Hakuna Malalamiko Zaidi Juu ya Ule Muziki
Majirani walikuwa wakilalamika juu ya ule muziki unaopigwa kupitia mfumo wa vikuza-sauti kwenye shule moja ya sekondari iliyo ya vidato vya chini katika Fukuoka Prefecture, Japani. Ndipo kijana mmoja alipopeleka shuleni kaseti za Kingdom Melodies. Baada ya kuzisikiliza, mwalimu alisema: “Huu ni muziki mzuri. Unaweza kuzipiga kanda hizo katika mfumo wa vikuza-sauti vya shule.” Tangu wakati huo wanafunzi, walimu, na hata majirani wamekuwa wakisikiliza hizo Kingdom Melodies kwa dakika 10 kila asubuhi na dakika 25 nyakati za mapumziko ya chakula cha mchana. Na kumekuwa hakuna malalamiko zaidi juu ya ule muziki!
Wewe pia unaweza kunufaika kutokana na hiyo mipangilio ya kimuziki inayoburudisha. Kila moja ya kaseti hizo, Kingdom Melodies 1, 2, 3, 4, 5, 6, 7, na 8, ni Kshs. 32.00 (Tshs. 160.00) tu. Pokea kaseti zilizoorodheshwa chini kwa kujaza na kutupelekea hati yenye anwani iliyoambatanishwa.
Tafadhali mnipelekee, mkiwa mmelipia malipo ya posta, kaseti iliyotiliwa (zilizotiliwa) alama hapa chini. Kwa kila kaseti ambayo mimi nimeagiza, nimewapelekea ninyi Kshs. 32.00 (Tshs. 160.00) ili kulipia gharama.
◻ Kingdom Melodies 1 ◻ Kingdom Melodies 2 ◻ Kingdom Melodies 3 ◻ Kingdom Melodies 4
◻ Kingdom Melodies 5 ◻ Kingdom Melodies 6 ◻ Kingdom Melodies 7 ◻ Kingdom Melodies 8