DOKEZO LA KUJIFUNZA
Jinsi ya Kuelewa Lugha ya Picha Katika Biblia
Biblia inatumia mara nyingi lugha ya picha. Hata hivyo, ni vigumu kwa wasomaji wengi wa Biblia kuelewa lugha hiyo ya picha. (Mt. 13:13) Ni nini kinachoweza kukusaidia kuelewa mifano hiyo inayotumiwa katika Biblia? Jaribu mambo yafuatayo:
Tambua habari inayozungumziwa na picha inayotumiwa. Lugha za picha zinalinganisha habari fulani na picha. Kwa mfano, Ufunuo 3:3 inalinganisha kuja kwa Yesu (habari) na kuja kwa mwizi (picha).
Tambua jinsi habari inayozungumziwa inavyofanana na picha hiyo. Tafuta mambo na sifa zinazofanya habari na picha hiyo zifanane.
Fikia mkataa ulio sahihi. Baadhi ya mambo yanayofanana kati ya habari inayozungumziwa na picha, yanaweza kusababisha tufikie mkataa usio sahihi. Katika mfano uliotajwa awali, Yesu haji kuiba chochote. Badala yake, muktadha unaonyesha kwamba kuja kwake kutakuwa kama kuja kwa mwizi katika maana ya kwamba kuja kwake kutakuwa bila kutarajiwa au kutangazwa.