Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w25 Septemba uku. 32
  • Yesu “Alijifunza Kutii”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yesu “Alijifunza Kutii”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2025
  • Habari Zinazolingana
  • “Alijifunza Kutii”
    ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
  • Jifunze Utii kwa Kukubali Nidhamu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Je, Una ‘Moyo Mtiifu’?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Utii Je, Ni Somo Muhimu Utotoni?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2025
w25 Septemba uku. 32

MSEMO WA BIBLIA

Yesu “Alijifunza Kutii”

Sikuzote Yesu amemtii Yehova. (Yoh. 8:29) Basi, kwa nini Biblia inasema: “Alijifunza kutii kutokana na mateso yaliyompata”?—Ebr. 5:8.

Yesu alipokuwa duniani, alikabili hali ambazo mbinguni hazikuwepo. Alilelewa na wazazi waliompenda Yehova lakini ambao hawakuwa wakamilifu. (Luka 2:51) Aliteswa na viongozi wa dini wenye ufisadi na watawala wasiotenda kwa haki. (Mt. 26:59; Marko 15:15) Kwa kuongezea, “alijinyenyekeza na kuwa mtiifu mpaka kifo,” kifo chenye maumivu makali.—Flp. 2:8.

Hali hizo alizopitia Yesu, zilimfundisha utii kwa njia ambayo hakuwahi kamwe kujifunza alipokuwa mbinguni. Hivyo basi, angeweza kuwa Mfalme na Kuhani Mkuu mkamilifu, ambaye angeweza kuusikitikia udhaifu wetu. (Ebr. 4:15; 5:9) Yesu alikuwa mwenye thamani zaidi kwa Yehova baada ya kujifunza utii kutokana na mateso aliyopitia. Sisi pia tunaweza kuwa wenye thamani zaidi kwa Yehova na anaweza kututumia zaidi kwenye mgawo wowote ambao atatupatia ikiwa tutaendelea kuwa watiifu chini ya hali zozote ngumu.—Yak. 1:4.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki