MSEMO WA BIBLIA
Yesu “Alijifunza Kutii”
Sikuzote Yesu amemtii Yehova. (Yoh. 8:29) Basi, kwa nini Biblia inasema: “Alijifunza kutii kutokana na mateso yaliyompata”?—Ebr. 5:8.
Yesu alipokuwa duniani, alikabili hali ambazo mbinguni hazikuwepo. Alilelewa na wazazi waliompenda Yehova lakini ambao hawakuwa wakamilifu. (Luka 2:51) Aliteswa na viongozi wa dini wenye ufisadi na watawala wasiotenda kwa haki. (Mt. 26:59; Marko 15:15) Kwa kuongezea, “alijinyenyekeza na kuwa mtiifu mpaka kifo,” kifo chenye maumivu makali.—Flp. 2:8.
Hali hizo alizopitia Yesu, zilimfundisha utii kwa njia ambayo hakuwahi kamwe kujifunza alipokuwa mbinguni. Hivyo basi, angeweza kuwa Mfalme na Kuhani Mkuu mkamilifu, ambaye angeweza kuusikitikia udhaifu wetu. (Ebr. 4:15; 5:9) Yesu alikuwa mwenye thamani zaidi kwa Yehova baada ya kujifunza utii kutokana na mateso aliyopitia. Sisi pia tunaweza kuwa wenye thamani zaidi kwa Yehova na anaweza kututumia zaidi kwenye mgawo wowote ambao atatupatia ikiwa tutaendelea kuwa watiifu chini ya hali zozote ngumu.—Yak. 1:4.