “Mungu Anamwahidi Rafiki Yake Kuzibarikia Jamii Zote za Binadamu.”
Wakati mtu anapojua habari njema zenye kuokoa uhai, je! si jambo lenye busara kuzishiriki na wengine?