DOKEZO LA KUJIFUNZA
Piga Picha Akilini Unaposoma Masimulizi ya Biblia
Biblia ina masimulizi mengi yanayofundisha masomo muhimu. Kwa kupiga picha akilini masimulizi hayo, tunaweza kuelewa vizuri zaidi mambo tunayosoma na kunufaika zaidi kutokana nayo. Fikiria baadhi ya madokezo yanayoweza kukusaidia kupiga picha akilini unaposoma masimulizi ya Biblia.
Soma kwa sauti. Kusoma Biblia kwa sauti kunaweza kukusaidia kupiga picha vizuri zaidi akilini. Mnaposoma Biblia mkiwa familia, mnaweza kulifanya simulizi hilo liwe halisi kwa kumgawia kila mtu asome sehemu za wahusika mbalimbali wanaotajwa katika simulizi.
Wazia hali au matukio yanayotajwa. Jaribu kuelewa mawazo na hisia za wahusika wanaotajwa. Kwa mfano, jiulize hivi: ‘Kwa nini mtu huyu alizungumza au kutenda kwa njia hii? Ningefikiria nini au ningehisije ikiwa ningekuwa katika hali hiyo?’
Chora. Kuchora matukio yanayotajwa katika Biblia kunaweza kukusaidia kupiga picha akilini na kukumbuka masimulizi vizuri, hata kama hujui kuchora vizuri.