MHUSIKA KATIKA BIBLIA
Manaeni—Alitanguliza Mambo ya Kiroho
Manaeni alikuwa miongoni mwa wale walioongoza mambo katika kutaniko la Antiokia la karne ya kwanza. ‘Alielimishwa pamoja na Herode mtawala wa wilaya.’ (Mdo. 13:1) Hivyo, Manaeni alikuwa na elimu ya juu na huenda alilelewa katika familia ya kitajiri.
Licha ya malezi yake, Manaeni aliamua kuwa Mkristo na kuliunga mkono kutaniko. Hakutumia elimu aliyokuwa nayo au uhusiano wake pamoja na watawala ili kujinufaisha mwenyewe. Badala yake, aliwatumikia ndugu zake.
Mfano wa Manaeni unaonyesha kwamba kumtumikia Yehova ni muhimu zaidi kuliko kufuatia umashuhuri katika ulimwengu huu. Kama Manaeni, tunapaswa kutanguliza utendaji wa kiroho, badala ya kufuatia utajiri au umashuhuri katika ulimwengu. (Mt. 6:33) Kwa kuongezea, ingawa tunathamini elimu, ‘tunahakikisha mambo muhimu zaidi’ na kuhakikisha kwamba utendaji mwingine katika ulimwengu huu hauingilii ibada yetu kwa Yehova.—Flp. 1:9, 10.