Je! Wewe Unatukuza Viumbe Isivyofaa?
Makala hii ni ya kutumia kwa mafunzo ya kitabu ya kundi
1. Ni hali gani ambayo tunaona juu ya ibada, hata katika Kristendomu?
KATIKA sehemu mbalimbali za ulimwengu tunaona watu wakivipa vitu vya namna zote heshima kuu, kutia na wanyama na wanadamu. Vingine vya hivi vinakubaliwa wazi kama miungu. Vingine haviitwi miungu, lakini sifa na uangalifu na, mara nyingi, utii na ibada inayotolewa kwa hivi inavifanya, kweli, kuwa miungu. Kwa kweli, hata katika Kristendomu, mara nyingi wafuasi wao wanavitolea vitu hivyo utumishi ulio zaidi kupita kuliko kumtolea Mungu mwenyewe ambaye wanajidai kumtumikia.
2. Jambo gani linatokea kwa mtu anayepotoka kutoka kwa ibada ya pekee ya Yehova?
2 Yehova Mungu, Mungu wa Biblia, ni “Mungu mwenye kutaka ibada ya pekee.” (Kut. 20:5, NW) Kupotoka ko kote kutoka kwa uaminifu wote na utumishi wa moyo wote kwa Mungu wa kweli kunaelekea kumfanya mwabudu kupotoka kutoka kwenye utii wa sheria Zake. Nguvu za mtu za kiroho na za adili zinavunjika na polepole yeye anakuwa mwasi wa Mungu na mwabudu sanamu. Mwisho, yeye haukubali tena utawala mkuu wa Yehova na anageuka kuwa adui ya Mungu.
IBADA YA SANAMU KATIKA ISRAELI
3. Hali gani iliyoliuwa ya ibada katika Yerusalemu katika siku za Ezekieli, na Yehova alifanya nini juu yake?
3 Katika Israeli wa kale makuhani na waalimu wa kidini walikuwa wameondoka polepole mbali na Sheria hata ibada ya pekee ya Mungu ikawa imeharibika kabisa. Kwa kweli, hali zilikuwa zimekuwa mbaya sana upesi mbele ya kuharibiwa kwa Yerusalemu kwa Wababeli hata ikawa imekuwa lazima Mungu aache hekalu lake lililokuwa katika Yerusalemu. Lakini hata hivyo, yeye alitaka wote wajue kwamba yeye alijua yaliyokuwa yakitendeka. Tena, Mungu alikuwa akifikiria wanyofu katikati ya Wayahudi, wapate kujua ni kwa sababu gani alikuwa akileta adhabu juu ya taifa. Kwa hiyo alimruhusu nabii wake Ezekieli aone na kufunua mambo ya kuchukiza sana ambayo viongozi walikuwa wakifanya hekaluni.
4, 5. Ni kwenye mahali gani ambako Ezekieli aliletwa kwa njozi, na kwanza aliona nini?
4 Katika njozi, Ezekieli alipelekwa kutoka Babeli kwenda Yerusalemu na alikuwa akiongozwa na Yehova katika utalii wa hekalu huko. Ezekieli anatoa taarifa hivi:
5 “Akanileta hata mlango wa ua; nami nilipoangalia, tazama, pana tundu katika ukuta. Ndipo akaniambia, Mwanadamu, toboa sasa katika ukuta huu; nami nilipotoboa, tazama, pana mlango.”—Eze. 8:7, 8.
6-8. Alipochungulia hekaluni, Ezekieli aliona nini?
6 Ezekieli aliweza kuingia ndani ama kupitia kwa tundu kubwa ama kupitia kwa “mlango” ulio karibu, na kuona yaliyokuwa yakifanyika. Yeye anatuambia hivi:
7 “Akaniambia, Ingia uyaone machukizo mabaya wanayoyafanya hapa. Basi, nikaingia, nikaona; na tazama, kila namna ya wadudu, na wanyama wachukizao, na taswira ya vinyago vyote vya nyumba ya Israeli, zimepigwa ukutani pande zote. Na watu sabini wa wazee wa Israeli walikuwa wamesimama na kuzielekea, na kati-kati yao alisimama Yaazania, mwana wa Shafani; kila mmoja ana chetezo mkononi mwake, na harufu ya moshi wa uvumba ilipaa juu. Kisha akaniambia, Mwanadamu, umeyaona wanayotenda wazee wa nyumba ya Israeli gizani, kila mtu ndani ya vyumba vyake vya sanamu? maana husema, [Yehova] hatuoni; [Yehova] ameiacha nchi hii.”—Eze. 8:9-12.
8 Wazia! Hawa wanaodhaniwa kuwa viongozi wa ibada ya kweli wakitoa heshima kuu kwa vitu vinavyotambaa vyenye kuchukiza sana, vichafu na wanyama kama miungu, ndani ya hekalu la Mungu aliye hai, ambaye alikuwa amewafanya wao kuwa taifa kubwa na akawa amewapa sheria za usafi na haki! Nao walikuwa wametumbukia katika hali hiyo ya moyoni iliyo mbaya sana hata wakafikiri kwamba Mungu Mwenye Nguvu Zote hakuona mambo ya kuchukiza ambayo walikuwa wakifanya.
MAENDELEO YENYE MAGEUZI HATARI
9-11. Watu katika Kristendomu wananaswa namna gani katika namna ya kuabudu wanyama?
9 Je! jambo hilo linawezekana kutukia katikati ya wanaojidai Wakristo? Ndiyo. Kwa kweli, ndiyo mojawapo za hatari kubwa leo. Namna gani?
10 Basi, fikiria, kwa jambo moja, kisio la maendeleo yenye mageuzi, ambalo mamilioni, kutia na wengi wanaokwenda kanisani, wanakubali. Wanaamini nini? Kwamba wao ati walitokana na mdudu mdogo sana katika bahari ya kale sana. Halafu, kutoka kwa mwanzo huo kwa mdudu mdogo sana polepole ukoo wao ukageuka kupitia kwa mageuzi mengi ya kukua, kutoka kwa namna za samaki na viumbe viwezavyo kuishi katika maji na vile vile katika nchi kavu mpaka kuwa wanyama wa nchi kavu, kutoka kwa hao ndiko mwisho mtu alikotoka na akasimama wima—hivyo ndivyo kisio lao lilivyo.
11 Ikiwa ungemwambia mtu kwamba yeye alitokana na jamaa ya nyoka, hapana shaka angetaka kukupiga wewe. Au kama ungesema kwamba babu yake wa ukoo alikuwa nyani mnyama asiye na akili, mnyama kama komba au mbwa, angejiona kuvunjiwa heshima sana. Hata hivyo, kulingana na kisio la maendeleo yenye mageuzi, mtu alitokana na wanyama hao kama babu zake. Kwa hiyo kisio la maendeleo yenye mageuzi linamvunjia mwanadamu heshima hata kumweka katika hali ya wanyama.
12. Kisio la mageuzi yenye maendeleo linageuza ukamatano wa mwanadamu kwa Mungu namna gani?
12 Baya zaidi kuliko hilo, kisio la maendeleo yenye mageuzi linakana kuwako kwa Mungu mwenye akili kupita wote. Au linamwita yeye mwongo wakati Neno lake Biblia linaposema kwamba tangu mwanzo, mtu alifanywa kwa mfano wa Mungu, akiwa na akili bora zaidi kupita wanyama, na uwezo wa kufikiri na sifa za adili na za kiroho. Imani ya maendeleo yenye mageuzi inaongoza watu wa kanisa kuabudu kama muumba, si Yehova Mungu, bali nguvu yenye kukisiwa tu, isiyo na akili ya maendeleo yenye mageuzi, katika umbo la “Mama Asili.” Ni lenye kuvunja heshima na la kukufuru kabisa, na ibada ya sanamu iliyo mbaya sana!
UTUKUZO WA TAIFA, MICHEZO, MABINGWA
13, 14. Je! ni vibaya kwa lazima kutumia wanyama na ndege kwa mfano kufananisha tabia za watu au mataifa?
13 Jambo jingine ambalo ni la werevu hata zaidi linaloweza kuwafanya wanaojidai kuwa Wakristo kupatikana wakiabudu viumbe na wanadamu au vitu vingine kama sanamu liko katika mambo ya utukuzo wa taifa na katika michezo na vitu vya kufurahisha. Katika njia gani?
14 Angalia, kwanza, wanyama wa mwitu na ndege ambao kwa hao mataifa ya Kristendomu yanawakilisha na kufananisha nchi zao. Labda ule mfano wa taifa haufikiriwi sana na raia mmoja mmoja. Na si vibaya kwa lazima kwa vile majina, mara nyingine ya ndege au wanyama, yanachaguliwa ili kuonyesha au kuwa pahali pa taifa. Katika Biblia Yehova kwa mfano anafananisha kuangalia kwake watu wake na kuangalia kwa tai makinda yake, na Yesu Kristo anaitwa “Simba aliye wa kabila ya Yuda,” simba akiwa mfano wa haki yenye uhodari. (Kut. 19:4; Ufu. 5:5) Vile vile mzee Yakobo alitoa unabii juu ya makabila kumi na mawili ya Israeli, akitabiri tabia fulani ambazo wangeonyesha kwa kuwafananisha na wanyama wenye tabia hizi.—Mwa. 49:9, 14, 17, 27.
15. Basi, ni wakati gani mifano hiyo ya mataifa inapokuwa yenye ibada ya sanamu?
15 Walakini, kwa habari ya mifano ya kitaifa, ulizo ni: Je! kuna ibada yo yote inayotolewa kwa mifano hiyo? Ni matokeo ya vitu hivyo juu ya maoni ya watu ndiyo yanayoamua kwamba ibada inatiwa ndani katika mifano hiyo au sivyo. Mawazo na maono yako ya moyoni yanavutwa namna gani wakati unapoina mifano hii? Je! wewe unaona kwamba watu wa kabila au taifa lako ni bora kuliko wengine? Au pahali pake je! wewe unafahamu ukweli wa kwamba Mungu “alifanya kila taifa la wanadamu kutoka katika mmoja” na ya kwamba yeye hana upendeleo wa kabila au taifa lo lote?—Matendo 17:26.
16. Ni kwa kadiri gani washupavu wa michezo wanafika katika kuheshimu timu au mabingwa wao wa michezo ambao wanapenda sana?
16 Katika michezo, wewe unaonaje juu kikoa au timu la mahali pako, au timu ambalo huenda ukapendelea? Leo mabingwa wa michezo ya kushindana wanatukuzwa kama mashujaa (washindi hodari), wafuasi wao wakitamani sana kufuata mfano wao, wanakula chakula kile kile na kuvaa mitindo ile ile ya mavazi. Kunakuwa na makelele makubwa kwa ajili ya majina yao. Mara nyingine magombano makali, hata mapigano makali yanafanywa kwa ajili ya wachezaji au timu, na fedha nyingi zinatolewa.
17. (a) Je! wale wanaotazamwa kama mashujaa ni wabaya zaidi kuliko watu wengine? (b) Ni jambo gani linalofanya iwe ni ibada ya mabingwa hao wa michezo? (c) Ni maulizo gani ambayo huenda yakaulizwa kuonyesha upumbavu wa kuwatazamia wanadamu kwa sababu tu ni wenye nguvu?
17 Jambo hili linakuwa ibada ya sanamu namna gani? Si kwamba kuna lo lote ambalo kwa lazima ni baya juu ya timu au mchezo. Wala “shujaa” mwenyewe hawezi kuchaguliwa peke yake kama ndiye mbaya zaidi kuliko watu wengine. Ni matokeo juu ya mfuasi na maoni yake ndiyo yanayofanya iwe ibada. Kwa sababu tu mabingwa hao wa michezo wanayo miili yenye nguvu na shupavu, je! watukuzwe mno? Zaidi ya uwezo huu, wao ni watu wa namna gani? Je! ni watu ambao mfano wao wa maisha umepaswa ufuatwe? Je! wanazo sifa za upendo, fadhili, imani katika Mungu, furaha, amani, kujiweza? Je! wao wenyewe wanatukuza jina la Mungu au jina lao wenyewe? Tena, bila kujali mtu ni wa namna gani, hakuna mwanadamu ambaye amepaswa atukuzwe mno.
18, 19. Jambo gani linaamua kwamba mmoja anaelekea kwenye ibada ya sanamu katika shauri la michezo ama sivyo?
18 Basi, ikiwa mtu anapoteza wakati mwingi na jitihada, akijifunza kwa uangalifu habari zote za hesabu na wastani za timu mbalimbali na wachezaji, kupendezwa kwake sana na kujitoa kuko wapi? Anapendezwa namna gani juu ya kujifunza zaidi juu ya kusudi la Mungu?
19 Ulizo ni: Kwa kweli mtu anafikiria sana juu ya nini? Yeye anapenda kufanya, kutazama, kusoma juu ya nini? Ni jambo gani ambalo yeye anaona ni bora? Yesu alisema: “Kwa kuwa hazina yako ilipo, ndipo utakapokuwapo na moyo wako.”—Mt. 6:21.
20. Ni tofauti gani kati ya bidii yenye shauku inayofuatana na ibada ya kweli na ile inayofuatana na michezo?
20 Katika kumwabudu na kumtumikia Yehova Mungu hakuna mambo ya kupita kadiri. Kweli, kuna furaha, kuna bidii, kuna shauku. Lakini yote yanatokeza kilicho chema, na ni chenye msaada kwa wengine. Uwazimu na mambo ya kupita kadiri yanayofanywa na watu wengi sana wenye kupenda michezo na wachezaji ni ushuhuda wa kwamba wanatukuza mno mchezo au wachezaji wake. Ebu chukua, kwa mfano, mara zile wafuasi washupavu wanapowatupia wachezaji au wakuu wa michezo chupa, na kupata hasira ya wazimu, wakivunja-vunja majani ya uwanjani na vifaa nyuma ya mchezo wa mpira wa kupiga kwa vibao au kwa miguu.
21, 22. Inaonekana namna gani kuwa na kufanana kati ya michezo ya kale ya Kirumi na michezo fulani leo?
21 Je! ye yote anayejidai kuwa Mkristo angefurahia mapigano yanayotokea katika viwanja vya michezo, ya mtindo wa Kirumi? Je! hakuna kufanana kwa michezo mingi, zaidi ile michezo ya leo ya karibu-karibu, kama vile mpira wa kupigwa kwa miguu, kupigana ngumi na mpira wa vingoe (hockey)?
22 Kwa mfano, katika mchezo wa mpira wa kupigwa kwa miguu kwa ajili ya uchumi kuna kinachoitwa “kikosi cha kujiua,” kikundi kinachopelekwa kwa pekee katika mchezo, kama gazeti Life lilivyosema, “kikiwa na kazi zenye jeuri kufanya.” Takwa kwa wanachama wa kikosi cha kujiua, gazeti Life linaeleza, ni “tabia za kikatili na bila kuogopa hata kidogo.” Mchezaji mmoja alisema hivi: “Mimi ninafikiria tu kumwumiza mtu mwingine, kwa sababu kila unapopigwa teke mpaka kuzimia, unaweza kutegemea kupiga teke watu wawili au watatu mpaka kuzimia. Hayo ndiyo maoni mazuri sana.”
23. Mtu anayehatirisha afya yake mwenyewe na kuhatirisha wengine katika mashindano ya michezo ni mwabudu wa sanamu namna gani?
23 Wakati mtu anapohatirisha, si afya yake mwenyewe, bali vile vile anajaribu kuumiza, labda kulemaza au kuua wengine ili kushinda mchezo kwamba ni kwa kutaka fedha, sifa, utukufu au kingine cho chote, je! hii si namna ya ibada ya sanamu juu ya mchezo huo? Kwa hakika ni kufikiri zaidi juu ya utukufu wa mtu mwenyewe kuliko kufikiria mwenzake, ambaye Mungu aliumba. Ni kutokumtii Muumba kwa wazi na ni kutumikia kitu kingine kama mungu, kama kinachostahili kuabudiwa na mtu na jitihada yake.
24, 25. Katika michezo yote, kwamba ni yenye kuumiza au sivyo, inampasa Mkristo ajilinde juu ya nini?
24 Bila shaka, si michezo yote ni yenye kuumiza, lakini mchezo wo wote ambao anaweza kupendelea, imempasa Mkristo ajiangalie usije ukachukua moyo wake kwa kadiri ambayo unaanza kuchukua wakati na uangalifu kutoka kwa funzo la Neno la Mungu kumtumikia Yeye.
25 Na hatuwezi kuchagua michezo peke yake kama jambo fulani liwezalo kuwa sanamu. Ikiwa sisi tunatazama mabingwa wa michezo wa televisheni au sinema, wapiga muziki, waimbaji au mabingwa wengine kwa woga wa kuheshimu au kutumia wakati mwingi mno tukiwatazama au kuwasikia, tunaiacha ibada ya Mungu kwa kuwapendelea wao.
ANGALIA HALI YA MOYO WAKO
26, 27. Nabii Ayubu alionyesha namna gani kwamba mtu anaweza kufanya dhambi ya ibada ya sanamu katika moyo wake?
26 Kwa hiyo, tunaweza kushiriki katika ibada ya sanamu ikiwa kwa shauku nyingi mno tunasaidia mambo haya ambayo katika hayo wanadamu wanatukuzwa, ikiwa tunatoa kwao mioyo yetu. Ikiwa hatuonyeshi waziwazi maoni hayo, ni lazima tuangalie hali yetu ya moyoni na moyo wetu. Kwa maana nabii wa kale Ayubu alionyesha kwamba mtu anaweza kuwa na hatia ya ibada ya sanamu ndani sirini mwa moyo wake mwenyewe. Alisema hivi:
27 “Kama nililitazama jua lilipoangaza, au mwezi ukiendelea katika kung’aa; na moyo wangu umeshawishwa kwa siri, na midomo yangu imeubusu mkono wangu; hilo nalo lingekuwa uovu wa kuadhibiwa na waamuzi; kwani [ningemkana Mungu wa kweli] aliye juu.”—Ayubu 31:26-28.
28. Yesu alisema namna gani juu ya lazima ya kujilinda sikuzote juu ya vishawishi vya werevu?
28 Ikiwa tunashawishwa katika moyo wetu kuwa na mapendo kwa kiumbe au kitu cho chote ambacho kinaondoa ibada yetu ya pekee kwa Mungu, kinakuwa sanamu kwetu na dhambi juu ya Mungu. Inafaa kukumbuka nyakati zote maneno ya Yesu yanayoonyesha hatari kubwa ya kuacha mioyo yetu ishawishwe na cho chote ambacho huenda kikatuvutia katika mwendo wa kumwasi Mungu. Alionya wanafunzi wake hivi: “Moyoni hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati, wivi, ushuhuda wa uongo, na matukano.” Tena alionyesha kwamba moyo wa mtu unaweza kumnasa mtu katika kufanya dhambi juu ya Mungu wakati aliposema hivi: “Mimi nawaambia, Kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake.”—Mt. 15:19; 5:28.
29. Kujizoeza kwa kimwili kuna mahali gani panapofaa katika maisha ya kimwili?
29 Vitu vya kufurahisha na mazoezi ya maungo ya mwili ni vizuri vikiwa mahali pao panapofaa. Mtume Paulo aliweka mambo katika utaratibu wao unaofaa wakati aliposema hivi: “Ujizoeze kupata utauwa. Kwa maana kujizoeza kupata nguvu za mwili kwafaa kidogo, lakini utauwa hufaa kwa mambo yote; yaani, unayo ahadi ya uzima wa sasa, na ya ule utakaokuwapo baadaye.”—1 Tim. 4:7, 8.
30.Wakristo wanatoa utukufu kwa vitu vingine kuliko kwa Mungu wanaangukia katika hali gani mbaya ya moyoni?
30 Basi tunaweza kuona kwamba njozi za Ezekieli zinatumika kwa nguvu sana leo. Kama vile Waisraeli fulani walivyonaswa, ndivyo na wengi wanaojidai Wakristo. Wakiisha kuvutwa katika ibada ya wanyama na sanamu nyingine, watu hao wa Israeli walifikiri ‘Yehova hakuwaona,’ kwamba wasingeletwa katika hukumu. Leo, ingawa Wakristo wanajua kwamba Yehova ni “mwenye kutaka ibada ya pekee” na kwamba ‘yeye hatampa mwingine utukufu, wala sanamu za kuchonga sifa yake,’ wengine wanajiachilia wenyewe kuvutwa katika mazoea ya ibada ya sanamu.—Isa. 42:8.
31. Mtume Yohana anaonyesha namna gani kwamba kutaka utukufu au kuwatukuza wanadamu ni shughuli ya bure
31 Kwa hiyo, Mkristo wa kweli lazima ajilinde juu ya mtego huo wa werevu sana, “kiburi cha uzima,” ambacho, mtume Yohana anasema, hakitokani ‘na Baba, bali chatokana na ulimwengu.’ Kutaka kujitukuza mwenyewe au kuwatukuza wanadamu kutamwingiza mtu katika ibada ya sanamu. Nao ni utukufu unaopita. Yohana anaendelea kusema: “Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele.”—1 Yohana 2:16, 17.
—Kutoka Kitabu ”The Nations Shall Know that I Am Jehovah”—How?