Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w73 10/15 kur. 478-479
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Unapaswa Kulipa Kodi?
    Amkeni!—2003
  • Je, Ni Lazima Ulipe Kodi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Jumuiya ya Wakristo Imesaliti Mungu na Biblia
    Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai?
  • “Mkiwiwa Kodi, Lipeni Kodi”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
w73 10/15 kur. 478-479

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

● Je! inawezekana kwamba hali yenye hatari iliyomo katika dini imeletwa na kutofaa kwa Ukristo?​—U.S.A.

Tunapofikiria jibu kwa ulizo hili, imetupasa tukumbuke kwamba kuna tofauti kati ya Ukristo wa makanisa ya Kristendomu na ule wa Biblia. Ingawa namna moja ya Ukristo huenda isifae, hii haingemaanisha kwamba namna ile nyingine lazima isifae vile vile.

Watu wengi wanaamini kwamba kufaa katika dini kunataka kujitia kwa bidii katika maulizo ya kisiasa, ya kijamii na ya matakwa ya watu ya kisasa. Wanaona kwamba kushindwa kwa makanisa kwa habari hii kunaonyesha kwamba haufai.

Lakini je! makanisa ya Kristendomu hayakujitia kwa bidii katika mambo ya ulimwengu? Kweli kweli! Katika nchi nyingi makanisa ya Kristendomu yamezoea uvutano mwingi wa kisiasa, hata kufikia kuutawala ulimwengu. Hata hivyo, makanisa yanadai kuwasaidia walio fukara. Makanisa yamejenga mahospitali, yakaongoza upaji wa sadaka na kuwatia moyo washiriki wao kuwa wenye bidii katika matengenezo ya kijamii. Ingawa faida fulani huenda imeletwa, jitihada hizo zimeleta faida zilizo bora kama inavyowezekana? Je! kwa kweli jitihada hizi zimegeuza maisha za watu, zikitokeza waume bora, wake, akina baba, mama na watoto? Uhakika wa kusikitisha ni kwamba mara nyingi tofauti kidogo sana inaonekana kati ya maisha za washiriki wa kanisa na wasio washiriki wa kanisa. Magereza yamejaa watu wa matengenezo ya kidini. Je! hii haionyeshi kwamba jambo jingine zaidi ya kujitia katika matengenezo ya kijamii na mengine kama hayo linatakiwa?

Mambo ambayo makanisa ya Kristendomu yamefanya ni tofauti na mafundisho ya mwanzilishi wa Ukristo. Yesu Kristo alisema juu ya wanafunzi wake: “Wao si wa ulimwengu.” (Yohana 17:16) Na mtume Yohana aliandika: “Twajua ya kuwa sisi tu wa Mungu; na dunia yote pia hukaa katika yule mwovu.” (1 Yohana 5:19) Kwa hiyo hata iwe inayoelekea kuwa faida imetimizwa, kujitia kwa bidii kwa Mkristo katika mambo ya ulimwengu kungemaanisha kuitegemeza taratibu inayokataliwa na Mungu. Kujitia huko hakuwezi wakati wo wote kupata ukubali wa Mungu na baraka, kama ilivyoonyeshwa vya kutosha na kushindwa mara nyingi kwa wanadamu kuuendeleza ulimwengu. Jitihada za wanadamu zinaweza kulinganishwa na kuyaondoa maji katika meli inayozama kwa kutumia kijiko. Kweli, maji yanaondolewa, lakini jitihada yote haitimizi jambo lo lote la kufaa.

Kwa upande mwingine, aliyoyafanya Yesu Kristo yalikuwa ya kufaa. Aliwapa watu wenye mioyo minyofu kila sababu ya kugeuza njia yao ya maisha kwa faida yao. Aliwasaidia kumjua Mungu kama mtu​—upendo wake mwingi sana, rehema, wema na fadhili zisizostahili. Hii iliwasukuma watu kutaka kuwa waigaji wa Mungu.

Vivyo hivyo, watu leo wanapokuja kufahamu haki ya sheria za Mungu na kufahamu kadiri ya upendo aliouonyesha Muumba kwa kumtoa Mwana wake mzaliwa wa pekee kama ukombozi, wanavutwa kupatanisha maisha zao na amri za Mungu. Wanatimiza onyo lililoongozwa na roho ya Mungu ‘kuvifisha viungo vyenu vilivyo katika nchi, uasherati, uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya, na kutamani.’ Wanaondosha “hasira, na ghadhabu, na uovu, na matukano, na matusi.”​—Kol. 3:5, 8.

Je! si kweli kwamba mambo yangekuwa tofauti sana leo kama watu kila mahali wangekuwa wakifanya vivyo hivyo? Namna hii ingeleta maendeleo katika maisha ya jamaa na kwa ujamaa wa mtu na wanadamu wenzake! Ndiyo, Ukristo wa kweli unafaa kwa kuwa unaweza kuwatokeza watu bora. Na, kama ilivyo wazi kati ya mashahidi wa Yehova leo, Ukristo wa kweli haupatwi na hali yenye hatari bali unafanikiwa​—katika zaidi ya nchi 200 duniani kote.

Kweli, makanisa ya Kristendomu yamo katika hali yenye hatari, lakini si kwa sababu ya kutofaa kwa Ukristo. Ni kwa sababu ya kushindwa kwao kuuiga mfano wa Yesu kujitenga na ulimwengu. Hizi taratibu za makanisa zimetumia wakati wa maana na jitihada kwa kujaribu kuiendeleza milele taratibu ya mambo ambayo imekataliwa na Mungu. Wametia mkazo mwingi katika hekima ya kibinadamu na mambo ya kimwili, hii ikifanya mioyo ya watu isisukumwe kuishi maisha za Kikristo. Hivyo, makanisa ya Kristendomu hayana kilicho bora kutoa kama vile usivyo nacho na ulimwengu wote kwa jumla. Wamelitupilia mbali jambo la pekee linalofaa, yaani, kuwasaidia watu kufahamu usawa na haki ya kuishi kupatana na Neno la Mungu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki